PICHA: Rais Kikwete katika ziara rasmi Ottawa, Canada

''Mwanajeshi'' wetu mbona ''marching'' yake haiendani na hao wanajeshi wengine?.......left....right......left......... right
I see...kweli penye wengi pana wengi.....sasa wewe umeenda hadi huko miguuni kutafuta nini.....ah....labda wao wanatembea ki-Canada bwana.....tutajuaje sisi!!!
 
ahhhaaa hili TAIFA kweli Rais tunaye, hivi kagame huwa naenda kwenye anasa na tafrija namna hii? anapokelewa na waziri wa mambo ya Nje, duh heshima ya tanzania Nje kwisha.

Mkuu PhD naona umepata avatar hapahapa
 
Acha wivu wewe mwenzako anakula matunda yake aliyoyachuka katika ujana wake.nasi tuwe na ndoto kama hizi jamani eboooooooooooooooooooooooooo.
 
BEFORE

Bartlett%252520with%252520Jakaya%252520Mrisho%252520Kikwete%252520and%252520wife%252520at%252520Mystic%252520Mountain.jpg



attachment.php



NOW

attachment.php


Dah! ... Vasco Bwana!
.
Wamemheshimu kwa kumpa farasi mweusi kama yeye.
 
Royal parade ya wapi mheshimiwa anaangalia mikia ya farasi badala ya parade ya wanajeshi ? HIYO PARADE IKO MSITUNI ? HIYO KALI NA ANA KESI YA KUJIBU.
 
Wengi humu wanaongea kuhusu kusafiri kwa JKkwakuwa hajawahi hata kupanda ndege ndio maana, same people ukiwapa passport inayoruhusu kusafiri kila nchi bila visa na pesa wangekuwa kila sehemu, ukitaka kuamini amgalia watz wangapi siku hiZi wanaenda south Africa as tourist.Kama Jk hasafiri hatawezaje kuattract investor AMA kuPata hiyo misaada Hama watachart kwenye Facebook, inabidi afanye trip ilihaweze kukutana na wafanyabiashara billionaires iliwaweze kuja Tz.Mimi sioni tatizo kwani mambo yako tight kila sehemu kuPata hata huo mkopo inabidi waangaike hakuna nchi inayotoa pesa tu hivi hivi.Kama nikiangalia hapa Uk David PM katoka US na Brazil two weeks ago sijasikia malalamiko kwani waingereza wanajua wanaitaji
 
mkuu Papizo umeandika kwa hisia kali sana kutokana uchungu ulionao kwa nchi yetu!

Mkuu wangu sana huyu jamaa hayupo serious kabisa na kila kitu kwake anachukulia simple tu,anaifanya nchi kama yake hivi,ina maana kila safari lazima asafiri yeye tu kuna umuhumu gani??
 
Ndio alichoenda kufanya huko kupewa heshima na kupanda farasi, Rais kweli tunae na tuna safari ndefu sanaaaaa

Hizi picha zingine Ikulu si wangekuwa wanazivisha nguo, khaaaaa! Jana bembea leo farasi. Huenda ndio protocol ya wacanada hiyo lakini kwa watu wa kwetu kuona Rais wao yuko kwenye mifarasi hata haipendezi!

Kwani kila picha lazima iwe for public?
 
Sasa kuna makosa gani rais kufanya Ziara nchi za nje kwenda kuzungumza na mataifa mengine.

Huoni kama hizo ni learning opportunities kwa Mr Presient na delegation yake?

Tangu aanze kusafiri hizo "learning opportunities" hazijatosha tu,mbona hatuoni kwa vitendo akizifanyia kazi?
 
Nchi jirani za afrika mashariki zina marais sisi tanzania tuna kikwete j.m
 
First lady kaogopa nini? Bado hajaenda Alaska na Korea Kaskazini sijui kama Urusi keshafika ingekuwa vizuri akamalizia mzunguko kabisa tujue moja
 
Kweli anapendeza sana.....ila nina maoni binafsi. Ningependa kama katiba hii tuliyonayo ingepindishwa kidogo ili Rais awe Rais na wakati huo huo awe Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 
Mbona sijawai kuona USA akifanyiwa hivi.!

akienda kwa kazi ya kiserikali na akawa mgeni wa serikali hiyo atafanyiwa hivyo pia tatizo huwa anaenda kwa matembezi yake binafsi. na mizunguko isiyo rasmi.
 
Ama kweli JK it is soo very dangers kwa jamii yetu.......!!!!


attachment.php


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitambulishwa kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada Mhe. John Baird baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Macdonald Cartier jijini Ottawa, Canada, kwa ziara rasmi ya siku mbili jijini humo Oktoba 4, 2012

attachment.php

attachment.php

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika viwanja vya jumba la Rideau Hall jijini Ottawa, Canada, katika hatua yake ya kwanza ya kuanza ziara rasmi ya siku mbili jijini humo Oktoba 4, 2012. Jumba hilo ndilo makazi na ofisi rasmi ya Gavana Jenerali wa Canada tangia mwaka 1867 ambapo pamoja na kuishi humo pia hapo ndipo hutumika kwa kuwatunukia wananchi wa Canada waliofanya vyema, pa kupokelea wageni mashuhuri wa nchi za nje na pia ndipo anapofanyia shughuli zote za kitaifa akiwa kama mwakilishi wa Malkia wa Uingereza.

attachment.php

attachment.php

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi katika viwanja vya jumba la Rideau Hall jijini Ottawa, Canada, katika hatua yake ya kwanza ya ziara rasmi ya siku mbili jijini humo Oktoba 4, 2012. Jumba hilo ndilo makazi na ofisi rasmi ya Gavana Jenerali wa Canada tangia mwaka 1867 ambapo pamoja na kuishi humo pia hapo ndipo hutumika kwa kuwatunukia wananchi wa Canada waliofanya vyema, pa kupokelea wageni mashuhuri wa nchi za nje na pia ndipo anapofanyia shughuli zote za kitaifa akiwa kama mwakilishi wa Malkia wa Uingereza.

attachment.php

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea heshima ya kupigiwa mizinga 21 katika viwanja vya jumba la Rideau Hall jijini Ottawa, Canada, katika hatua yake ya kwanza ya ziara rasmi ya siku mbili jijini humo Oktoba 4, 2012.

attachment.php
 
nyie leteni tu hizi picha hamjui mnazidi kupandisha mori watu kuusaka kwa udi na uvumba. Baba wa taifa alisema Urais ni mzigo ila hapa kwenye hili gari la farasi kuna mzigo kweli?

Hebu ngoja na mimi nione kama naweza kugombea kama BINAFSI, inavutia kwa kweli - teh teh teh
 
nyie leteni tu hizi picha hamjui mnazidi kupandisha mori watu kuusaka kwa udi na uvumba. Baba wa taifa alisema Urais ni mzigo ila hapa kwenye hili gari la punda kuna mzigo kweli? maana huwezi kukumbuka chochote hata sakata la gasi ya ntwara lazima lifutike kwa muda

Hebu ngoja na mimi nione kama naweza kugombea kama BINAFSI, inavutia kwa kweli - teh teh teh
 
SnS picha inaongea zaidi ya maneno! Surely JK amechoka sana!!!!

Yupo tu, muda uende nina uhakika ile tamaa yake imekwisha kabisa!!!

Wanamuita DEGE John, Kazi tunayo KODI ZETU MSHIKAJI ZAKE STAREHE TU.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom