Scolari Ndenga
JF-Expert Member
- Aug 4, 2008
- 271
- 43
Kweli Bavicha mnatupa matumaini vijana wenzenu. Hongereni kamanda Munishi (Katibu mkuu) na Heche (Mwenyekiti)
Naamini hamtatuangusha Vijana tulio nyuma yenu. Ila itakua vema tukajua sumu mliyomwaga huko Morogoro.
Jamaa walikwenda kufungua matawi ya vijana na taarifa iliyopatikana ni kwamba wamefungua matawi manne yenye wanachama 187, wamefungua ofisi ya kata, wamehutubia mkutano wa hadhara na wamechangisha pesa taslimu kwa ajili ya shughuli za chama huko Morogoro.
Munishi aliwashambulia vijana wa Morogoro kwa kukubali kusababisha hali ngumu ya maisha kwa vijana wengine Tanzania kwa kukubali kuikumbatia CCM na kuifanya kama dini yao. Pia aliwaambia ugumu wa maisha unaowakabili ni makosa yao wenyewe na hivyo ni kujiunga na CDM ili kuunganisha nguvu zao na vijana wengine Tanzania kuiondoa CCM iliyokosa dira, mipango, na mikakati thabiti ya kuliongoza taifa. Aliendelea kuishambulia CCM kuwa imeoza kiasi kwamba hata malaika ashuke kutoka mbinguni kuiongoza Tanzania kupitia chama hicho ni lazima atafail tuu. Aliwataka kutambua kuwa hatma ya taifa hili liko mikononi mwa vijana. Wakizembea tu watakua wanawanyanyasa wazazi wao, wadogo zao, watoto wao na hata wajukuu wao na laana itakua juu yao.
Kamanda heche alitetemesha Morogoro kwa kuwataka vijana kuiunga mkono CDM kudai katiba mpya ya ukweli na sio ya kihuni huni. Katiba ambayo itapunguza mamlaka ya raisi, katiba itakayoweka ardhi mikononi mwa wananchi, katiba itakayoilazimisha serikali kuwapatia wananchi huduma za kijamii kama elimu na afya ili ikishindwa watu waweze kuishtaki. Katiba itakayoweka mamlaka ya nchi mikononi mwa umma tofauti na ya sasa iliyokaa kinafki nafki hivi.
Aligusia swala la mgomo wa madaktari na kuitaka serikali kuweka wazi madhara yaliopatikana kutokana na uzembe wake wa kutokushulikia madai ya madaktari.
Haya ndio niliyorushiwa na kamanda mmoja ambaye ni mwandishi wa habari huko Moro wazeiya!