JIULIZE KWANZA
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 2,569
- 499
hebu tupite mkoa wa rukwa tuone virojaMh.Pinda huku ni kutudhihaki Watanzania.Eti unashangaa watu kujenga nyumba za nyasi Ngara! Umetembea nchi nzima na kuona? Hujaona nyumba za tembe zilivyo zagaa Shinyanga,Tabora,Singida na Dodoma? Maisha yetu magumu sana wakati ninyi mnajinufaisha! Pesa tu ya mlo wa kilasiku kwetu ni mbinde,simenti na bati tutaviweza? Tujengeeni nyumba kisha mtupe bure,kwani pesa kiasi gani zinapotea? Nasi twataka kuifaidi nchi yetu wala sio wachache.Wengine mnaishi peponi bwana wakati sisi tupo kwenye mateso.Usishangae kwani Mh.wewe hujui?
Na kulia lia eti wachungaji wakemee mafisadi maana ni waumini wao kweli waziri mkuu unaweza kumtegemea mchungaji/sheikh awakemei mafisadi wakati serikali inawajua na haitaki kuwachukulia hatua...juzi aliomba majina ya wasambazaji wa sukari huko Bukoba sijui anataka kuwafanya nini au ni unafiki tu kama ni kuwachukulia hatua siaanze na mapapa walio tuibia mabilioni....Mkwere nae analialia tu uoh chadema wataleta machafuko ujinga mtupu....Mnamshangaa Pinda kushangaa kwanini watu wanaishi nyumba za nyasi? mbona bosi wake aliulizwa kwa nini Tanzania ni masikini kupindukia naye akashangaa na kusema hajui kwa nini TZ ni masikini. Hao ndio Nahodha na Msaidizi wake katika meli yetu iliyo safarini ikipigwa na mawimbi. Lakini wao hawajui wapi north wapi east, bora liende tuu.