sir.JAPHET
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 699
- 133
Thursday, 09 August 2012 21:08
Reginald Miruko, Dodoma
SERIKALI inachunguza sakata la Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma la kugoma kutekeleza tamko lake la kuitaka kuacha kukusanya ushuru kwa wachuuzi wadogo.Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alilieleza Bunge jana wakati akijibu maswali ya papo kwa hapo, kuwa kodi hizo ni kero na bughudha kwa wananchi wanaotegemea biashara ndogo ndogo na mboga mboga kujipatia mahitaji yao.
Alisema badala ya kodi hiyo , Serikali ilianzisha ruzuku maalumu ili kufidia pengo lililotokana na kufuta kwa kodi kero kwa wananchi.Maelezo ya Waziri Mkuu yalitokana na swali lililoulizwa na Peter Serukamba (Kigoma Mjini-CCM) juu ya meya wa Manispaa wa Kigoma kufunga masoko akilazimisha kodi hizo kutozwa, licha ya kuwapo tamko la Naibu Waziri wa Tamisemi, Agrey Mwanri, na kuzuia kodi hizo.
Pinda alisema, tamko la Mwanri ni sahihi kwa kuwa wananchi wanaofanya bishara za uchuuzi wanabughudhiwa, hivyo akaahidi kutoa agizo hilo kwa maandishi ili kuona nani anayekataa kutekeleza.
Kama Kigoma wameona General Purpose Grant (GPG) haiwafai, sisi tutawithdraw (tutaiondoa) ili tuone kama huo ushuru utaweza kuwasaidia, alisema Pinda.
Katika swali lake la msingi, Serukamba alisema Serikali ilianzisha GPG ili wachuuzi wadogo wasitozwe ushuru na maelekezo yametolewa na Mwanri akiwa Kigoma, lakini halmashauri zimekataa zinaendelea kuutoza.
Reginald Miruko, Dodoma
SERIKALI inachunguza sakata la Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma la kugoma kutekeleza tamko lake la kuitaka kuacha kukusanya ushuru kwa wachuuzi wadogo.Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alilieleza Bunge jana wakati akijibu maswali ya papo kwa hapo, kuwa kodi hizo ni kero na bughudha kwa wananchi wanaotegemea biashara ndogo ndogo na mboga mboga kujipatia mahitaji yao.
Alisema badala ya kodi hiyo , Serikali ilianzisha ruzuku maalumu ili kufidia pengo lililotokana na kufuta kwa kodi kero kwa wananchi.Maelezo ya Waziri Mkuu yalitokana na swali lililoulizwa na Peter Serukamba (Kigoma Mjini-CCM) juu ya meya wa Manispaa wa Kigoma kufunga masoko akilazimisha kodi hizo kutozwa, licha ya kuwapo tamko la Naibu Waziri wa Tamisemi, Agrey Mwanri, na kuzuia kodi hizo.
Pinda alisema, tamko la Mwanri ni sahihi kwa kuwa wananchi wanaofanya bishara za uchuuzi wanabughudhiwa, hivyo akaahidi kutoa agizo hilo kwa maandishi ili kuona nani anayekataa kutekeleza.
Kama Kigoma wameona General Purpose Grant (GPG) haiwafai, sisi tutawithdraw (tutaiondoa) ili tuone kama huo ushuru utaweza kuwasaidia, alisema Pinda.
Katika swali lake la msingi, Serukamba alisema Serikali ilianzisha GPG ili wachuuzi wadogo wasitozwe ushuru na maelekezo yametolewa na Mwanri akiwa Kigoma, lakini halmashauri zimekataa zinaendelea kuutoza.