Picha: Kasri a.k.a Nyumba Mpya ya Mh. Mchg. Dkt Rwakatare ktk ufukwe wa Bahari

'Mnanijengea jumba kuuuuuuuuubwa, kwani mimi tembo'
 
huyu mama ni mmoja wa matapeli ndani ya ccm na taifa. ana maovu mengi kuliko mmjuavyo. ubunge amepata kwa rushwa na anapata tenda ya mitihani ya taifa f2 kusahihishwa shuleni kwake huku ukifanyka udhurumaji mkubwa kwa walimu
 
Pamoja na Hongera nasikia Mch. Rwakatare hana mume lakini jina analotumia ni la mumewe waliochana naye, ni kweli? lakini anafundisha watu waishi vizuri na ndoa zao ukweli uko wp????????????
 
Tufanye kazi kwa bidii ndiyo tutafanikiwa..tuachane na mambo ya wivu..unafanya kazi masaa 2 alafu uje ufanikiwe lini..haujiongezi kupata source nyingine ya pesa..ukitoka kazini -bar-nyumbani.alafu mafanikio utapataje..
 
Ndiyo maana WALIKIPIGA sana vita Kibabu cha Loliondo na wanaendelea kukisakama.

Babu wa Loliondo alikuja na kasi ya ajabu na kuwaweka chini wote.

Vipato vyao vikaanza kupungua na sasa vimerudi kwa kasi kubwa.

Hivi hawa wanaombea watu huwa Wizara ya Afya inakwenda kuwapima kweli kama wamepona?

Naweza kumwamini zaidi Babu kuliko hawa ambao kwa mbaali tu unanusa UTAPELI.
 
Sadaka huwa hazina jasho isipokua kununua vikapu vyakutosha, ila faida zake ndio hizi.
 
Ama kweli pesa haidanganyi kamwe

Hawachelewagi kusema hizo nguzo (Pillars) za nyumba ya mchungaji ni za Kifreemanson!!!!


entrance.png
 
Mungu tunusuru ,sasa cha kufungua nyumba na sherehe ndo nini?ingekuwa vyema kama angewaalika wachungaji wenzake wakaibarikikwa maombi,sasa hapo anawaambia nini waumini wake?naweza wadhurumu na kujenga mjengo kama huu ,kudadeki zenu,this is tooo much .
 
Nimejifunza kitu kimoja, hakuna kitu mwandamu atafanya asipate Upinzani. Lakini ninasikitika sana mtu anyemtafuta Mungu akifanikiwa maswali yanakuwa mengi sana, hivyo wakati mwingine huwa najiuliza watu wanomuomba MUNGU iliwafanikiwe wakijua MUNGU atawasaidia au Wanajaribu tu liwalo naliwe nahata wakisaidiwa hawajui kuwa wamesaidiwa?.KwaniniMtu akumshukuru MUNGU kwa mafanikio watu wanoana shida? au ni imani kuwa MUNGU hawezi kumpa mtu Utajiri/mali na hivyo shetani ndiyo mwenye uweza wa kufanya hivyo.

Nimefuatlila mijadala mingi hata mtu akimwombea mtu akapona wazo la kwanza ni shetani kafanya, kanisa likiwa na waumini wengi mawazo ni kuwa nguvu zimetoka zinazo wavuta ni za kichawi, hivi ni mawazo sahihi au akiri za watu zimetekwa sana na mambo ya giza sisiamini nguvu ya MUNGU?. Au ndiyo silaha ya Uovu kuwatia watu giza wasiamini uweza Mtakatifu?.

Haya ni mawazo yangu naomba nifikiri na wewe, Kama kweli Unamwamini MUNGU, na kweli unaamini anauweza kufumfanya mtu aishi maisha bora kama yalivyo makusidi yake;je si kweli watumishi wake wangeishi maisha bora zaidi kuliko mtu yeyote kwa sababu wanfanya kazi yake?, mbona tumeona wanomtumikia shetani /freemason wanishi maisha bora na angali tuanamini MUNGU ana nguvu zaidi. sasa nini shida watumishi wa MUNGU wakimiliki mali inakuwa taabu wakati MUNGU wao ndiye mwenye Fedha na dhahabu.

Naamini tunakosea mahali furani juu ya imani zetu, penginepo hatujui tuna mwamini mungu yupi(kwa wale wenye kuamini MUNGU) na pia hatujui uweza wake na mawazo yake juu ya watu wake, na ndiyo maana tumekuwa watu wakubebwa na yale tuno yasikia na kuyaona kila siku kutoka upande wa shetani.Mfano; tunafahamu kuwa watu wengi wanafanya kazi, biashara au kutoa huduma mbalimbali huku wakiwa wamekwenda kwa mafundi, waganga, wachawi na wengine hatakutoa kafara za damu za watu na wanyama na jambo hili limeene sana masikioni mwa watu hata kiasi kwambau ukiongea habari za mafanikio na MUNGU wanona ni jambo la uongo.

Ombi langu ni MUNGU ajionyeshe zaidi ili watu watambue uwepo wake na Waliofanikiwa wakiwa na uhakika kuwa ni MUNGU JEHOVA amefanya wajitangaze zaidi ili kushawishi watu, kwani shetani na watu wake wanajitangaza zaidi na kuufunika ulimwengu. Sisi sote tunahitaji kumili vitu vizuri hivyo ni rahisi kushawishika upande wowote ili upate, MUNGU awasidie wamwaminio kuangukia upande wake.

Ni kweli kabisa mkuu...
Going back to history katika jamii yetu hamna uzoefu wa nguvu ya Mungu aliye hai tumezoea dini tulizo hubiriwa na wakoloni ambazo hazikuonesha ufunuo ambao leo unadhihirishwa na Mungu mwenyewe katika kristo Yesu. Mababu zetu waliabudu miungu mingine maisha yao yote. Hata walipo letewa injili ya dini ilichukua muda kuelewa lakini bado haikuwa full gospel , ilikuwa partial haikuweza kuwafanya watanzania wawe independent. Full gospel ni ile injili ya asili aliyohubiri Yesu Kristo na mitume wake ambayo ina ishara, miujiza, kukemea pepo na nguvu za giza, unabii and may more(reveals the power of God).

Hakuna familia (kama zipo ni chache sana) ambayo wamekua wakiona baba/mama au kaka akikemea pepo/jini na likaondoka au kumponya mgonjwa kwa kuwekelea mikono na akapona. wengi hawajakuwa katika imani hiyo. Hata serikali za vijiji nakumbuka enzi hizo kijijini kwetu alisha wahi kuletwa mganga atoe wachawi mtaa kwa mtaa. Hii inaonesha ni jinsi gani ilivyo rahis sana watu kuamini uchawi/shetani kuliko Mungu aliye hai, ingawa anaona kabisha majini na mapepo (agents of the devil) yanavyo surrender litajwapo jina la Yesu Kristo wa Nazareth.

Ni tatizo la kihistoria na hivyo, watanzania tubadilike na tuwe na shukrani hata kwa hao wakoloni maana; naamini dini walizoleta zimetupa idea kwamba yupo Mungu aliyeumba haya tuyaonayo na yale tusioona, then tuchukue hatua kumtafuta yule Mungu aliye hai, anayeongea na aliye halisi tusiongee sana, maana yupo anatusubiri tumrudie tule mema ya nchi..."mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi". Maana imeandikwa uzima na mauti vi katika ulimi wa mwanadamu. Usihukumu watu/viongozi wa imani Maana imeandikwa judge not, for it is by the same measure you shall also be judged.

Jamani God is real, Jesus is real, Holy Ghost(spirit) is real and heaven is real. The devil i a Liar, Tanzania wake up pray for the nation and stop being lazy.
 
Neema za Mungu...
Hii inafaa kwenye zile picha za mashindano ya nyumba za Dar es Salaam na Nairobi...
 
Back
Top Bottom