Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 733
Huyu kaka ambae jina lake nalihifadhi, ni mkazi wa Mwananyamala kwa mama Zakaria inasemekana amekuwa mchonganishi kwa kutoa maneno huku na kuyapeleka kule mpaka kufikia watu kupigana ile mbaya.Sasa leo mchana wahusika wasichana kwa waavulana ambao wamedai kuchoshwa na tabia yake hiyo wamemkamata wamempiga na kumuamuru kuvaa kanga,wakamwamuru apike, afue, afagie, aoshe vyombo n.k
hapo kapewa kanga kaambiwa ajifunge...ili akafanye kazi za kike
ukimtazama kwa karibu utaona uvimbe,hapo ni baada ya kupigwa maskini yaani mpaka nilimuonea huruma........
amepakwa lipstik na eye shedow akaambiwa aweke pozi
kuna mdada hapa alikuwa anamwambia akae vizuri anyooshee vidole ampake rangi.........
mwanakaka alikuwa naamrishwa kufanya kila jambo kutoka kwa wabaya wake,hapo anaambiwa aweke pozi anyanyue kidole ka maringo...mmmh watu wabaya..