kamandamakini
Senior Member
- Feb 17, 2012
- 165
- 137
Leo mbunge Msigwa akisindkizwa na mbunge wa arumeru mashariki Mh. Nassari aka dogo janja wamepiga mkutano wa nguvu iringa mjini, katika mkutano huu kada wa zamani alie vua gamba na kuvaa gwanda pia alikuwepo ndugu bananga, Mkutano ulihudhuriwa na wakazi wengi wa mji wa iringa na vitongoji vyake huku wananchi wengi wakionekana kuvutiwa na viongozi hawa.
Akiongea na wananchi wajimboni hapa mbunge Nassari ameweza kuwaeleza wanairinga kwamba jimbo la iringa nawananchi wake walikua na mchango mkubwa katika kumfanya yeye apate ubunge kwakile alicho dai kwamba mbunge wao Msigwa alifanya kazi kubwa katika ushindi huo, akikiongea kwa nafasi yake Mh. Msigwa ameendelea kuwa taka wananchi wa iringa wawapuuzee na kudharau propaganda za wanaccm ambao wanajaribu kudanganya na kuleta fitina zisizo na msingi.
Katika hatua nyingine ameweza kugawa zawadi kwawatoto wa shule walio jitokeza mkutanoni hapo ikiwa ni pamoja na madaftari, kalamu na lula. pia ametoa jezi na mipira kwa timu zilizo kuwa zime muomba mkutanoni hapo.
Kwa upande wake kamanda Bananga amewaeeleza wana Iringa kuwa Mbunge waliyemchangua hawakukosea kwani umakini wake unadhihirika.
Wanachi waliweza kupata fursa yakuuliza maswali na pia kutoa michango na kero zao ili Mh. Msigwa awezekuwakilisha vyema bungeni.
Moja ya swali lililokuwa gumu kwa Mh. Msigwa ni lile lililoulizwa na mtoto alietaka kujua ni kwanini Rais Kikwete aliweza kutoa rambi rambi ya million 10 kwenye msiba wa Steve Kanumba na kushindwa kutoa rambirambi yoyote kwenye msiba wa marehemu Daudi Mwangosi.
Mwisho wananchi waliweza kumchangia mjane wa mwangosi kiasi cha zaidi ya laki mbili.
chanzo:MH. PETER MSIGWA BLOG