Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Hili ndiyo Bweni la wanafunzi wavulana wa shule ya Sekondari Zingibar ambalo Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza alitembelea ghafla na kutoa machozi baada ya kukuta mazingira yake mabovu, bweni hilo wanaishi jumla ya wanafunzi 25.
Na Dege Masoli ,Mkinga .
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza, mwishoni mwa wiki iliyopita alilazimika kutoa machozi mbele ya kadamnasi baada ya kufanya ziara katika shule ya Sekondari ya Zingibari iliyopo Wilayani hapa. Naibu Waziri huyo alifanya ziara ya kushtukiza ya kukagua shule hiyo ambapo alikuta wanafunzi wakiishi katika hali mbaya ikiwemo uchakavu wa mabweni. Alikuta wanafunzi wa kidato cha nne wa shule hiyo wakiishi katika nyumba chakavu ya makuti ambayo.
Maoni:
Kwa wanafunzi hawa ukiwauliza ni kitu gani wanakihitaji sasa hivi ili elimu yao iwe katika mazingira mazuri, vitambulisho vya smart card au makazi yenye hadhi na heshima ya mwanadamu. Bila ya shaka watataka makazi ili wawe salama.
Ukiliuliza swali hilo hilo kwa serikali watasema "wanahitaji vitambulisho hivi vya kisasa ili tuweze kujua wako wangapi, afya zao, na ili tuweze kuweka mkakati wa kuwapatia jengo zuri linaloendana na mahitaji yao.".