Philemon Luhanjo: Ni nini kazi yake? Mbona hastaafu?

Nadhani bado haijampendeza rais si unajua tena mambo ya siku hizi sio sheria ni kwa kiasi gani rais amependa iwe hivyo. Masikini nchi yangu
 
Justified how,naomba udadavuzi mkuu.Samahani lakini.Maana tumeshazoea kusikia mtu amefikisha umri wa kustaafu kwa lazima lakini utasikia amekuwa akifanya kazi kwa mkataba au alikuwa kwenye mkataba miaka 2 au 3 n.k wakati vijana na watu wa rika la kati wapo.

Ni kwa maana mbili: Moja, umri wa kustaafu utumishi wa umma ni miaka 60, na huyu bwana mkubwa alishavuka umri huo sio mwaka huu wala mwaka jana, na alikuwa kwenye mkataba ambao hata umma ulikuwa unatambua kwamba mwisho ni tarehe 9 Dec 2011;

Mbili, kutokana na jinsi mambo yalivyojiri bungeni wakati kamati teule inawasilisha ripoti yake, huyu bwana mkubwa ilitakiwa atumie busara na angalau kuonyesha kwamba anali heshimu bunge, hivyo kuondoka kazini mapema iwezekanavyo, especially baada ya tarehe yake rasmi kustaafu kuwa ni tarehe 9 Dec;

Ni sababu hizi mbili ndizo zilipelekea nije na comment kwamba swali la mtoa hoja halina chembe ya majungu yoyote, ni swali ambalo lipo justified kwa maana kwamba - lipo reasonable, with adequate grounding;
 
Mizee kama hii ndio inazidi kutuweka kwenye umasikini na uchu wao wa madaraka.
 
Wakati wa sakata la Jairo tuliambiwa kuwa Luhanjo angestaafu tarehe 09/ 12/ 11 baada ya kufanikisha sherehe za miaka 50 ya uhuru. Juzi juzi nimemsikia akitaja majina ya mabalozi wapya walioteuliwa kuchukua kazi kwenye nchi mbalimbali. Leo hii bado siku 6 tumalize mwaka. Je huyu Luhanjo ajira yake haina kikomo?
inaonekana ni kisiki cha mpingo.
 
Mhamishia vyeo bado anacheki ni mshikaji wake gani atafiti pale.Maana masela wake kibao ssa hv wamemzunguka,jamani ni kazi ngumu kuwamwaga masela wako wa karibu!
 
Mhamishia vyeo bado anacheki ni mshikaji wake gani atafiti pale.Maana masela wake kibao ssa hv wamemzunguka,jamani ni kazi ngumu kuwamwaga masela wako wa karibu!
 
Na unafikiri hao ma-novice wake wana sifa ya kuwa Chief Secretary? Wathibitishe uwezo Sao ndipo wafikiriwe kwa nafasi za juu.
 
Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) hustaafu kama viongozi wengine, mfano makatibu na manaibu katibu wakuu wa Wizara. KMK hayuko katika kundi la viongozi wa kisiasa ambao hawana suala la kustaafu kama Mawaziri, Wakuu wa Mikoa nk.

Kweli muda wake wa kustaafu ulifika, lakini akaongezewa muda. Hilo la kuongezewa muda liko Serikalini kama wanaona kuna umuhimu wa kufanya hivyo.

Ahsante kwa ufafanuzi!
 
Ni kweli sheria inaruhusu mtumishi kuongezewa mkataba mara baada ya muda wa lazima wa kustaafu kufikia. Hivyo siyo ajabu kwa Luhanjo kuongezewa muda wa utumishi. Hata hivyo utaratibu huu hauwatendei haki vijana walioko katika utumishi kwani unawanyima fursa ya kupanda vyeo. Halikadhalika kwa upande wa ajira mpya, wastaafu wanakuwa bado wameziba nafasi hivyo vijana wanaomaliza masomo hawawezi kuajiriwa. Vijana pingeni utaratibu huu siyo kwa Luhanjo pekee, bali kwa wote walioongezewa muda wa ajira baada ya kustaafu serekalini na mashirika ya uma. Akina Luhanjo ni wengi sana kwa mamia serikalini na mashirika ya uma.
 
Si hayo tu huyo jamaa alistaafu na ni kweli yupo kwa ajilia JK na akimaliza kipindi chake ndio wastaafu wote. Sina hakika sana km ni kikatiba ila nadhani maslahi binafsi.
 
huyu mzee kashapiga sana hela toka wizara ya maliasili , alivyokwenda mambo ya nje hata safari alikuwa ataki ...si intersts yake kubaki ..manake yeye ndo anachafuliwa ..ni interests za mkuu wa nchii ...jamaa amemlindia sana mauchafu yake ...alafu pamoja na ufisadi twende mbele turudi nyuma jamaa anapiga kazi ila hii hai justify kuongezewa muda kila wakati ...mbaya zaidi ni kwamba alishastaafu toka miaka 3 nyuma ...miaka yote hii yupo kwenye mikataba ...bongo tambarare ...
 
Kwa JK, Luhanjo ni Jembe kama Nape alivyo kwa CCM! So ni vigumu sana akampoteza hivi wakati fursa ya ku-construct mikataba ipo wazi!
 
He played a big role na kampeni za mtandao kushika power, however Rais ana uwezo kikatiba kum-keep kwenye kazi yoyote anayemtaka na kama unamjua vizuri JK huwa hapendi kabisa watu kubaki muda ukifika. Meaning anamuhitaji sana cause nimewahi kuona JK akimstaafisha ndugu yake wa damu.
 
Back
Top Bottom