platozoom
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 9,366
- 11,154
Nazungumzia kuingia kwenye penzi kwa mara ya kwanza halafu ukapenda kikwelikweli.
Ilinitokea tena nikiwa na miaka 18..nilimpenda sana huyu binti, sidhani kama kuna saa ilipita bila kumuwaza .kibaya zaidi mawazo kumhusu yeye yalikuwa negative tu: Hivi sasa hivi yuko wapi? Kuna mtu yuko naye nini? mbona simuoni kama ilivyo kawaida.
Kiukweli hata yeye alinipenda sana .na kuna wakati aliniambia naye huwaza hivyohivyo. Nakumbuka nilivyokuwa nakwenda nyumbani kwao mida ya usiku kumuiba tena kwa ujasiri mkubwa nikishiriana na rafiki yangu.
Inakuwa hivi: Mida ya mchana tunapanga mchezo mzima Usiku mida ya saa 4 nazuka kwao nyuma ya nyumba..na kumtuma kijana mmoja mdogomdogo hivi (Sasa hivi kakua..humtumi tena).. halafu yeye anaingia kwao na binti na kumpiga konye.
Binti anajiandaa kabisa akisubiri Wazazi na ndugu walale (Yeye alikuwa analala chumba kimoja na dada yake ambaye tulikuwa tunashibana). Halafu mida ya saa tano anatoroka kupitia mlango wa uwani..Dada anaufunga!
Sijapata kupenda kama nilivyowahi kupenda wakati ule. Kuna siku nilimuona na jamaa mmoja hivi wakipiga story kwa muda mrefu sana .Nikajua nimeibiwa, wacha nimtandike na barua ndefu ya talaka huku moyo unadunda ..Nilivyompa nikabaki najilaumu Hivi akikubali tuachane kweli nitahimili?
Saa 8 saa 9 saa 10 hakuna dalili yeyote ya majibu ya kukubali kuvunja uhusianao au kuomba msamaha .Dah!! Si Roho wala mwili haukuwa wangu, Jasho linanitoka chakula hakipiti kila mtu anajua nimepata maradhi ya ghafla Sitasahau .Ilipofika saa 12 akamtuma mtu na barua ya kuomba msamaha ..Nilifurahi hakuna mfano
Unajua nilimjibu vipi ..USIRUDIE TENA SIPENDI TABIA HII, MPENZI HALAFU UJE TUONANE.
Aaah penzi la kwanza kwenye utineja lione hivyo hivyo!!!!!!!!!!
Nawasilisha nanyi nipeni uzoefu wenu.
Ilinitokea tena nikiwa na miaka 18..nilimpenda sana huyu binti, sidhani kama kuna saa ilipita bila kumuwaza .kibaya zaidi mawazo kumhusu yeye yalikuwa negative tu: Hivi sasa hivi yuko wapi? Kuna mtu yuko naye nini? mbona simuoni kama ilivyo kawaida.
Kiukweli hata yeye alinipenda sana .na kuna wakati aliniambia naye huwaza hivyohivyo. Nakumbuka nilivyokuwa nakwenda nyumbani kwao mida ya usiku kumuiba tena kwa ujasiri mkubwa nikishiriana na rafiki yangu.
Inakuwa hivi: Mida ya mchana tunapanga mchezo mzima Usiku mida ya saa 4 nazuka kwao nyuma ya nyumba..na kumtuma kijana mmoja mdogomdogo hivi (Sasa hivi kakua..humtumi tena).. halafu yeye anaingia kwao na binti na kumpiga konye.
Binti anajiandaa kabisa akisubiri Wazazi na ndugu walale (Yeye alikuwa analala chumba kimoja na dada yake ambaye tulikuwa tunashibana). Halafu mida ya saa tano anatoroka kupitia mlango wa uwani..Dada anaufunga!
Sijapata kupenda kama nilivyowahi kupenda wakati ule. Kuna siku nilimuona na jamaa mmoja hivi wakipiga story kwa muda mrefu sana .Nikajua nimeibiwa, wacha nimtandike na barua ndefu ya talaka huku moyo unadunda ..Nilivyompa nikabaki najilaumu Hivi akikubali tuachane kweli nitahimili?
Saa 8 saa 9 saa 10 hakuna dalili yeyote ya majibu ya kukubali kuvunja uhusianao au kuomba msamaha .Dah!! Si Roho wala mwili haukuwa wangu, Jasho linanitoka chakula hakipiti kila mtu anajua nimepata maradhi ya ghafla Sitasahau .Ilipofika saa 12 akamtuma mtu na barua ya kuomba msamaha ..Nilifurahi hakuna mfano
Unajua nilimjibu vipi ..USIRUDIE TENA SIPENDI TABIA HII, MPENZI HALAFU UJE TUONANE.
Aaah penzi la kwanza kwenye utineja lione hivyo hivyo!!!!!!!!!!
Nawasilisha nanyi nipeni uzoefu wenu.