Pinda akerwa na ‘ujeuri’ wa Barrick

Huyu Barrick jeuri yake inatokana na rais wetu kukubali kuhongwa. Hawa walisema mtatufanya nini, hata rais wenu tunamhonga? What do you expect?

Chunguzeni uhusiano wa mzungu anaitwa SinClair , Barrick gold na mkweree ndio mtajua jeuri yao wanaitoa wapi!! Pinda anajishaua shaua tu hajui kinachoendelea nyuma ya pazia mwisho wake atakuja kalipiwa na bosi wake. Ikumbukwe tu kwamba corporate social responsibility haiwalazimishi wawekezaji kuwasaidia vijiji jirani ni hiari yao kiasi gani watasaidia; wangetaka iwe lazima serikali ingehakikisha kwenye mikataba ya uwekezaji nchini inawekwa wazi ni kwa aslili mia ngapi ya faida migodi inayopata kila mwaka itumie kwa misada hiyo.
 
Chunguzeni uhusiano wa mzungu anaitwa SinClair , Barrick gold na mkweree ndio mtajua jeuri yao wanaitoa wapi!! Pinda anajishaua shaua tu hajui kinachoendelea nyuma ya pazia mwisho wake atakuja kalipiwa na bosi wake. Ikumbukwe tu kwamba corporate social responsibility haiwalazimishi wawekezaji kuwasaidia vijiji jirani ni hiari yao kiasi gani watasaidia; wangetaka iwe lazima serikali ingehakikisha kwenye mikataba ya uwekezaji nchini inawekwa wazi ni kwa aslili mia ngapi ya faida migodi inayopata kila mwaka itumie kwa misada hiyo.
Hapo kwenye red, Umetutamanisha mkuu, mwaga data tafadhari mkuuuuuuu
 
Hivi atawaombaje wakutane? Anatakiwa kuwaita na si kuwaomba as a PM. What a shame!!!!!!
huyu anaenda kuchukua gold hana kitu, alisema mafisadi wanapesa ni hatari kwa taifa sasa anawezaje kukohoa kwa hawa mult billion company
mpuuzi tu huyu wewe ale hapo atulie

PM anashitaki wawekezaji kwa wananchi ili kiwe nini?
PEOPLE POWERS pinda anajua timu ya ushindi ni wananchi sio hiyo ya mafisadi ili ujinga ndio unasumbua hapa

msipoangalia ataanza kulia sasa hivi
kikwete kamnunua kwa hicho cheo ili amtumie kama sabuni

Kwa hadhi yake hakupaswa kulalamika. Alitakiwa kuchukua hatua. Kwa namna hii ndiyo maana serikali inaonekana kuwa dhaifu.

Lowasa alishawashitukia hawa akawambia BUNGENI kwa ni serikali legelege wacha wamvamie kwa matusi,
hakuna mchapakazi serikalini kuna wagonjwa tu wanasubilia kwende kutibia INDIA kwa kodi za wananchi in fact wako madarakani kwa sababu ya afya zao mbovu
 
Hili zee nalo lina sura ya kazi lakini mwoga kama kunguru.
Ndio maana watu kama hawa wanapo staafu watu hujitoa mhanga na kuwazaba vibao mbele ya hadhira kumbe huwa wanajitakia wao wenyewe.
 
Tatizo siyo wawekezaji, bali ni hao waliowaweka. Huyo pinda naye aache siasa tunataka achukue hatua kisha atuambie kuwa kachua hatua hizo kutokana na kukerwa siyo kutafuta cheap popularity for doing nothing
 
Kama wewe Pinda Peter Kayanza Pinda unasoma hii Thread elewa sisi Watanzania tunakujua huna maamuzi na wewe ni Mnafiki sana.
 
In short Barrick alishaiweka mfukoni serikali ya Tanzania hakuna kiongozi wa kufurukuta hata Pinda yupo ndani ya mfuko hapo anaongopea wanaMara kwa unafiki hata lolote na matatizo kwenye migodi yote yanajulikana na wananchi hawana mtetezi zaidi ya wanaharakati
 
Kweli kila siku kuna wasanii. Hata hao wanaijiita wawekezaji wakiamua kuwapa hao wananchi umeme anaodai wa ziada Tanesco wako tayari kuuchukua? TPC pale Moshi wana umeme wa ziada kila wakifanya mawasiliano na Tanesco waongeze umeme wanagoma. Mji wa moshi wote unaweza kupewa umeme na TPC bila shida. Hawataki hawa ama hawana taarifa hizo? Waache unafiki wao. Aseme naye anaenda kuchukua kilo zake kadhaa za dhahabu atkomee zake!

wanataka umeme wa bure TANESCO wana uwezo wa kuondoa ili tatizo sema kila anayetaka kusaidia kwenye kutoa umeme ananyimwa kwa sababu mafisadi dili itakata
 
Na wewe usiturudishe nyuma na watu wako wachafu wa maadili. Wewe unataka wakurupukaji? Mimi nadhani hatua ya Pinda ni nzuri na hata siku moja serikali haiendeshwi kwa kukurupuka na kufoka foka kama unvyotaka wewe!


Huyu ni waziri mkuu si haki yeye kulalamika,serikali yetu kila mtu akiongea ni kulalamika kama wameshindwa si bora wajiuzuru kuliko kulalamika ovyo ovyo
 
Pinda anajishaua tu hana lolote. Hao barrick walimuingiza kingi kagasheki, akaahidi kumueleza pinda juu ya uhuni huo lakini hadi leo hakuna kilichofanyika pamoja na wananchi wa nyamongo kuathirtika sana wengine wakafariki pamoja na mifugo yao kutokana na sumu iliyoingia mto tigithe toka mgodini.

Sanasana anatafuta tu kujipendekeza kwa barrick waangalie watamgawia nini,kama wabunge wanapata laki tano kwa trip basi wazirti mkuu bahasha yake itakuwa nzito kidogo.
 
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda ameoneshwa kukerwa na jeuri inayooneshwa na uongozi wa Mgodi wa Dhahabu wa North Mara (Nyamongo) unaomilikiwa na Kampuni ya African Barrick Gold uliopoTarime katika kuwasaidia wananchi wanaozunguka mgodi huo.
Hapa kwenye nyekundu kwa mtu usiyemfahamu pindi unaweza kupata matumaini kuwa sasa viongozi wameamua kuwajali wananchi, lakini kwa mimi tokea ishu ya Jairo alipokuwa anatuambia angekuwa yeye ange.............. halafu kilichofuta ITV ni ...............................na leo mi ndo naona hayahaya
 
Huyu Pinda naye anatuangusha na falsafa yake rahisii ya mtoto wa mkulima. Mkulima gani anaona wenzake wananyanyaswa na mabwenyenye yeye yupo tu anaomba anaomba nini badala ya kutoa agizo. Kwani serilkali yetu isigeuze 80% share ownership ya migodi haya na wakati hii imewezekana kule Venezuela kwa makampuni yenye kiburi yaondoke. Eti hatutakubali makampuni mengine yaje na madharau, kwahiyo Barrick waendelee kutudharau eeh.

Kweli Tz tu magogo viongozi
 
Mnasema ohh wakurya jeuri sasa hawa majizi wa Barrick wanakwiba mchana kweupe watu wa Tarime wakikaataa nchi nzima inasema watu wa mara wakorofi!!
 
Habari za pinda huwa zinatia kichefuchefu siku hizi. Mtu mzima yuko pale lakini hana maamuzi yoyote na sijui kwanini asijiudhuru kwa hili la Jairo! Ameenda kuonyesha utindiga wake tena huko kwa wazungu. Kama alishindwa kwa Jairo Je wazungu atawaweza wapi huyu mbwa mzee asiyekuwa na meno?
 
Alisema Serikali haitavumilia tena kupokea wawekezaji ambao baada ya kuwasili nchini na kuwekeza wanaanza kutoa kauli za kijeuri dhidi ya Serikali kwa kisingizio kwamba wao ni wawekezaji wanaotafuta faida.

“Hatuwezi kukubali eti kwa vile wanawajibika kwa Wizara ya Nishati na Madini, basi watu wengine wasiwaguse au kuhoji juu ya suala lolote, ni lazima faida wanayoipata isaidie kupunguza matatizo ya kimsingi kwa wananchi wa jirani,” alisema.

Haya maneno ya Pinda yana kera na yanaleta kichefuchefu sababu kila dakika uwekezaji usio na tija unawekwa saini sasa sijui Pinda anataka kutuambia nn na hao magamba wenzie!!
 
HIvi ni uamuzi upi Pinda amewahi kufanya. Tatizo ni unafiki tu hapa!! Pinda JK na viongozi wote wa magamba wako mifukoni mwa wawekezaji. wengine hata C**p** watahongwa!

Mtoto wa mtaani utamjua. Matusi ya nini?
 
Back
Top Bottom