Picha za Makamanda Vitani na Wapiganaji wao: CHADEMA yaweza kujifunza somo?

Mwanakijiji napingana na wewe kabisa.

Kununua nguo ni garama. Nguo zenye rangi ya bendera ya CDM au CCM au magwanda ya CDM ni garama.

Pamoja na garama hiyo, lakini nguo na hapa naongelea sare, lazima zivaliwe, kwani ni kama ishara.

CCM (mathalani kwa huyo mtoto uliyemwonyesha) wana uwezo wa kugaramia sare kwa washabiki wao (tembea maeneo ya vijijini, uangalie ni watu wangapi wana t-shirts zao).

CDM, hawana uwezo wa kugaramia sare kwa washabiki wao. Kama nilivyosema awali, kama ishara ya haiba na mwonekano wa chama (naamini unajua maana ya magwanda kwa CDM) ni lazima ivaliwe japo kwa wale wenye uwezo.

Ukifananisha na jeshi, unajua kuwa hata uwe na uwezo mkubwa kiasi gani kifedha, hauruhusiwi kujinunulia na kuvaa nishani za vyeo ambavyo hauna. Ila kwa CDM, mtu yeyote, anaruhusiwa kununua na kuvaa gwanda hata kama ni kali kuliko la Mbowe, kama ana uwezo.

Kuhusu staili ya kuzungukwa na watu walioshikana mikono, naamini ni staili tu ya kurahisisha ulinzi kwa viongozi wao. CDM wamefanya maandamano mengi sana nchini, wamekutana na changamoto nyingi, wamekabiliana nazo kwa staili tofauti, na naamini pengine kwa sasa wanaona staili hiyo ndiyo yenye inayofanya kazi pengine kwa garama ndogo wanazoweza kuzigaramia.
Hiyo Ulowashauri, nayo ni nzuri, lakini nahisi inaweza kuwa na garama zaidi, kwani unajua kuwa kila mtu anaruhusiwa kuvaa magwanda, na kama ukisema walinzi wavae sare tofauti na watu wengine, tayari unajenga haiba fulani ya kulindwa na watu ambao 'sio wenzetu'.
Ahsante
 
Makamanda na wapiganaji wa CHADEMA wanatofautiana sana kama mbingu na dunia. Acha tu watofautiane hata kwa mavazi haya.
 
Mkuu kwa mara ya kwanza nimeshindwa kukuelewa, na hoja yako imekosa mifano inayoeleweka ili kuiunga mkono. Naliona tatizo kubwa liko kwenye maneno haya...
Niliandika jambo hili zaidi ya mwaka mmoja uliopita sipendi mavazi ya mgambo ya Chadema ambayo yanawatenganisha viongozi wao na wanachama wao
na si uniformity kama ulivyodai maana umetoa mfano wa vazi la CCM....Hebu angalia hapa kuna Uniformity...?

05_11_qv7s9r.jpg
 
Wakati tunaelewa vizuri umuhimu,ulazima na faida za kuwa na sare kwa askari/wanajeshi wa vikosi rasmi vya ulinzi na usalama,hasa wawapo vitani. Na huku nikikubali kuwa ni vyema makamanda wavaa sare sawa na wapiganaji wengine wa kikosi kimoja; Nadhani ni vyema tukijiuliza umuhimu au faida za sare kwa wapambanaji wa kisiasa kama wale wafuasi wa vyama na viongozi wao. Hapa sizungumzii ulazima kwani siamini kwamba ni lazima. Mathalani mimi na wewe ni wana PPT-MAENDELEO,hebu tujiulize hapa:

  1. Kama ni kuonesha umoja, basi tuelewe ni umoja na akina nani? Je ni wanachama na wafuasi wenzetu wa chama tu? Kama ndivyo basi ni vyema tukihimizana tuvae sare ili tujipambanue. Lakini Je hatutamani kuwa wamoja na wengine ambao si wafuasi na wapenzi wa chama chetu?
  2. Kama ni kupamba na kupendezesha mandhari pale tunapokutana, je tunapamba ili nani afurahie, sisi wenyewe au wanaotuangalia? Na je ni ipi nafasi ya wanaotuangalia kuja kuungana nasi na hata kusogea mbele na kubeba bango,ilhali hajavaa sare japo amehamasika kama sisi? Na je aliyevutika na kupendeza kwetu, na rangi zetu, ataendelea kuwa na sisi kikitokea chama ambacho kina sare za kupendeza zaidi yetu?
  3. Kama ni namna ya kuonesha mapenzi na loyalty kwa chama; je ipi nafasi ya mpenzi na shabiki wa chama ambaye hawezi kununua sare? (si unajua PPT hatuwezi kugawa fulana na kofia bure? )
  4. Kama ni sababu za kiulinzi na kiusalama,je tunajilinda dhidi ya nani? au tunamvamia nani?

Lakini kabla sija-conclude, labda tujiulize pia, tunapungukiwa nini tukiwa na ufuasi mkubwa watu ambao hawana sare ila wana mapenzi na chama? Kama tunapungukiwa je sare ni kila kitu kinachoweza kutukamilisha?
Kwa mtazamo wangu, suala la sare pamoja na umuhimu wake linaweza lisiwepo kabisa katika orodha ya mambo ambayo CDM,kama ilivyo na PPT yangu, inapaswa kuyafanyia kazi,walau kwa sasa. Orodha ni ndefu sana yakiwemo mambo mengi ambayo tumeyajadili hapa JF.
Magwanda wakivaa viongozi wao na wanachama waandamizi yanatosha nadhani kama SYMBOL yao; kama vile ambavyo hatuna mlingoti wa bendera kila nyumba na kila ofisi. Mwenye kuweza kununua kofia haya,mwenye fulana hayaa, lakini uma wote ujione na nafasi ya kujiunga nao bila "kizuizi" cha SARE. It's PEOPLE'S POWER they say,isn't it?
 
Yes & No. But I cannot tell you pyschologically haya magandwa ya kaki yana impact gani kwa vijana na watanzania waliopigika kimaisha. Watu wanapagawa (literally) wakiwaona hawa wandugu 'DANTAUNI' ndani ya magwanda. Sasa hivi huku mtaani akipita kijana kavaa hata sharti la rangi ya kaki watu wanamwangalia mara mbili mbili na niseme anaonekana (1)jasiri (2) kachoka ufisadi (3) brave /can speak his mind na hana nidhamu ya woga.

Ukiangalia picha za zamani around Independence time Mwl Nyerere alikuwa anavaa nguo za kimgambo mgambo. Kuna uwezekano CDM are trying to revive feelings za kwamba tuko kwenye harakati za kujikomboa hivyo wanatoka kwenye CDM-political party na kwenda kwenye CDM freedom fighter. Kwa sasa wakirudi wote kwenye nguo za CDM wanaweza kuondoa hizi 'intrisic value' za kwamba wako beyond politics! Kwenye vita mtutu una-limitations zake so you have to have pyschological touch!
 
of coz mavazi na upiganaji wapi na wapi haijawai kukatazwa mwanachama kutovaa mavazi ya kipiganaji and ofcoz hatuko kwenye sherehe za sare tuwe na nia moja ya kuondoa unyonyaji na kukemea maovu tumeshawekwa kimatabaka sana,sasa tuwe pamoja kujitoa regardles on what tumevaa
 
Nadhani tutaelewana tu

nimekuelewa mwanzoni tu wa article yako, nimemalizia kwa sababu ni tamu, nilivyomaliza nimeelewa sana

This is truly an inputs that Chadem need to work on it immediately...Re-branding is very common, we have seen how Voda and Airtel have done that, the situation is unavoidable especially when logical reasoning and comments like this is posed.
 
Yes & No. But I cannot tell you pyschologically haya magandwa ya kaki yana impact gani kwa vijana na watanzania waliopigika kimaisha. Watu wanapagawa (literally) wakiwaona hawa wandugu 'DANTAUNI' ndani ya magwanda. Sasa hivi huku mtaani akipita kijana kavaa hata sharti la rangi ya kaki watu wanamwangalia mara mbili mbili na niseme anaonekana (1)jasiri (2) kachoka ufisadi (3) brave /can speak his mind na hana nidhamu ya woga.

Ukiangalia picha za zamani around Independence time Mwl Nyerere alikuwa anavaa nguo za kimgambo mgambo. Kuna uwezekano CDM are trying to revive feelings za kwamba tuko kwenye harakati za kujikomboa hivyo wanatoka kwenye CDM-political party na kwenda kwenye CDM freedom fighter. Kwa sasa wakirudi wote kwenye nguo za CDM wanaweza kuondoa hizi 'intrisic value' za kwamba wako beyond politics! Kwenye vita mtutu una-limitations zake so you have to have pyschological touch!

Wow! This sound convincing! However, is it not that the same nguo may look like people who are ready for shari anytime?
 
nimekuelewa mwanzoni tu wa article yako, nimemalizia kwa sababu ni tamu, nilivyomaliza nimeelewa sana

This is truly an inputs that Chadem need to work on it immediately...Re-branding is very common, we have seen how Voda and Airtel have done that, the situation is unavoidable especially when logical reasoning and comments like this is posed.

You can not copy & past techniques za Corporate branding and apply them onto 'politcal party' branding. they will simply make a mockery out of you.
 
majeshi huvaa sare kwa sababu za kiusalama,wanagharamiwa na kodi za wananchi pia wapo kambini,CDM ni makamanda wa ukombozi wa pili kwa watanzani,sare za mapambona zipo mioyoni mwa wanachama na wakerekwetwa wa ukombozi,na hizo unazotaka zipo zinauzwa na si kwa viongozi tu!
 
kombati ni vazi ambalo kwa chadema limebuniwa na mbowe mwaka 2003 tarifa hii mliipata kwenye kongamano la wanafunzi wa vyou vikuu dodoma alisema kuwa alikua anapenda kuwapata vijana wengi na pia linaonesha ukakamavu pia alisema kuwa halijapitishwa kwenye vikao vya chama kuwa vazi la chama kwa hiyo ni ubunifu wa mbowe alafu watu wakaiga sasa hivi ukimuona mtu anavaa gwanda utamjua tu huyu chadema pia alikua anajua litasapoti faisafa nguvu ya uma
 
Hivi chadema ni wapiganaji wanao pigania nini? Mie naona ni wanasiasa tu, tena siasa mbovu, za manung'uniko yasiyo kwisha kila kukicha. Wapiganaji wana nug'unika? Nashanga!
 
Kwanza kushona magwanda ni gharama kubwa na sio kila mpenzi wa chama anaweza kuimudu hiyo gharama. Hivyo wanaovaa magwanda ni wale wanaojiweza na hii inaleta utengano katika kadamnasi badala ya umoja. Lakini Kama ni lazima kuvaa magwanda basi CHADEMA wavae magwanda ya rangi za chama na sio rangi ya khaki. Unaweza kabisa ukabuni gwanda lenye rangi za chama na ukaoneka jasiri. Cha muhimu katika Gwanda ni ushonaji na sio rangi. Kama tunadai wao ni wabunifu basi watumie huo ubunifu wao katika hili. Wale wasio na uwezo wa kushona gwanda watavaa rangi za chama na wote watajiona level moja. Waache kuvaa magwanda yanayofanana na polisi na mgambo ambayo yanawatisha wananchi. Wako watu wengi wanaipenda CHADEMA lakini wanachelea kuiunga mkono kwa ajili wanayaogopa hayo magwanda yanayofanana na polisi na mgambo ambao ni wabakaji wakubwa wa haki zao.
 
Wow! This sound convincing! However, is it not that the same nguo may look like people who are ready for shari anytime?


Waberoya, ccm tried to brand them but it didnt work. Ndani ya magwanda wanaongea issues zinazogusa wananchi na zaidi wana-track record to inayoonesha indeed cdm can 'walk the walk and not talk the talk'
 
Wave tu rangi za zchama kama wanachama wengine. Its about time to ditch magwandaz
Mkuu nafikiri tupo kwenye kipindi cha mpito kuikwamua nchi kwenye mikono dhalimu.for now mavazi sioni kama kikwazo kwa cdm.endelea kama unavyofanya kuwashauri cdm but for this not now plz tusijaribu kufanya yote kwa mpigo.but kwa wanaojua dizaini,kitambaa na rangi ya tunayoita magwanda ya cdm pls hayafanani na mgambo! Au ndo yale ya ule uji wa yebo yebo na zile kandambili? Tuwe makini isijekuwa "just I dont like it" alafu tuna transfer kwa watu huo mtizamo.mitaani cku hizi mavazi ya cdm yameanza kuwa fashen hata mm nimeshangaa yanavyopendwa na vijana.nafikiri tusifanye kila wanachofanya ccm isipokuwa pa msingi.nameelewa falsafa ya MM na kuihusisha na mbinu za kijeshi lakini inabidi tujue pia aina gani ya vita tunavyopigana.vita kubwa ni elimu ya uraia kwa watz then hayo mengine yatakuja tukiwa na msingi imara wa elimu ya uraia.Heshima kwako mkuu.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom