Pinda alishamuahidi Dr. Ulimboka alipokuja CPL kuwa atapata matatizo

acha ujinga wewe....usilete pumba zako na kuvuruga amani ya nchi. Usionge vitu usivyo kuwa na ushahidi navyo. Bora ukae kimya..waachie polisi wafanye kazi yao.
Yawezekana kweli muanzilishi wa thread ameongea bila ushahidi
Ila na wewe unaongea utumbo kudai polisi waachiwe hili
Tume huru pekee ndio itakayoachiwa na watu wakaridhika na matokeo ya uchunguzi wao
Credibility ya polisi ilishapotea kitambo
 
hivi kweli hayo maneno yalisemwa na waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa tanzania??

ndiyo, alisema kwenye ukumbi wa central pathology labolatory - MNH alipokuja kuwapotosha madaktari bada ya kubanwa na kamati ya magreth sita Bungen. Pindi ni km Rubi....sh ktk nafasi ya uwaziri mkuu.
 
acha ujinga wewe....usilete pumba zako na kuvuruga amani ya nchi. Usionge vitu usivyo kuwa na ushahidi navyo. Bora ukae kimya..waachie polisi wafanye kazi yao.

Wewe ndio mjinga kwakuwa hujui ulisemalo wala unalolitenda. nikiwa mtanzania mzalendo ninaemuogopa Muumba wa mbingu na dunia, nimehuzunishwa sana na hili tukio la dr Ulimboka. Mungu akuponye dr Ulimboka na mungu atawaumbua hawa wote (serikali ) waliofanya kitendo hiki. Hawa ni sawa na mashetani
 
Mnakumbuka kauli ya Pinda kwa waliokuwa CPL -MNH siku hiyo.? . . .nanukuu. .

Ulimboka
: Tunaomba kusiwe na victimization ya aina yoyote. .

Pinda: Hakutakuwa na victimization lakini mkikuta kapigwa na majambazi au kagongwa na gari msiseme ni serikali' mwisho wa nukuu

Duh, JF kweli ni noma yaani ni GT, alimwahidi hivyo? Basi mpango ulianza kusukwa toka siku hiyo Pinda amesema hivyo. He should be held responsible.
 
Watanzania msilalamike! Mliyataka wenyewe!! Acheni serikali ifanye kazi yake! Hiyo serikali mnayoilalamikia mliiweka madarakani wenyewe. Mkatanguliza ushabiki wa Yanga na Simba katika siasa bila kujali uhalisia wa mambo. Sasa tulieni mnyooshwe vizuri hadi hapo mtakapopata akili 2015.
 
naona yalio tokea libya , na syria sasa yanakuja tanzania ..utabiti wa mrema....

huko libya wakundi ya kutumika walikua wakiua watu then akisingiziwa ghadafi na serikali yake..hatimae tunajua kilichofata...
na huko syria wauaji walio funzwa vyema wanauwa vichanga , watoto na wanawake then wanasingiziwa majeshi ya serikali...propaganda zinapigwa dunia nzima kwamba serikali ya Bashar assad inaua...mbona huko nyuma hajamuua hata sisismizi ?
mbinu hizi zilitumika sehemu nyingi ..lengo kuifanya jamii waichukie serikali yao....
naomba serikali ichuke tahadhari kubwa na kufanya uchunguzi wa kina na pia ushauri wa mrema na kauli yake kwamba aliwahi kuitwa na ubalozi mmoja ili kufanya mambo kama haya lakini mrema alikua shujaa na mzalendo halisi akakataa.

hakuna mantiki kwa serikali au pinda au kikwete kuwa wanahusika...serikali sana sana ingewafukuza hawa madaktari na kuwapiga marufuku kufanya shughuli yoyote ndani ya nchi.basi ingetosha kuwa ni adabu ya kwao kugoma kwa sababu za kisiasa.
tujihadhari...

Wewe nafikiri upo kwenye sayari ya pekee yako, kama unathubutu hata kusema kuwa serikali ya Asad ilikuwa haiui wananchi wake siku za nyuma, nadhani hatuna haja ya kubishana nawe. Serikali ya Syria ambayo hata Jumuia ya kimataifa ilikuwa ikijua siku nyingi juu ya uwezo wake wa kuua raia wake mpaka wa nchi jirani. Ni Syria ndiyo iliyokuwa ikitekeleza mauaji mpaka ndani ya Lebanoni dhidi ya wananchi waliokuwa wakionekana kupinga makundi ya kiislam yenye msimao mkali kama Hamasi.
 
Kwa kauli hiyo na uhitaji wa kupoteza ushahidi unaoweza jitokeza sasa basi ni wakati wa madaktari kujilinda. Kwa sasa wawe kwenye zamu sio tu ya kutibu ila hata wao kwa wao waangaliane kwa mashaka maana inaweza kuwa movie story sasa hivi. Maadam yuko mikononi mwa madaktari wenzake basi uwezekano wa kupona--- na Kwa neema ya Mungu ni mkubwa. Hakikisheni nani anampa dawa, nani anashughulikia vipimo, nani anachoma sindano etc. najua dr. ni professionals, ila hapo wanaweza kuwepo professionals wengine 'intelijensia' Be at alert!
 
madaktari wamegoma wako nyumbani au wanaripoti ila hawafanyi kazi? Wale waliompiga afsa usalama waliingiaje? Na kama wanaingia wakiwa kwenye mgomo mmmh, mwe!
 
damu yake itatoa majibu kwa serikali.

na ifahamike hakuna ukombozi wa kweli bila umwagaji damu, ule uhuru aliopewa mwalimu ni usanii tu sasa huu unaokuja ndio wa kweli, msiogope kufa kwani ndo gharama ya ukombozi wa kweli na ndo tutaheshimiana vema kwa kuwa tumeshatambua gharama ya ukombozi wa kweli. Kwa wale wakristu tunaamini kabisa kuwa yesu pia alibidi afe kwa kumwaga damu ili ukombozi wa mwanadamu kutoka dhambini utimie...sembuse sisi wanadamu...huu ndo ukweli na dawa halisi..hata kama ni chungu ili tupone lazima tuinywe.
 
Ukisha ona serikali inayo victimize viongozi wa vyama vya wafanyakazi, jua kwamba mwisho wa serikali hiyo umekaribia.
 
Wewe nafikiri upo kwenye sayari ya pekee yako, kama unathubutu hata kusema kuwa serikali ya Asad ilikuwa haiui wananchi wake siku za nyuma, nadhani hatuna haja ya kubishana nawe. Serikali ya Syria ambayo hata Jumuia ya kimataifa ilikuwa ikijua siku nyingi juu ya uwezo wake wa kuua raia wake mpaka wa nchi jirani. Ni Syria ndiyo iliyokuwa ikitekeleza mauaji mpaka ndani ya Lebanoni dhidi ya wananchi waliokuwa wakionekana kupinga makundi ya kiislam yenye msimao mkali kama Hamasi.

Kaka huyo macos, ni miongoni mwa wale tunaowaita slow thinkers, au short minded, kwani yeye anadhani madaktari wanagoma kwa sababu za kisiasa. kwani kuna anaegombea urais au ubunge? au ndo hao waliotekeleza utekaji wa steven ulimboka nini? wanajiita utawala bor eti...aibu kubwa hata kama ni mpango wa serikali bado umeonesha udhaifu huwezi kufanya tendo kama hilo wakati kama huu, kiongozi dhaifu, mipango dhaifu, idara dhaifu, dhaifu dhaifu dhaifu dhaiffffuuuuu
 
mnakumbuka kauli ya pinda kwa waliokuwa cpl -mnh siku hiyo.? . . .nanukuu. .

ulimboka
: Tunaomba kusiwe na victimization ya aina yoyote. .

pinda: Hakutakuwa na victimization lakini mkikuta kapigwa na majambazi au kagongwa na gari msiseme ni serikali' mwisho wa nukuu

bila shaka hata mpango anaujua, kwani nae si katokea huko huko, ndo mambo ya kuangalia, wenzetu wazungu ukikuta mtu intelligence ni intelligent kweli kweli, sasa sisi kama intelligence yenyewe ndo kama yakina pinda....du! Tujipe poleeee! Lakini ndivyo ilivyo ni majungu tu hakuna kitu wanafanya. Kama kweli ni hodari ile issue ya ubalozi wa marekani wangezuia...pale ndo kipimo kama tuna intelligence au watu wa majungu tu. Haya mtandao wa madawa yakulevya mbona hawajafanya chochete, wahamiaji haramu wa kisomali mbona wanaingia kila siku tena hapo hapo ikulu kwenye mlango wa bahari mbona hatujasikia wanakamatwa, hakuna kitu ni majungu tuuuuu
 
Back
Top Bottom