Watu wanatofautiana kitabia, kuna watu ambao ni waaminifu kwa wenza wao na kuna ambao ambao sio waaminifu na kwa maana hiyo hata kama mtu amevaa pete ya ndoa bado tabia yake inabaki pale pale. Aidha kuna wale wanaovaa pete ya ndoa kama fashion; kwa maana hiyo mtu kuwa na kutokuwa na pete ya ndoa sio uthibitisho kuwa kaolewa au kaoa, kuna wale ambao wameoa lakini imani zao haziwaruhus kuvaa pete na bado wana tabia za kutoka nje kwa hiyo unaweza kutana na mtu ambaye hana pete ukadhani ni jimbo huru kambe lina mwenyewe au amevaa pete kubwaaaaaaaa anavunja "amri ile" ukamwingiza kwenye kundi la wenye ndoa kumbe ni hana ndoa.