Mkuu swala sio nani kafanya nini isipokuwa swala ni wewe kujiuliza kwa nini unachukua Upande?..Wewe mwenyewe umeshaona kosa moja sii kosa isipokuwa jingine na kwa kutumia karata ya Udini. Mimi nawasoma nyote humu kila mmoja wenu anavutia dini yake wakati hizi ndizo sababu zilizotufiisha hapa tulipo...hawa waislam wana wivu sn,sasa kesi ya kukojolea quran yaan ndo wameharibu hadi vifaa vya kanisani na kuharibu makanisa! wana uhakika gani km aliefanya hivyo ni mkristo au wameona anaitwa emmanuel basi wakajua ni mkristo.
Hivi inafikia nini kijana kukojolea Kuruan? Unapofundisha watoto wako na kuwaambia Uislaam ni dini ya SHETANI unategemea nini mtoto wako atafanya kesho?. Je, inakuwaje vijana wengine wakachome makanisa na sio kuitaka sheria maana wamefundishwa wakristu ni Makafir tu.. Kwa nini vita vianze kwa kutazam nani kavaa kanzu, hijabu na mwenye sigda usoni kuwa alama ya mwenza au adui - UDINI. Kama mlikuwa hamjui UDINI huwa hauna logic wala mantiki basi ndio leo mtafahamu..Endeleeni na matusi yenu lakini mfahamu ya kwamba mnakaribisha na kupandikiza mbegu mbaya sana. Sitoshangaa kama haya mambo hayajaisha bado kiporo..