Peter Kisumo Vs. Anne Killango - vita vya maneno

HIVI yeye ni nani hasa! unajua tembo akisifiwa!! huyu fisadi kisumo kasifiwa sana eti mdhamini wa CCM etc,

Hivi bado ana ambitions zozote za kisiasa au lengo lake ni kutetea tu

Hapana unajua toka Mramba atoswe, sasa amekuwa nje ya the loop kwa hayo anajaribu kurudi tena kwenye system ya mtandao, kama Mkapa mzee hunywa sana kinywaji, na kule Upare aligombana sana na Msuyakwa hii misimamo yake, na unajua huko Pare kugombana na Musya na wananchi wakajua wa huko, ujue you are on your own maana Msuya hachezewi huko, kwa kisaikolojia ametengwa na wananchi, his only hope ni mtandao kuwepo kwenye power,

Ni mmoja wa viongozi wachache wa zamani ambaye bado yupo, baadhi ya viongozi wa CCM, na hasa mtandao, waligundua siku nyingi dhana moja ya kujidai kuheshimu viongozi wa zamani kwa kuwatanua kisifa, na baadaye kuwatumia against new politicians ili kuwatisha wanapotaka kupitisha agenda zao, nsio maana mpaka leo Kingunge bado yupo bungeni,

Mtandao walioamua kumtumia huyu mzee, walimtanua kwanza kwenye magazeti yao kisiasa, ndipo ile siku muungwana natangaza kuchukua fomu ya urais wakamleta huyu mzee kama ndiye mdhamini mkuu, wakampa mgwao wake, na akadai Marmba lazima awe waziri, wakampa kwa shingo upande, sasa wamemtema na mzee anajua kuwa mtandao wamemsahau maana na wao wana too many troubles, na pia kumbuka siku moja nilisema kuwa Rostam akisema majina ya viongozi aliwahi kuwapa hela kama mtikila, huyu mzee atakuwa wa kwanza kwenye list!

Hizi ni kelele za kuwakumbusha mtandao kuwa jamani nipo mbona mnaanza kunisahau!
 
Msisahau kuwa Kisumo ana mkono wenye afya njema kwa mkoa wa Pwani, I think ndie muasisi wa mkoa huo na ndie aliyeileta TAMCO kibaha akitumia ukaribu wake na Mwal Nyerere by then, If u remember kuna siku nilimzungumzia sana Warioba na tifu la Nyerere-UDSM against Mzee Luka Mkoka na ugaidi pale NDC. Mzee Kisumo ni mmoja wa washauri wabovu ambao NDC hawatamsahau hususani ktk issue ya TAMCO-Kibaha.

Simpingi wala kumkubali juu ya yale aloyasema kuhusu Madame Malecela ila ninamshauri tu mzee, ajitizame kwenye kioo na ajiulize kama anafanana na siasa za sasa za Tz au la.
 
Muda mfupi uliopita ametoa statement ya kukanusha mambo yote yaliyoandikwa gazetini kumhusu yeye kumkandia Kilango na mareale. Anasema anazungumza na wakili wake juu ya hatua za kumchukulia mwandishi aliyeandika kwa sababu yeye hajawahi kufanya naye mahojiano kuhusiana na jambo lolote
 
Muda mfupi uliopita ametoa statement ya kukanusha mambo yote yaliyoandikwa gazetini kumhusu yeye kumkandia Kilango na mareale. Anasema anazungumza na wakili wake juu ya hatua za kumchukulia mwandishi aliyeandika kwa sababu yeye hajawahi kufanya naye mahojiano kuhusiana na jambo lolote


Du makuubwa haya!!!!!
 
Kilango amjibu Kisumo

na Martin Malera
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MBUNGE wa Same Mashariki, Anne Kilango (CCM), ameeleza kusikitishwa na matamshi yaliyotolewa dhidi yake na mwanasiasa wa siku nyingi, Peter Kisumo.

Kilango, mmoja wa wabunge walio mstari wa mbele kukemea vitendo vya ufisadi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali wakiwa bungeni na nje, alisema tuhuma zilizotolewa na Kisumo dhidi yake ni za kutumwa.

Mbunge huyo ambaye ni mke wa Makamu Mwenyekiti mstaafu wa CCM, John Malecela, alitoa matamshi hayo jana wakati alipofanya mahojiano ya simu na Tanzania Daima.

Kilango ambaye alifikia hatua ya kusema kwamba alikuwa akiwafahamu waliomtuma Kisumo hata kutoa matamshi hayo, alisema ataendelea kusimama kidete kupambana na mambo ambayo yanakitia doa chama chake na serikali.

Pasipo kuwataja kwa majina wale anaoamini kuwa wamemtuma Kisumo, mbunge huyo alisema alikuwa bado haamini sawasawa iwapo kauli dhidi yake zimetolewa na mwanasiasa wa kariba ya Kisumo, aliyejijengea heshima ndani ya chama na serikali kwa miaka mingi iliyopita.

“Hivi kweli maneno hayo ni ya Kisumo ninayemfahamu mimi! Kisumo yupi? Kisumo ninayemjua mimi ni yule mwanachama mkongwe wa CCM, anayepaswa kuilinda CCM na serikali ili isidhalilishwe na mafisadi.

“Kisumo ninayemfahamu mimi ni kiongozi wa siku nyingi, ambaye amewahi kuwa mbunge, waziri na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, anapaswa kujielekeza kwenye majukumu ya chama,” alisema Kilango kwa kujiamini na kwa sauti kali.

Akifafanua kuhusu kutumwa kwa Kisumo, mbunge huyo machachari, alisema maneno aliyotumia mwanasiasa huyo dhidi yake yanatokana na mazungumzo ya ndani kati ya wabunge wa CCM na Katibu Mkuu wa chama chao, Yussuf Makamba.

“Kisumo si mbunge. Haya maneno ya kikao cha ndani cha wabunge wa CCM na Makamba cha sisi kuzuiliwa kuikosoa serikali kayatoa wapi?” alihoji Kilango.

Pamoja na hilo, Kilango alieleza kushangazwa na maneno aliyotoa Kisumo akidai kwamba yeye (Kilango) alikuwa hana sifa ya kuwa hata naibu waziri katika serikali.

“Kisumo anasema eti mimi sina hata sifa ya kuwa naibu waziri. Amepata wapi sifa za watu wanaotakiwa kuwa mawaziri au naibu mawaziri?” alihoji Kilango.

Alisema Kisumo anapaswa kujua kuwa, yeye (Kilango) ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) na analifahamu Azimio la Butiama na madhara ya kutokemea maovu yanayotendwa na baadhi ya viongozi wa serikali ya CCM.

Alisema Kisumo, mtu aliyepata kushika nyadhifa za juu za ukuu wa mkoa na uwaziri zama za Serikali ya Awamu ya Kwanza, anapaswa kujua kuwa yeye (Kilango), alichaguliwa kwa kura kuingia bungeni na akala kiapo cha kukijenga chama, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha ufisadi unaangamizwa nchini.

Kutokana na kulitambua hilo, alisema ataendeleza msimamo wake wa kuikosoa CCM, na kwamba yuko tayari kwa lolote wakati anapokabiliana na kukemea vitendo vya kifisadi.

“Nataka Kisumo ajue, nitasimamia ninachokiamini, nitaendelea kukemea kwa nguvu zangu zote viongozi na watendaji waovu, kwa sababu wanakidhalilisha chama na serikali, na mawazo ya Kisumo wala hayanishughulishi,” alisema Kilango.

Mbali ya hayo, Kilango alieleza kusikitishwa pia na tuhuma za Kisumo dhidi ya mwana CCM mwingine, Aggrey Marealle, za kuhoji sababu za kutoa misaada Moshi Mjini hata kufikia hatua ya kusema hana sifa za kuwa mbunge wa jimbo hilo.

Katika hili, Kilango alisema matamshi hayo ya Kisumo yamemfanya agundue sababu za CCM kushindwa katika jimbo hilo la uchaguzi kila wakati.

Alisema anaamini kwamba, moja ya sababu za chama hicho tawala kulipoteza jimbo hilo kwa wapinzani ni kuwapo kwa wanachama wenye mawazo kama ya Kisumo. Kwa vipindi viwili mfululizo jimbo hilo linaongozwa na Mbunge wa CHADEMA, Philemon Ndesamburo.

“Sizungumzii nani anapaswa kuwa mbunge Moshi Mjini, lakini Kisumo hawezi kutoa kauli ya kuonyesha nani anafaa au nani hafai kuwa mgombea, hii maana yake, yupo mtu anayemtaka yeye na hilo si jambo zuri,” alisema Kilango.

Kwa upande wake, Marealle, alikataa kuzungumzia kwa undani kauli ya Kisumo kumponda, akisema asingependa kutoa kauli yake pamoja na kusisitiza kuwa, alikuwa anayo haki ya kutoa msaada wowote kwa chama chake pale anapoona inafaa.

Mjadala huu umeibuka siku moja tu, baada ya Kisumo kuzungumza na waandishi wa habari akimshutumu Kilango kwa msimamo wake wa kuikosoa CCM na serikali kila wakati.

Kisumo katika mazungumzo yake hayo ya juzi, alisema Kilango amejivisha jukumu la wapinzani kwa kuishutumu serikali juu ya tuhuma za ufisadi, wakati yeye mwenyewe akiwa mwanachama na mbunge anayetokana na chama hicho.

Kauli hiyo ya Kisumo kwa wadadisi wa mambo inaweza kukumbusha msimamo wa mwanasiasa huyo mkongwe aliyejitokeza hadharani kumpigia Rais Jakaya Kikwete debe wakati akitangaza azima yake ya kugombea urais mwaka 2005, kwa kuwataka wazee wenzake kuwaachia vijana kulitumikia taifa.

Kauli hiyo ya Kisumo dhidi ya wazee kwa kiwango kikubwa ilionekana kumlenga zaidi Malecela, ambaye ni mume wa Kilango, aliyekuwa akipewa nafasi kubwa ya kutoa upinzani mkali kwa wagombea wengine wa urais, akiwamo Kikwete.
 
Huyo Kisumo hopeless, sasa anataka ku spin mambo!

Pasipo kuwataja kwa majina wale anaoamini kuwa wamemtuma Kisumo, mbunge huyo alisema alikuwa bado haamini sawasawa iwapo kauli dhidi yake zimetolewa na mwanasiasa wa kariba ya Kisumo, aliyejijengea heshima ndani ya chama na serikali kwa miaka mingi iliyopita.

"Hivi kweli maneno hayo ni ya Kisumo ninayemfahamu mimi! Kisumo yupi? Kisumo ninayemjua mimi ni yule mwanachama mkongwe wa CCM, anayepaswa kuilinda CCM na serikali ili isidhalilishwe na mafisadi.

"Kisumo ninayemfahamu mimi ni kiongozi wa siku nyingi, ambaye amewahi kuwa mbunge, waziri na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, anapaswa kujielekeza kwenye majukumu ya chama," alisema Kilango kwa kujiamini na kwa sauti kali.

Huyu Mama anachemka kama kawaida yake, kwanza anasema anawajua waliomtuma Kisumo na hawezi kutetereka, halafu anasema haamini kama Kisumo kasema maneno hayo.

Sasa lipi ni lipi? Hivi lini viongozi wetu watajifunza kuwa na breki za mdomo?

Kama huamini kwamba Kisumo kasema maneno hayo utaendaje kumu attack na kusema unajua waliomtuma?

Kama una confidence ya kusema unajua waliomtuma itakuwaje useme huamini kama Kisumo kasema maneno haya?

Hii inaonyesha low IQ, kukosa mantiki, kupenda misifa na kupenda kubwabwaja tu.
 
Hawa ndio wanaotumiwa kuikaba koo serikali ya Muungwana ,tabu yake wanatumika bila mipango,Pinda kasema Zanzibar si nchi,waziri mwengine kasema kuweka mwimbo wa Taifa kuwa ni ring tone ni kosa la jinai ,wanavuluga wakibanwa eti wanakitupia Chama wakati anaetamka ni mtu wa serikali maana hata Chama kinaweza kuruka.
 
Kazi ipo hapo maana Mama kilango anasema anajua Kisumo ametumwa na nani....nini maana yake?maana ukiangalia kwa undani..Kisumo huyu huyu ndie aliekuwa mzee wa kwanza kumuunga mkono mgombea nafasi ya kuwania uraisi katika chama ,JK...hadi akaulizwa "Mzee Huogopi"?hayo ni maneno ya JK mwenyewe kwa Mzee huyu....kwa hiyo ukiangalia kwa undani utajua kuwa hapo kuna kitu kikubwa sana ama cha kutumwa ama cha kujiingiza kwenye mtandao kwa nguvu(kama bado hajaingia tangu wakati ule).....kazi ipooo....inaitwa double dutch
 
Huyo Kisumo hopeless, sasa anataka ku spin mambo!



Huyu Mama anachemka kama kawaida yake, kwanza anasema anawajua waliomtuma Kisumo na hawezi kutetereka, halafu anasema haamini kama Kisumo kasema maneno hayo..

Sidhani kama mama anachemka. Hii ni njia ya kistaarabu ya kumwambia bwana Kisumo kuwa hakupaswa kutamaka maneno kama yale...
Kwa vyovyote wote wawili wanajua kwanini wanapeana maneno hayo..siye tunachoweza kufanya ni kusikiliza na ku harzard a guess kama wengi wanavyofanya sasa ...all in all wana haki ya kuzungumza ili kuondoa yaliyo mioyoni mwao.
 
Sidhani kama mama anachemka. Hii ni njia ya kistaarabu ya kumwambia bwana Kisumo kuwa hakupaswa kutamaka maneno kama yale...
Kwa vyovyote wote wawili wanajua kwanini wanapeana maneno hayo..siye tunachoweza kufanya ni kusikiliza na ku harzard a guess kama wengi wanavyofanya sasa ...all in all wana haki ya kuzungumza ili kuondoa yaliyo mioyoni mwao.

There is a need for unambiguous, categorical statements.Haya mambo ya nilisema hivi lakini nilimaanisha hivi ni usanii mwingi tu.

Kama unataka kumkoma nyani mkome tu, usianze kumpamba eti huamini kasema hivyo and this and that...
 
mmemsahau huyu mzee? si yule aliyeungana na wazee wachovu kama yeye akina siyovelwa_RIP, eti wakafungua kesi kuitaka mahakama iifute cuf. wanaonichefua zaidi ni hawa waandishi wa habari wanomfuata kumtaka atoe hoja, hali inajulikana wazi alishadata muda mrefu
 
...huyu Mzee Ni Mjinga...nimeshasema Mara Nyingi Hapa....nimebahatika Kukaa Naye Na Kumsikiliza Hasa Wakati Ule Wa Uteuzi...maneno Mabaya Aliyokuwa Akiongea Dhidi Ya Salim Na Malecela Hayaandikiki......

Lakini Si Kosa Lake....ni Mjinga Tangu Zamani Miaka Ya Mwisho Ya 50 Alipokuwa House Boy Na Kuli Wa Wahindi Pale Arusha....na Funza Miguuni...daima Mdomo Wake Mchafu Umemlisha..hassa Alipoweza Kuchaguliwa Kuwa Kiongozi Wa Wafanyakazi Wa Ndani..kwenye Chama Cha Wafanyakazi Enzi Zile Na Ikawa Njia Yake Kuingia Siasa....
Eeeeeeeee shshshssh kumbe alikuwa house boy? ama kweli alidhani kwa sababu ni mzee watu hawamuelewi vizuri? na adharauliwe kwa umbumbu wake.
 
Huyu Mama anachemka kama kawaida yake, kwanza anasema anawajua waliomtuma Kisumo na hawezi kutetereka, halafu anasema haamini kama Kisumo kasema maneno hayo.

Sasa lipi ni lipi? Hivi lini viongozi wetu watajifunza kuwa na breki za mdomo?

Kama huamini kwamba Kisumo kasema maneno hayo utaendaje kumu attack na kusema unajua waliomtuma?

Kama una confidence ya kusema unajua waliomtuma itakuwaje useme huamini kama Kisumo kasema maneno haya?

Hii inaonyesha low IQ, kukosa mantiki, kupenda misifa na kupenda kubwabwaja tu.

Mama Kilango,

Amesema kuwa haamini kuwa Kisumo anayemjua kuwa anaweza within himself ku-create hayo maneno aliyomrushia, ni kwa sababu haaamini hivyo ndio maana amesema kuwa anawajua waliomtuma Kisumo, ili amrushie hayo maneno yasiyokuwa na heshima kwa kiongozi jasiri wa taifa kama yeye, Mama Kilango,

Kwa hiyo hapa ni clear kuwa kuna mtu mwenye Low IQ, sasa sielewi ni nani kati ya Kisumo aliyetumwa kusema asichokijua, au yoyote yule aliyeshindwa kuelewa maneno ya Mama Kilango,

Tuache kukurupuka na kuropoka maneno ya chooni bila ya kuwa na haja!
 
Mama Kilango,

Amesema kuwa haamini kuwa Kisumo anayemjua kuwa anaweza within himself ku-create hayo maneno aliyomrushia, ni kwa sababu haaamini hivyo ndio maana amesema kuwa anawajua waliomtuma Kisumo, ili amrushie hayo maneno yasiyokuwa na heshima kwa kiongozi jasiri wa taifa kama yeye, Mama Kilango,

Kwa hiyo hapa ni clear kuwa kuna mtu mwenye Low IQ, sasa sielewi ni nani kati ya Kisuma aliyetumwa kusema asichokijua, au yoyote yule aliyeshindwa kuelewa maneno ya Mama Kilango,

Tuache kukurupuka na kuropoka manenio ya chooni bila ya kuwa na haja!

In any other case, neno "apologist" lingetumikwa na my good friend FMES.

Hapa Mama Kilango anakuwa "Kisumo apologist" simple and clear.
 
Nakubaliana na Pundit kuwa Straight forward politics ndio zinazo make sense...Or at least tunazihitaji wakati huu.
Na kwa hiyo hakuna maana ya vijembe tena kwasababu wananchi wetu hawana uelewa wa maneno ya kutaka watumie IQ..Kwanza IQ ipi na NJAA ZOTE NA MAGONJWA? Tusije kujisahahu halafu wananchi wa kawaida ambao ni wasomaji wakaona tunzungumza siri na wao hawaelewi so wakdhani sisi ni majasusi...Wajamaica wanakwambia ama pienetrait strait.
 
In any other case, neno "apologist" lingetumikwa na my good friend FMES.
Hapa Mama Kilango anakuwa "Kisumo apologist" simple and clear.

Mkuu Heshima Mbele,

Mama Kilango, ana washauri wazuri sana wanaomlinda kisiasa, yeye ni mbunge mwanamke wa Same East, ambako mwanamke bado ni mwanamke na hizi za kisumo ni siasa za jimbo la Ubunge, sio za taifa kama unavyofikiri,

Siasa za Tanzania sio sawa na za huko majuu, at the end of the day bado Kisumo ni mwanaume anyetakliwa kuheshimiwa huko upareni, pamoja na mapungufu yake, jimbo la ubunge sio sawa na The Truth Commision,

Ndio maana Mama Anna Abdallah, amemaliza political career yake, baada tu ya kumrushia maneno Mama Kilango, Kisumo sio active politician hana anything to lose, Mama kilango, has a lot to lose than to gain kwa kurushiana maneno na a loser kama Kisumo, ambaye sasa hivi anaisha na pombe.

Ahsante Mkuu!
 
nikumwacha tu hajui alitendalo,inaonyesha issue zake zinayumba akibwabwaja hata kama ni ujinga wakuu watampa mshiko hata kama ni vijisenti.uhuru wa Mtanzania bado,hakuna uzalendo,waheshimiwa wanajali issue zao na familia zao,sijui kitaelweka lini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom