Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 863
Wakuu, Salaam!
Jana nilikuwa kwenye maandamano katika Wilaya ya Chato nyumbani kwa Maghufuli ambako kulikuwa na umati mkubwa wa watu. Maandamano yalikuwa ni ya Kilometa nane yaliyoshirikisha magari,pikipiki na waendao kwa miguu. Baada ya maandamano kama kawaida ulifanyika mkutano mkubwa wa hadhara. Leo wakati tunarudi Mwanza tukafanya maandamano madogo na mkutano wa hadhara katika Kata ya Katoro jimboni Busanda ambako nako watu walijitokeza kwa wingi. Hakika watanzania wameamua kuunga mkono mabadiliko. Kama tungeanza mapema vuguvugu hili nadhani saa hizi tungekuwa tunazungmza mengine kabisa.
Maandamano Kanda ya Ziwa ndio yamehitimishwa na baadhi ya Viongozi wamesharejea kwenye Makazi Yao. Wengine bado tupo hapa jijini Mwanza tunakula Sato. Tumehitimisha kwaajili ya kufanya tathmini na kujipanga upya kwaajili ya Kanda zingine.
Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke.
Kutoka Jijiji Mwanza
Regia E Mtema
Waziri Kivuli- Kazi na Ajira.
============================
Jana nilikuwa kwenye maandamano katika Wilaya ya Chato nyumbani kwa Maghufuli ambako kulikuwa na umati mkubwa wa watu. Maandamano yalikuwa ni ya Kilometa nane yaliyoshirikisha magari,pikipiki na waendao kwa miguu. Baada ya maandamano kama kawaida ulifanyika mkutano mkubwa wa hadhara. Leo wakati tunarudi Mwanza tukafanya maandamano madogo na mkutano wa hadhara katika Kata ya Katoro jimboni Busanda ambako nako watu walijitokeza kwa wingi. Hakika watanzania wameamua kuunga mkono mabadiliko. Kama tungeanza mapema vuguvugu hili nadhani saa hizi tungekuwa tunazungmza mengine kabisa.
Maandamano Kanda ya Ziwa ndio yamehitimishwa na baadhi ya Viongozi wamesharejea kwenye Makazi Yao. Wengine bado tupo hapa jijini Mwanza tunakula Sato. Tumehitimisha kwaajili ya kufanya tathmini na kujipanga upya kwaajili ya Kanda zingine.
Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke.
Kutoka Jijiji Mwanza
Regia E Mtema
Waziri Kivuli- Kazi na Ajira.
============================