Pikipiki kuwakaanga viongozi CCM Arusha

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,722
21,775
Pikipiki kuwakaanga viongozi CCM Arusha

Mussa Juma, Arusha


KAMATI ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) mkoani Arusha, imependekeza zichukuliwe hatua za kinidhamu dhidi ya viongozi waandamizi wa chama hicho wilaya ya Arusha kwa kumwalika Mwenyekiti Taifa, Rais Jakaya Kikwete, katika hafla ya kugawa pikipiki zilizo kuwa na utata.


Mapendekezo ya kamati hiyo, ambayo yalijadiliwa juzi usiku na Kamati ya Maadili ya CCM mkoa yalipelekwa jana kwa njia ya Fax kwenye sekretarieti ya chama Taifa.


Wajumbe kamati ya maadili waliokutana katika ofisi za CCM mkoa kujadili mapendekezo ya kamati ya siasa ya mkoa ni Katibu wa CCM mkoa , Mohamed Mbonde, mwenyekiti wake, Onesmo Nangole, mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) wa mkoa wa Arusha, Elishilia Kaaya, Katibu Uenezi na Itikadi mkoa, Loota Sanare na Mkuu wa Mkoa, Isdori Shirima pamoja na Samweli Urassa.


Habari za uhakika toka ndani ya kikao cha awali cha kamati ya siasa ya mkoa zimeeleza kwamba, licha ya viongozi wote wa kamati ya siasa ya chama wilayani Arusha, kuomba radhi kwa maandishi kwa kitendo hicho, kamati ya mkoa imependekeza kuwa wachukuliwe hatua.


Vikao vya kamati hiyo ya siasa na maadili vya CCM mkoa wa Arusha, vilikutana mfululizo kutokana na agizo la Rais Kikwete kwa viongozi wa chama wa mkoa kwamba, apewe taarifa juu ya tukio zima la kutakiwa kugawa pikipiki hizo ambazo

miongoni mwake zipo zilizotolewa na mfanyabiashara mmoja anayekabiliwa na kesi ya ufisadi wa mabilioni ya fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania.


Habari toka ndani ya uongozi wa CCM mkoa, zimeeleza kuwa baada ya viongozi hao kuhojiwa, akiwemo Mbunge wa jimbo la Arusha, Felix Mrema, Mwenyekiti wa wilaya, Jubilate Kileo na wake Mohamed Nyawenga na viongozi wengine, ilibainika kulikuwa na kasoro katika mipango ya ugawaji wa pikipiki hizo.


Mjumbe mmoja wa kikao kilichowahoji viongozi hao, aliyeomba kutotajwa jina alifahamisha kuwa kitendo cha kumualika Rais Kikwete katika tukio hilo kilitafsiriwa kama kutaka kuhujumu jitihada zake za kupiga vita ufisadi.


“Tuliwauliza kwamba, hata kama mfanyabiashara huyo alichangia pikipiki hizo mwaka 2007, ilikuwaje aalikwe ili apongezwe na rais wakati inajulikana kuwa ana kesi ya EPA mahakamani?” alisema mjumbe huyo.


Katika kikao hicho, viongozi hao walibanwa sababu za kuzigawa pikipiki hizo wakati Rais Kikwete alisita na kuagiza

apewe taarifa, lakini walijitetea kuwa aliruhusu baada ya

kusema ameziona na wagawane wenyewe.


Hata hivyo, kiongozi mmoja wa wilaya alisema awali ilipendekezwa kuwa mfanyabiashara huyo asiudhurie na badala yake atume mjumbe, lakini bila wao kutarajia siku ya tuko alifika yeye mwenyewe.


“Hata sisi tulishangaa kumuona pale kwani tunajua anakesi. Lakini pia ikumbukwe kuwa alichangia pikipiki hizo mwaka 2007 na kama ulikuwepo siku ya tukio, nadhani hata wewe uliona hali ilivyokuwa,” alisema kiongozi huyo.


Hata hivyo, wakati kamati ya Siasa ya CCM mkoa ikiwa imependekeza kuswachukuliwa hatua baadhi ya viongozi wa wilaya, tayari kumeibuka mgawanyiko mkubwa ndani ya chama mkoani.


Kundi moja la wana CCM wilayani Arusha linapinga kuchukuliwa hatua kwa viongozi wao kwa madai kuwa, pikipiki hizo zilitolewa kwa nia njema ya kukisaidia chama mwaka 2007 na kwamba, mtuhumiwa huyo wa EPA licha ya kuchangia pikipiki hizo kwa miaka mingi amekuwa akikisaida chama katika ngazi mbali mbali.
 
Watanzania ukitaka kuwaua au watoane macho leta misaada hapo ndiyo utajua fikra za kila mtu.

pole zao.
 
Huyo mhisani mwenye kesi ya EPA mbona hatajwi kwenye hii taarifa? Ndio kazi fyongo hizi za vyombo vyetu vya habari.

Halafu kama hujui unyuma wa hili tukio huwezi kufahamu kwa kusoma hii taarifa iwapo Kikwete alikuja kwenye hafla au hakuja. Na kama alikuja, alijuaje na alijua katika kipindi gani kwamba pikipiki hazifai yeye kuzigawa? Au ni kwamba hakuja ila alishtukia akiwa Ikulu kwamba amepewa mwaliko famba?

Lakini inaoneka kama Rais alikuwepo Arusha. Kwa hiyo aliingia mkenge, kwa maana kwamba, aliamua kusafiri wakati barua ya mwaliko kwa Rais haikusema pikipiki zimetoka kwa nani. Yani Rais na watu wake walijiendeaendea tu kama wanahudhuria sherehe ya pilau.

Nani alimtonya akiwa Arusha kwamba pikipiki hizi baba ni za marehemu Ballali au Jeetu Patel au za Benno Ndullu wa BOT and so forth?

Au Kikwete alikuwa anaanza kugawa pikipiki halafu akaona Patel yule pale kwenye halaiki, akaona mmh, hapa nuksi, akachomoa? Yani ki taarifa hakikupi mwanga wowote juu ya tukio hili. Nini kilitokea?

Anaejua zaidi ya huyu mwandishi labda atueleze, ili waandishi wachukua habari hapa halafu ndio warudi kuandika. Wanatia huruma yani wanahabari wetu.

Lugha yenyewe nayo tabu tupu. Mwandishi wa gazeti la kiswahili unaandika maneno fyongo kama "asiudhurie," "kuswachukuliwa," pia hujui kwamba "zilizokuwa" sio maneno mawili "zilizo kuwa," na mhariri nae anapitisha! Wanaandika "Fax" kiingereza wakati kuna neno la kiswahili, tena wanaliweka kwa herufi kubwa "F" katikati ya sentensi. Kama wanafunzi watoro wa darasa la sita vile!
 
ebu soma hii katika gazeti la Nipashe siku hiyo hiyo

JK akwepa kumtunuku cheti mtuhumiwa EPA

JK akwepa kumtunuku cheti mtuhumiwa EPA

2009-01-11 15:59:33
Na Novatus Makunga, Arusha


Rais Jakaya Kikwete jana alikwepa kumtunuku mmoja wa watuhumiwa wa kesi za wizi wa fedha katika akaunti ya madeni ya nje(EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania(BoT), wakati akitakiwa kugawa pikipiki kwa makatibu wa Chama cha Mapinduzi wilayani hapa.

Rais alikwepa kugawa pikipiki hizo zenye thamani ya sh.milioni 24.5 baada ya kubaini uchangiaji huo ulijumuisha mfadhili ambaye ni mfanyabiashara maarufu wa mafuta, Japhet Lema maarufu kama Njake, anayetuhumiwa katika wizi wa fedha EPA.

Mfanyabiashara huyo alihudhuria hafla hiyo ili naye atunukiwe cheti cha shukrani.

Pikipiki hizo ambazo zimekaa kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu sasa katika ofisi ya CCM wilayani Arusha zikitafuta \'mzito\' wa kuja kuzigawa, zilikuwa zikabidhiwe sanjari na vyeti vya shukrani kwa waliozitoa,katika shughuli iliyoandaliwa na chama hicho wilaya.

Kwa mujibu wa habari za ndani ya chama hicho, waliochangia pikipiki hizo kumi na tisa ni pamoja na mbunge wa Arusha Felix Mrema na mwenyekiti wa CCM wilayani Arusha Jubilate Kileo.

Rais Kikwete pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, aliwasili katika uwanja wa CCM wilayani hapa majira ya saa kumi jioni na baada ya kukaribishwa kuzungumza, ikitegemewa baadaye ndipo ataanza kazi ya kugawa pikipiki hizo, akasema kamwe hataweza kufanya hivyo bali atawaachia viongozi wa wilaya wajigawie wenyewe.

``Nimeziona lakini sitaweza kugawa moja baada ya nyingine, mimi sijui mlikozipata, lakini wenyewe mnajua mtakaa mtagawana wenyewe,``alisema.

Hata hivyo, Rais Kikwete aliwaonya kutotafuta raslimali ambazo zitawaletea matatizo hapo baadaye na kuwataka wazidishe mshikamano na umoja kama nguzu muhimu ya mafanikio.

Aliwataka wakamilishe maandalizi ya chaguzi za serikali za mitaa ili waweze kupata ushindi mzuri na pia aliwatakia kila la heri katika uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata ya kati unaotarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu. kwani ni vizuri kuwa na vitendea kazi wakati tunaelekea katika uchaguzi,``alieleza Rais Kikwete katika hutuba yake ambayo haikuzidi dakika tano.

Hata hivyo, pamoja na Rais Kikwete kuachia jukumu hilo kwa uongozi wa wilaya, mpaka viongozi wa ngazi mbalimbali wanaondoka, pikipiki hizo zilikuwa hazijagawanywa katika kile kilichoonekana kila mmoja kukwepa kufanya shughuli hiyo na kumrushia mpira mwenzake.

Mara baada ya Rais Kikwete kuondoka, Mwenyekiti wa CCM wilaya Bw.Kileo alikuwa wa kwanza kuongea na kueleza kwamba shughuli ya ugawaji itafanywa na katibu wa wilaya, lakini baadaye katibu wa wilaya naye alieleza shughuli hiyo itafanywa na katibu wa uenezi na siasa.

Jitihada za kumpata Katibu wa CCM wa wilaya ya Arusha, Bw.Mohammed Nyawenga ambaye aliondoka na Rais Kikwete kwenda uwanja wa ndege hazikufanikiwa kwani simu yake ilikuwa inaita bila ya kupokelewa.

Katibu wa uenezi na siasa wa wilaya hiyo, Bw.Semmy Kiondo alieleza kuwa anachofahamu watu ambao wangekabidhiwa vyeti vya shukrani ni Mrema na Kileo na alipoulizwa kwanini Lema alihudhuria shughuli hiyo alijibu kuwa alikuja kama wanachama wengine.


SOURCE: Nipashe
 
Hivi hawa viongozi wa CCM Arusha wana tamaa gani kupokea hisani kwa mtuhumiwa wa EPA. Huu ni udhihirisho wa jinsi CCM inavyoukumbatia ufisadi.
Bora waingie kikaangoni!
 
Huyo Njake amekuwa akichangia SSM mamilioni ya uchaguzi na shughuli za chama. Kama kuna mtu yuko Arusha ukienda ofisini kwake utakuta hati za shukrani lukuki kutoka SSM kila kona ya ukuta nyingine hadi rangi haionekani. Hata wakati Kikwete anafanya kampeni Arusha, Njake aligharimia maandalizi, hata vikao vya kuchangisha alikuwa anakaa kiti cha mbele. Leo hii ili kujisafisha SSM top leader huyo huyo anaona aibu kugawa pikipiki kwa kuwa anaogopa wananchi. Ni kweli ni lazima aogope maana 2010 iko karibu. Hizo naweza kusema ni double standards. Mbona kuna viongozi na wafanyabiashara ambao wana skendo kubwa kuliko hata ya Njake but Kikwete na top wote wa SSM wanawakumbatia na hawataki waguswe (untaouchables)????

Ila tu nataka kama kuna mtu yumo ndani ya forum ambaye anamfahamu Njake na anaweza kumpa ujumbe ni kwamba ""Ajihadhari sana na kuchangia changia, katika wale ambao wamekua earmarked kwa ajili ya kutumikia kifungo kwa sakata la EPA, Njake ni mmojawapo""". Hiii imetokana na kwamba, japo Njake anachangia sana SSM but si Swahiba wa Kikwete kabisa so kama akimsulubisha hana anachokosa kwake baada ya urais wake kumalizika. Kikwete anaogopa kusulubisha marafiki ili asije akawakosa baada ya urais wake kumalizika. Inafahamika kuwa kuna watu kutoka ndani ya system wanaenda kwa Njake kumdangaya na anawapa hela kuwa eti kesi ya EPA ni siasa tu na hakuna kufungwa. Naamini tangu Sakata la EPA limeanza ameshaliwa fedha nyingi sana (mamilioni), wengine walimdangaya wataficha documents, mara tutahakikisha hutapelekwa mahakamani kumbe wanamdanganya na Kisutu amekanyaga.

Jambo lingine ni kwamba, Njake ni mjanjamjanja sana katika masuala ya kutafuta bingo. Anatakiwa afahamu kuwa ameshapata utajiri wa kutosha, haijalishi aliupataje kutoka kuwa muuza nyama mabuchani na ambaye hajakanyaga hata darasa la kwanza (japo alifundishwa namna ya kuandika jina lake na kuweka saini) bali aachane na njia hizo sasa asimamie mali aliyo nayo kwani na umri nao umeshampata.

Lingine akumbuke kuwa katika sakata la EPA alimwingiza Jonathan Munisi akimdanganya kuwa amwandikie na kumjazia documents za kupeleka BOT huku Njake akiendeleza mipango yake na Balali Holiday Inn na kuwa pesa hizo ni mikopo na ni halali. Munisi aliposhtuka kwa nini katika write up hakuna maelezo ya namna ya kurejesha mkopo na alipomuuliza alimhakikishia kuwa hauna tabu. Mbaya zaidi akapitisha fedha ndani ya account yake ili abadilishe ziwe dola ampe marehemu Babali, na Munisi alipohoji ni za nini alimwambia kuna biashara anafanya na Balali. Mambo yalipotoka kuwa fedha zilikuwa na wizi na Munisi alipomtafuta na kumuuliza kwa nini alimwambia amwandikie biashara ya wizi bado Njake aliendelea kumdanganya kuwa hakuna tabu atamlinda na atamlipa fidia kama lolote litatokea. Sasa leo hii Munisi yuko Keko, Njake hajishughulishi kumtoa akijua Munisi hana uwezo wa dhamana kubwa vile. Kazi kubwa aliyofanya ni kwenda kuhudhuria kikao cha kugawa pikipiki ili kujisafisha na akatolewa nje!!!! Ukiona kuna watu wanaibuka na utajiri wa mashaka ujue kuna jambo lisilo la kawaida ndani yake. Huke eti Njake anajiita Mlokole na anachangia sana makanisa. Kumbe jizi. SSM imekuwa ikifadhiliwa na wezi na isijifanya leo hii kuwakataa wezi wake kama Njake au Japhet Lyandui Lema, kina Jeet ambao wanafanya sherehe na kuwaalika kula vya wajinga, wote hao wanaotuhumiwa na EPA wanavinjari na viongozi kwa namna moja au nyingine, wengine hadi wana urafiki na watoto wao kama akina Jonson Lukaza (Riz ni rafiki, mwenye simu na ya Riz na ile ya Lukaza, ukipata print out tu utaona communications zao!!!). Huo ni mfano tu, achilia mbali watoto wa EDDO Mmaasai na Lukaza.
 
Ni fisadi lema naona watu wanazunguka.....
 
mzee Lema ni mchangiaji mzuri hata lile Scania la mwinjilisti mahiri Mwakasege ni yeye alimpa,pia safari za kwenda Israel za mtumishi Mwakasege na kikundi chake zimekuwa zikifadhiliwa na Njake.Kipindi cha kampeni mwaka 2005 magari ya CCM na wakereketwa yalikuwa yakipewa mafuta na Njake.Mzee Lema {Njake} alikuwa mwenyekiti wa kuandaa mapokezi ya Eduard Lowasa mara baada ya lile skendo la Richard Monduli {RICHMOND}.
 
Back
Top Bottom