Elections 2010 PICHA: Mwanza Yalipuka - Mkutano wa Slaa

Jamani nyie acheni tu!! Mchana tulipigwa mabomu Furahisha lakini bado jioni tukarudi tena Magomeni., Mngeona watu walivyokuwa wanamsubiri kwa hamu,, alivyoingia kwenye saa kumi na mbili hivi watu wakawa wanimba Raisi raisi raisi yaani inaleta rahaaaaaaaaaaa. Alivyouona ule umati wetu akasema, "jamani watu wa Mwanza, mnanifanya nitokwe machozi kuuona umati wenu". Jamani watu walimshangilia na ilikuwa akitaka kuongea watu wananyamaza kimya, akiongea pointi wanashangilia na kunyamaza ili kumsikiliza. Ama kweli tuombe MUNGU wapige kura wote kwa hakika ushindi wa Slaa mwaka huu utakuwa ni wa kishindoooooooooo!!
 
Ukichemka 2015 tunakumwaga pia.
Jamani tusiseme hivi ila tumwombee kwa Mwenyezi Mungu ampe utashi wa kutuongoza kwa hekima na busara na aondoe dhuluma zote hapa nchini ili kila Mtanzania afaidike na matunda ya uhuru wa taifa hili................tusianze kuweka mashaka mashaka haitatusaidia kamwe............Alipo Mwenyezi Mungu neema na riziki yetu ipo tu.........
 
Jamani mbona mi siioni hiyo picha??? mi machozi yamenitoka kuona kila m2 sasa anaelewa kwa nini thithiem ishindwe!!!!! Mungu ahsante kwani sasa tunajua uko pamoja nasi

Anzaneni kufuatilia na kukunguta vumbi la kadi za kupigia kura, usije kuta mende wamesha kula nusu afu ikawa tabu.
 
Nilipigiwa simu juu ya kujaa FFU katika jiji la mwanza tangia asubuhi, watu wengi ambao walikuwa na mpango wa kuhudhuria walishindwa. Hawa hawakubebwa na mabasi na madaladala kama wanavyobebwa kwenda kuhudhuria mikutano ya chama kilee, hawa hawakupewa t-shirt, kanga kofia na maji ili wahudhurie mkutano, bali walikuja wenyewe kwa utashi wao. Tuseme nini sasa jamani, the time of change is today
 
sababu waliyozuilia kiwanja cha Furahisha adi sasa wamenishangaza
ccm kirumba ya ccm...
shida matokeo ya kura kama yatakuwa ya haki!!
lets see
 
Hakika saa ya ukombozi imewadia. Mola amesikia kilio cha waja wake. Kilichobaki sasa ni kwa wale wote waliokwishazinduka toka usingizini kuwaamsha ndugu na jamaa zao ambao bado wako usingizini, hasa katika mikoa ya LINDI, MTWARA na PWANI kwamba sasa kumepambazuka.
 
japo wengi waliondoka baada ya kufukuzwa uwanja bado ulijjaaaaaa aaaa lol

Je kama ungekuwa ni uwanja wa FURAISHA si wangefika mpaka kule mwisho maaana ule uwanja ni zaidi ya viwanja viwili vya mpira nadhani ndio maana walifanyiwa mizengwe.

Na kama kweli hao watu wote wataenda kupiga kura basi CCM iko matatani sana na ndio maana nimepata tetesi JK anaenda mwanza na hilo ni wazi kuwa nyamagana Masha nae anawakati mgumu sana

 


Je kama ungekuwa ni uwanja wa FURAISHA si wangefika mpaka kule mwisho maaana ule uwanja ni zaidi ya viwanja viwili vya mpira nadhani ndio maana walifanyiwa mizengwe.

Na kama kweli hao watu wote wataenda kupiga kura basi CCM iko matatani sana na ndio maana nimepata tetesi JK anaenda mwanza na hilo ni wazi kuwa nyamagana Masha nae anawakati mgumu sana


washashi hawana masihala wakiamua kitu!!
 
Mimi binafsi niko Dar es salaam, na kata ninayoishi nimegunduwa watu wanapenda sana pombe, huu ni utafiti ambao nimeufanya kwenye chaguzi mbalimbali, kwa nini hawa watu huwa hawapigi kura? sasa basi kwa kuwa mungu ameamuwa ccm sasa basi nimeoganaizi na mtandao wa wamiliki wa baa zote katika kata yangu, kwamba siku ya uchaguzi baa hazitofunguliwa mpaka saa nane mchane, wamenielewa na wamekubali, wamesema hawawezi kupata hasara kwa masaa kwa kufaniisha tukio ambalo linafanyika mara moja kila baada ya miaka mitano. shime kama kuna mdau hasa kule arusha tumieni huu mkakati ambao nimeusisi. ccm hawatoki mwaka huu.:A S thumbs_up::A S thumbs_up:
 
Umati mkubwa wa wakazi wa mji wa Mwanza na vitongoji vyake wakiongozwa na viongozi na wafuasi wa Chadema, jana walifurika katika uwanja wa Magomeni Kirumba, kumsikiliza mgombea urais kupitia chama hicho, Dk. Slaa, saa chache baada ya askari polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kuwatawanya katika uwanja wa Furahisha, ulioko mjini hapa.

Watu hao walianza kumiminika kama mvua uwanjani hapo, kuanzia saa 7:00 nchana na hadi kufika saa 10:00 jioni, ulifurika kiasi ambacho hakukuwa na nafasi ya mtu kuweza kusimama katika eneo la uwanja huo.

Hali hiyo iliwafanya baadhi ya watu kulazimika kupanda juu ya miti na wengine kusikiliza hotuba ya mgombea huyo wa urais wakiwa wamesimama eneo la mbali ya uwanja huo.

Hata hivyo, wakati hali ikiwa hivyo, hakukuwa na ulinzi wa polisi, baada ya askari wa jeshi hilo kushindwa kukaribia eneo la mkutano kwa ajili ya kuweka ulinzi kama ilivyo kwaida.

Hali hiyo ilizua hofu kubwa muda wote wa mkutano juu ya usalama wa watu waliokuwapo uwanjani hapo.

Kutokana na hali hiyo, Mratibu wa Kampeni za Dk. Slaa, Suzan Kiwanga, aliwataka walinzi wa chama kuimarisha ulinzi.

Dk. Slaa aliwasili uwanjani hapo saa 11:52 jioni na kushangiliwa kwa sauti kubwa na umati wa watu waliofurika.

Mara baada ya kuwasili na kushuhudia umati huo, Dk. Slaa alishindwa kujizuia na kujikuta akitamka: “Kwa wingi huu mnanifanya nitokwe na machozi.”

Aliwashukuru wananchi hao kwa mahudhurio makubwa waliyoyaonyesha kwake na kusema: “Kwa mapenzi mliyonionyesha nitawatumikia kwa uaminifu.”

Aidha, aliwapa pole watu waliojeruhiwa katika mashambulizi ya mabomu ya kutoa machozi yaliyofanywa na FFU katika uwanja wa Furahisha.

Akihutubia mkutano huo, Dk. Slaa alisema katika kufanya maamuzi magumu kuhusu kufuta kodi ya serikali katika vifaa vya ujenzi, hatatazama nchi za Afrika Mashariki, kama anavyotaka Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashriki, Dk. Diodurus Kamala kwa vile maamuzi atakayochukua ni kwa ajili ya maslahi ya Watanzania.

“Nasema sitakuwa na woga katika kufanya maamuzi kwa ajili ya maslahi ya Watanzania,” alisema Dk. Slaa.

Nipashe
 
washashi hawana masihala wakiamua kitu!!

Teh teh Umenikumbusha Mgombea wa Chadema Mr. Wenje ni mtu wa kutoka Tarime na washashi wamejaaa huko Igogo/Bugando/Mabatini kuelekea nyakato duhhhh mbona makubwa na huko Buzuruga si ndio hatopata kabisa ndugu yangu Masha

 
Yaaani ukisikia timu beki hazikabi bass ndo JK na hake ya kampeni....hahaaaa atarudi mwanza hat a Mara 5 mwaka huu mwisho aje aanguke
 
Pamoja na Polisi kuwatawanya wafuasi na wanachi kwa mambomu katika viwanja vya Furahisha..Umati mkubwa wa watu ulijitokeza kumsikiliza Dr.Slaa jana jioni mjni Mwanza.

Tazama picha..maana umati huo ni sehemu tu ya watu.Umati wa watu umeacha gumzo kubwa mjni mwanza...waliohdhuria wataelezea zaidi
 
Thank you maana naona hawataki kabsaa kumsikia huyu jamaaa, hivi kweli hawatamzushia kuwa sio mtanzania??? Maana kule Karatu wengi ni wahamiaji...Naogopa sana
 
slaa_mwanza.jpg


Mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, akiwahutubia maelfu ya wakazi wa Jiji la Mwanza na vitongoji vyake, katika mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Magomeni, Kirumba .



kama mwanza imeripuka tutaenda kuizima tarehe 31.10 tu haina shida kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom