Picha za MNYIKA akitolewa nje ya Viwanja vya Bunge

Wabunge wa cdm na wengine wasiopenda kujipendekeza msirudi nyuma na sisi wengine tuwatie moyo kwani wanafanya hivyo kwa niaba yetu.
 


masopakyindi una nidhamu ya uoga, na watu kama wewe ndio mnaochelewesha mabadiliko, ni afadhali kuwa na mnyika mmoja kuliko kuwa na watu kama wewe elfu moja, hovyo kabisa!
Ule ulikuwa ushauri wa bure kabisa kwa kijana mwanasiasa Mnyika.
Anaweza kuukubali au kuukataa na kuutupa kapuni.
Hiyo ni hiari yake.

Akitumia busara na umahiri wake katika kujenga hoja anaweza kufika mbali pamoja na kuwasaidia watanzania.
Kwa tunao mfahamu jazba si hulka yake sijui nini kimempata masikini huyu.

Hata hivyo mlio karibu naye mumshauri tu kama anapenda confrontation mbona uwanja mkubwa sana?
Na ndio nikasema awasiliane na Lema kwa kucompare notes na aone kisiasa anaweza himili mikiki kwa muda gani zaidi.
Angalizo tu ni kuwa JK kama taasisi, is very large and looming, anybody can go for him-officially!
 
Hivi kusema ukweli ni matusi?

Kwani kikwete yeye ni Mungu mtu asiambiwe ukweli?hivi huyu ndugai ndo kupalilia kibarua au?mbona magamba wanaongea mipasho kejeli lakini hizo ibara na vifungu vya sheria havisomwi?

Ukweli utabaki kuwa ukweli tena mi naona kama ametumia kauli nzuri sana maana huyo mzee ni mshenzi sana kaanza kwa kujichekesha2 sasa kicheko kimekwisha amebaki sura imemshuka kama paka jizi,watz tunataabika wamebaki kuchukua milungula kwa wawekezaji
 
kikweeeeeeeeeeeeteeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee ccm juuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuup, juuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuup , juuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuup
ufisadi juuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu,ufreemason wa ccm juuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu,wauwaji wa ccm juuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu,2015 ccm byeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee,majambazi wakubwa na rais wenu
 
msikubali kunenepeana wabunge wa CDM...unene unaleta kufikiri kudogo sana...waandgalieni wenzenu wanavyopata shida kusoma na kutafakari...mengine yamelala tu...ungalia wewe baba mwepesi hata kufikiri baba...CDM juuuuuu

sasa ww naona umegeuza ukumbi wa bunge kuwa sehemu ya kuonyesha ubunifu wa mavazi.Umesikia Modos wanatafutwa pale? acha hizo.
 
Dare to be different, dare to take a stand for what you know is right...:flame::flame:
 
Naomba kutofautiana nawe katika hoja hii kama ifuatavyo:
Wabunge wanaeleweka kama ni professional katika uwanja wao. Tofauti na wengi ambao tunapongeza hatua ambayo Mnyika amefanya kwani haijaonyesha kitaaluma na kitaalamu hoja pamoja na kuwa na uzito kutoiwasilisha kama professional member.

Mnyika ni msomi na anajua fika namna ya kujenga hoja na kuchagua lugha ya kufkisha ujumbe, lakini kwa namna na hisia aliyokuwa nayo amepitiliza kiwango ambacho angetazamiwa kufanya. Ukisema unaenda kujisaida (restroom) na mwenzako akasema anaenda kunya au kukojoa (samahani kwa lugha hiyo) nadhani maana ni moja lakini inatoa taswira tofauti kwa atakayawasikia. Wote mnaenda kufanya kitu kilekile lakini matumizi ya lugha yamenya mtofautiane kimtazamo na kistaarabu kutokana na uwezo wa kufikiri haraka na kuchagua lugha ya kutumia.

Pamoja na kwamba walio upande wa Mnyika wamejiridhisha kwamba Mnyika kasema ukweli, lakini kwa wenye busara na hekima watakuambia Mnyika ameteleza katika kufikisha hoja yake kwa kukosa ubunifu wa kuchagua lugha sahihi ya kutumia katika bunge tukufu na kwa namna ye yote amekiuka taratibu za matumizi ya lugha inayotakiwa kutumika bungeni.

Mimi si mtu wa kufuata upepo sababu ya kile moyo ukipenda, ula ukweli uendane na ustaarabu, elimu na busara katika maisha, mahusiano na shughuli za kila siku. Kama ni shauri ya kuropoka tu kila mtu afanye hivyo nadhani tusingekuwa hapa tulipo.

Tunapaswa kuwajenga hawa watu na kujitahidi kuwakosoa wanapoteleza, isiwe kila wafanyavyo hata kikikosa hekima na busara ni kusahbikia tu kama timu ya nyumani hata kama mtu kafunga goli mpira wa miguu kwa mkono, hii imekaaje?

Mkuu unachosema ni sawa ila lazima uangalie mazingira yaliyopelekea kutolewa kwa kauli hiyo! Bunge letu tukufu limepoteza weledi na ndo maana unasikia mipasho+kejeli za kila aina na si ujengaji wa hoja! Katika mazingira hayo huna namna ila "to call a spade, a spade"! Ukitilia maanani ni kodi yangu mie niliyepigika kimaisha hivi ndo inawalipa posho, sina namna ila kukubaliana tu na Mnyika!
 
what d you mean yaani mnyika ni takataka ?

Kwani mnyika ameshikwa mkononi????

Hao unaowaona ni OFFICE CLEANERS wa Bungeni. Muda ule naibu Spika aliposema wamtoe nje, walitoka kubeba Dust bin hivyo walijisahau kuvua Gloves.
 
Wadanganyika wamejengwa - Nidhamu ya Woga. Hakika CCM itatawala milele kwa sababu wanajua mikwara imesha jengewa jeneza. Ikiwa Wabunge hawawezi kusema kuwa Rais wao ni dhaifu, je nani atakayeweza kumkemea rais?.Je huu sii utumwa wa akili kumtukuza mtu hata kama mwenyewe hapendi kutukuzwa hivyo!. Nina hakika JK mwenyewe anacheka sana hapo alipo maana kayatumia maneno haya sana tu.. au ndio mkubwa akijamba lawama huzichukua watoto..Jamani matumizi ya lugha ya Kiswahili yanaanza kupotea hata kwa Watanzania wenyewe hii ni dalili kubwa ya kwamba tunaipoteza lugha yetu.

Leo hii tunagombana juu ya neno DHAIFU ambalo sijawahi kuliona mahala popote likitumika kama tusi.. Mimi mwenyewe leo najisikia dhaifu sana hata kazini sikwenda kutokana na homa kali - Hivi nimejitukana kumbe?. Jamani jamani acheni hii nidhamu ya woga kushabikia kitu ambacho kesho wewe mwenyewe utapenda kusema udhaifu wa mtu au hata rais mwingine asiyekuwa JK. Hakuna lugha nzuri ya kusema mapungufu ya rais ktk kushindwa utendaji kazi wake isipokuwa neno - DHAIFU - WEAK na hili neno limetumika ktk mihadhara, mbio za uchaguzi, bungeni na hata mahakamani ktk kujenga hoja kuonyesha uwezo mdogo wa upande wa pili kuliko kusema hana uwezo ama hafai kuwa rais wakati amechaguliwa na wenggi kutokana na sifa hizo.

Mtanisamehe sana Wadanganyika siasa za vyama vingi hamuiwezi.. vitimbi vya kisiasa hamuviwezi, hivyo bora mrudi ktk chama kimoja na ijulikane kabisa tuna baba wa Taifa ambaye hana udhaifu wala mapungufu.
 
Nimesoma ktk mtandao kwani vipi?

Mkuu wangu, waheshimiwa hawajikiti katika kujenga hoja, mipasho, majibizano na ushindani ndio vilivyotawala katika bunge. Unless kama ulisikiliza mwenyewe ila ni kazi sana kucomment, kwa kuwa vyombo vya habari vinaandika kwa upande vinavyoona sawa, na ni the same applies kwenye hii mitandao.

Mkuu wangu, si upinzani, si chama tawala isipokuwa wachache sana, hawajadili bajeti ila wamegeuza bunge kama ni sehemu ya kampeni ama ya kuombea kura. Mkuu wangu [MENTION]mkandara [/MENTION]hakuna nidhamu kabisa bungeni, nimeweka post moja juu ya msigwa, anawasha kipaza sauti wakati wabunge wengine wanaongea, ilibidi naibu spika amshitaki kwa wapiga kuwa wake. Ukiangalia alichofanya mnyika ni mashindano ya kitoto naweza kusema, it was so simple baadaya kufahamishwa na kanuni kuwa si sahihi kwa mbunge kumuattack rais tena kwa jina lake, kama angekuwa matured na kwa faida ya wapiga kura wake, angeodoa ile kauli ili aweze kufikisha message ya wapiga kura wake, sio kusema SIFUTI ule ni ubabe wa mitaani.

Kwa hiyo mkuu wangu, habari za bunge zichuje vyema kabla hujachangia zina mgogoro sana.
 
Mkuu unachosema ni sawa ila lazima uangalie mazingira yaliyopelekea kutolewa kwa kauli hiyo! Bunge letu tukufu limepoteza weledi na ndo maana unasikia mipasho+kejeli za kila aina na si ujengaji wa hoja! Katika mazingira hayo huna namna ila "to call a spade, a spade"! Ukitilia maanani ni kodi yangu mie niliyepigika kimaisha hivi ndo inawalipa posho, sina namna ila kukubaliana tu na Mnyika!

kwa mafanikio yyt ktk maisha ni matokeo ya matumizi mazuri ya ulimi.
 
Jk siku zote hana maamuzi ni mtu asiyejua majukumu yake na kwa nini yeye ni Raisi .Hivyo Mnyika hakukosea kumwita legelege
 
Mkuu unachosema ni sawa ila lazima uangalie mazingira yaliyopelekea kutolewa kwa kauli hiyo! Bunge letu tukufu limepoteza weledi na ndo maana unasikia mipasho+kejeli za kila aina na si ujengaji wa hoja! Katika mazingira hayo huna namna ila "to call a spade, a spade"! Ukitilia maanani ni kodi yangu mie niliyepigika kimaisha hivi ndo inawalipa posho, sina namna ila kukubaliana tu na Mnyika!

Give me a break dear brather and comrade there is no way one can tolorate what is going on now in our country while the Honorable presedent and the security organs like usalama wa taifa are totaly sleeping without any action. Kwa niaba ya mnyika namwomba radhi sana rais wetu kwa kweli kama ameudhika kitu ambacho sidhani kama kwa upande wake kipo ila kwa wapambe wake tena wale NUKSI tuu na ndiyo maana nimesikia yupo dodoma tusubirie huenda ameshatafakari na hatua thabiti na sahihi zitafuata kwa wale wote waliomwangusha kiasi hicho mpaka kusemwa vibaya BUNGENI.
 
Nalazimika kuamua kuandika haya kutokana na niliyoyashuhudia katika bunge letu la bajeti linaloendelea hivi sasa mjini Dodoma.

Ndugu zangu ukweli tulonge bila kumungunya maneno watakaokasirika na wakasirikre lakini kwa nafasi tofauti tuseme haya hatupaswi kunyamaza.

Mimi nimeamua kulitoa hili na sijui kama wenyewe wanalitambua ama wamezibwa masikio na mawazo wameyafunga

Nimefatilia kwa ukaribu sana mjadala wa bajeti iliyowasilishwa bungeni na serikali kupitia kwa waziri wa fedha, na nimekuwa mfuatiliaji mzuri wa hoja zilizokuwa zinachangiwa kuhusu bajeti ya serikali, hiyo siyo issue kwangu, issue ni jinsi wabunge wa CCM wanavyotumia nguvu nyingi kukilinda chama chao kuliko maslahi ya wananchi waliowaweka madarakani.

Wote waliochangia idadi kubwa walikuwa wanatetea CCM tena kwa maneno mengi ya kuvutia huku wakiwaponda wapinzani na bajeti yao.

Nilishangazwa na kujiuliza pale mbunge wa mtera, Livingstone Lusinde, na mwenzake kapten John Komba , kwa kweli bila kuficha waheshimiwa hawa live wako bungeni kwa lengo la kukisaidia chama cha mapinduzi si wananchi.


Tunajua ni lazima wakilinde chama chao , lakini basi angalau waonyeshe kujali na maslahi ya wananchi waliowafanya wawe mjengoni, palipo na ukweli waseme siyo mwanzo mwisho kutetea ccm na kuwaponda wapinzani.


Wakati bado ningali nayakumbuka maneno ya mbunge wa mtera kwa wananchi wa Arumeru mashariki , maneno machafu yasiyofaa hata kusikilizwa na watoto wadogo wala watu wenye heshima zao ,Huku nikijiuliza kama kweli mheshimiwa huyu amechaguliwa na wananchi kuwawakilisha na leo wapiga kura wake wasikie maneno machafu aliyokuwa akiyatamka, kama hamuamini ndugu zangu tembeleeni baadhi ya mitandao ya kijamii muone matusi hayo.


Ningali nayakumbuka maneno hayo ya muheshimiwa sana, na bado yananiumiza kichwa kwa sababu niliyasikia live bila chenga , leo tena nashuhudia ndani ya Bunge Tukufu kambi rasmi ya upinzani Bungeni ikitukanwa tena matusi makubwa eti ni wendawazimu waliokosea Njia, najiuliza mwendawazimu ni nani, aliyetukana mbele ya wapiga kura wake wanaomuamini , mbele ya watoto wake waliokaa katika Runinga wakiangalia baba akifanya mambo yake Bungeni, ama Yule anayejaribu kuongea kuwatetea walalahoi walio wengi katika nchi hii, kama mimi.


Nimeshindwa kumpata mwendawazimu wa kweli kati yao, lakini sitaki kuamini maneno ya muheshimiwa Yule kuwa bungeni kuna wendawazimu, hivi inawezekana watu tuliowaamini, tukawachague wakatutetee leo wawe wendawazimu?


Eti walikosea njia walipaswa kuanzia milembe kabla ya kwenda Bungeni, halafu Yule aliyetukana matusi hayo kanuni na sheria hazikumuoni akaonekana Yule anayejaribu kusema ukweli ,mbunge wa ubungo John Mnyika.



Wabunge wetu, waheshimiwa sana labda mnajisahau jambo moja kuwa watanzania hivi sasa tunaona, tunajua, tunawasoma na ni waelewa sana tena na kwa kuwa hivi sasa tunaliona Bunge LIVE hatudanganyiki jamani, fanyeni kazi tuliyowatuma siyo kutetea mambo ambayo hayavumiliki.

Nawashauri waheshimiwa wangu kwenye ukweli semeni, kwa masilahi ya wananchi wenu waliowaweka madarakani, mwaka 2015 siyo mbali mtarudi kwetu tutawawajibisha


Vile vile kwa wale wanaokatishwa tamaa, msiogope kazeni uzi watanzania tuko nyuma yenu. Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni usiogope wewe ndie unayeongoza jaazi, usikate tamaa ili walio nyuma yako wapate ujasili, mnyika kaza uzi baba tutetee sisi tulikosa watetezi, chadema tunawaamini tuteteeni sisi tulioachwa kama yatima


JAMANI KUSOMA HATUJUI HATA PICHA HATUONI? SOMENI ALAMA ZA NYAKATI.


M4
 
Mkuu wangu, waheshimiwa hawajikiti katika kujenga hoja, mipasho, majibizano na ushindani ndio vilivyotawala katika bunge. Unless kama ulisikiliza mwenyewe ila ni kazi sana kucomment, kwa kuwa vyombo vya habari vinaandika kwa upande vinavyoona sawa, na ni the same applies kwenye hii mitandao.

Mkuu wangu, si upinzani, si chama tawala isipokuwa wachache sana, hawajadili bajeti ila wamegeuza bunge kama ni sehemu ya kampeni ama ya kuombea kura. Mkuu wangu mkandara hakuna nidhamu kabisa bungeni, nimeweka post moja juu ya msigwa, anawasha kipaza sauti wakati wabunge wengine wanaongea, ilibidi naibu spika amshitaki kwa wapiga kuwa wake. Ukiangalia alichofanya mnyika ni mashindano ya kitoto naweza kusema, it was so simple baadaya kufahamishwa na kanuni kuwa si sahihi kwa mbunge kumuattack rais tena kwa jina lake, kama angekuwa matured na kwa faida ya wapiga kura wake, angeodoa ile kauli ili aweze kufikisha message ya wapiga kura wake, sio kusema SIFUTI ule ni ubabe wa mitaani.

Kwa hiyo mkuu wangu, habari za bunge zichuje vyema kabla hujachangia zina mgogoro sana.
Ahlan Wasaalan...Shukran sana unapozungumzia maswala ya bunge na udhaifu wa wabunge ktk utoaji hoja na wala hujawatukana. Hili kwanza ulifahamu na nimekuewa vizuri ulipoyasema yote japokuwa wao wanaweza kabisa kusema umewatukana. hapakuwa na lugha yoyote ungeitumia kutafsiri vitendo vinavyofanyika Bungeni.

Sasa tuache swala la hao wengine, Ikiwa kanuni ya Bunge inakataza kumshambulia rais tena kwa jina lake wewe huoni kama huu ni ujinga mwingine. Nidhamu ina maana nyingi na ndipo nikasema tuna nidhamu ya woga kwa sababu rais hatakiwi kushambuliwa ktk utendaji kazi wake. Kwa mfano bunge limepitisha bajeti na yeye akitekeleza bajeti hiyo mnaanza kumshambulia bungeni on something kilichokwisha pita. Haya nimeyaona ktk vikao vya bunge vilivyopita na hayakukemewa. Ukosefu wa nidhamu ni pale utamwita rais Muongo wakati hakuongopa lakini ikigundulika kaongopa kweli unaruhusiwa kumshambulia maana kenda nje ya kiapo.

Hivyo ni lazima tufahamu mipaka ya mashambulizi na kanuni zinazungumzia wakati gani. Kama rais is on line ktk utendaji kazi wake ukamzushia uongo ama kumshambulia ktk swala ambalo lipo ktk majukumu yake na analifanyakama alivyupaswa kufanya hutakiwi kumshambulia. Nitarudia kusema Bush aliposema Uongo kuuyhusu WMD aliitwa muongo kwa sababu ilikuwa kweli.. Clinton aliitwa muongo alipodanganya kuhusu urafiki wake na binti yule, Nixon alipoteza urais kwa kulidanganya bunge, Jimmy Carter aliitwa rais dhaifu American ever had tena kwa sababu alitetea wanyonge na nchi maskini. Obama kisha itwa dhaifu mara kibao na majuzi tu ktk swala la Usalama tena bungeni wala sii nje lakini Demokratic walikuja na utetezi au niseme majibu kuonyesha Obama sii udhaifu kama wanavyodai.

Kinachokatazwa ni kumshambulia raisi kwa uzushi, ni kweli bunge letu watu hawana nidhamu kwa sababu wanataka sana kusikiliza sauti zao wenyewe wakirudi nyumabni kwenye luninga baada ya wake zao kufanya nakala. Kila mtu mjuaji, siye wa mujini tunasema tumebishana Kisomali, maana kiasili hawa jamaa huzungumza bila kupena nafasi. Yaani kila mtu anazungumza wakati mtu mwingine anazungumza na ajabu wanasikilizana.

Binafsi yangu nitaendelea kupinga hizi Nidhamu za woga, tunamheshimu rais wetu na tutampa kila protection inapobidi kwa maslahi ya Taifa letu lakini inapotokea kwamba bajeti haikulenga maslahi ya wananchi tuna kila sababu ya kumshambulia. Naye kwa kuelewa makosa hayo atayarekebisha maana tulomwajiri ni sisi. Mnyika kama mbunge mwakilishi wetu hana sababu ya kuomba msamaha ktk swala linalolinda maslahi ya wananchi. Aombe msamaha pale aliposimamia haki ya wananchi ili iweje? Wee nambie kama Mnyika angeomba msamaha kingetokea kitu gani zaidi kama sii kufuta hoja nzima!.

Jamani JK mwenyewe anaelewa kwamba hakuna njia ya kukosolewa kiongozi isipokuwa kwa kuonyesha sehemu alizokuwa na udhaifu nazo. Na bungeni ni mahala safi na pekee panaporuhusu Upinzani kuonyesha udhaifu huo iwe bajeti, sera au kiongozi. Hizi kanuni za kumkuza mtu kama Mungu au mtume ni kufuru kwetu sisi wengine kulingana na imani zetu. JK atakosolewa pale alipokosea, ni binaadam kama walivyo wengine isipokuwa heshima yake kama rais atapewa na tunampa sote iwe bungeni au mikoani. Tunampenda sana laa sivyo asingeweza kuendelea kutawala.

Binafsi yangu nampenda na kumpa heshima zote tena naweza sema ktk viongozi waliojitahidi sana kuijenga nchi yetu basi yeye mmoja wao isipokuwa anaongoza WATU walopoteza Uzalendo, na ktk MAZINGIRA ambayo hana uwezo nayo. Ameshindwa kuchukua maamuzi magumu sii mara moja kwa kuhofia chama chake ama kuchukua lawama za watu na huu ni udhaifu kutokana na hali halisi.

Na Mnyika ni mmoja kati ya wabunge waliotaka achukue maamuzi magumu zaidi, udhaifu kila mtu anao nakumbuka enzi za kucheza mpira ukiwa beki watu wanakatiza kwako unaitwa umelegea, wakisema Jikaze mwanamme mbona umelegea! haikuwa tusi hata kidogo kwa sababu timu ilikuwa inafungwa na wewe ndio ulikuwa njia ya mkato..Wewe ndio sababu ya kushindwa, sasa ukianza kufikiria neno UJiKAZE na kusema wamekutukana basi wewe ndio huta improve ktk uchezaji.

JK is good but not good enough kulingana na hali aloikuta, hivyo kauli ya Mnyika ni kumwambia rais wetu aongoeze nguvu na makali ktk uongozi wake. Maadam UONGOZI BORA ni nyenzo kubwa ya maendeleo haitakiwi kuchukuliwa kiholela na kuogopana - Call spade a spade!
 
Back
Top Bottom