~~Penzi la Kumegeana~~

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,988
Penzi la kumegeana, si penzi la kupeana,
Penzi la kutegeana, kwa kibaba kupeana,
Penzi la kutishiana, la nini la kugawana?
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!

Penzi la kumegeana, ni penzi la kuchokana
Penzi la kuringishana, hilo la kuchomoana,
Penzi la kutafutana, ni mwiba wa kuchomana,
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!

Penzi la kumegeana, ni penzi la kutesana,
Penzi la kuudhiana, ni penzi la kushindana,
Penzi la kunyimiana, mabaya kutafutana,
Penzi la kumegemeana, si penzi hilo hiana!

Penzi la kumegeana, la vipande kugawana,
Penzi la kutukanana, ni penzi la kuumizana,
Penzi la kukorogana, siyo penzi la mwanana,
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!

Penzi la kumegeana, la sirini kuitana,
Penzi la kukimbizana, la mwingine kugawana,
Penzi la kuchakuana, gizani kutafunana,
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!

Penzi la kumegeana, mwenzenu ninalikana,
Penzi la kuulizana, maswali ya kiaina,
Penzi la kuudhiana, na vidonda vikatona,
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!

Ukitaka kweli penzi, sitake la kumegeana!
Tafuta wako muenzi, mpende mkapendana,
Awe wako wa aziz, wa penzi lililoshibana,
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!


Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
 
Last edited by a moderator:
MKJJ,
i hope kwamba utakuwa na stock kubwa ya mashairi,why dn't you compile a book?u cn do it men,then yatatumika wizara ya elimu.

Kwasasa kuna uhaba mkubwa sana wa washairi,na baraza la mtihani linarudia rudia tu vitabu.

MAKE USE OF U R TALENT BWANA
 
MKJJ,
i hope kwamba utakuwa na stock kubwa ya mashairi,why dn't you compile a book?u cn do it men,then yatatumika wizara ya elimu.

Kwasasa kuna uhaba mkubwa sana wa washairi,na baraza la mtihani linarudia rudia tu vitabu.

MAKE USE OF U R TALENT BWANA


shukrani.. lakini hata vitabu si vitakuwa vya bure.? watu wafurahie tu siku moja mtu mwingine ataamua kuyakusanya.
 
shukrani.. lakini hata vitabu si vitakuwa vya bure.? watu wafurahie tu siku moja mtu mwingine ataamua kuyakusanya.

is that so?vitabu vya bure how?iwapo tu wakubwa wizarani wataarpove basi umeula!cha muhimu print vitabu vyako hata kopi kumi tu peleka wizarani pale,na hapa TUKI,wavifanyie assessments then we pray for the best wavikubali!

Hamna ishu ya bure bwana!
 
is that so?vitabu vya bure how?iwapo tu wakubwa wizarani wataarpove basi umeula!cha muhimu print vitabu vyako hata kopi kumi tu peleka wizarani pale,na hapa TUKI,wavifanyie assessments then we pray for the best wavikubali!

Hamna ishu ya bure bwana!

nashukuru kwa kunipa moyo; nataria kutoa vitabu vitatu kabla ya uchaguzi mkuu! Tatizo ndiyo hilo inabidi nigawe bure wabongo hawanunui.. na wakinunua basi wanaazimana utadhani maktaba!
 
Penzi la kumegeana, si penzi la kupeana,
Penzi la kutegeana, kwa kibaba kupeana,
Penzi la kutishiana, la nini la kugawana?
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!

Penzi la kumegeana, ni penzi la kuchokana
Penzi la kuringishana, hilo la kuchomoana,
Penzi la kutafutana, ni mwiba wa kuchomana,
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!

Penzi la kumegeana, ni penzi la kutesana,
Penzi la kuudhiana, ni penzi la kushindana,
Penzi la kunyimiana, mabaya kutafutana,
Penzi la kumegemeana, si penzi hilo hiana!

Penzi la kumegeana, la vipande kugawana,
Penzi la kutukanana, ni penzi la kuumizana,
Penzi la kukorogana, siyo penzi la mwanana,
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!

Penzi la kumegeana, la sirini kuitana,
Penzi la kukimbizana, la mwingine kugawana,
Penzi la kuchakuana, gizani kutafunana,
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!

Penzi la kumegeana, mwenzenu ninalikana,
Penzi la kuulizana, maswali ya kiaina,
Penzi la kuudhiana, na vidonda vikatona,
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!

Ukitaka kweli penzi, sitake la kumegeana!
Tafuta wako muenzi, mpende mkapendana,
Awe wako wa aziz, wa penzi lililoshibana,
Penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana!


Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)

Naaaaaaaaam! Manshallah
 
kila siku kupigana, ni aibu barazani,
hamuishi kutukanana, matusi mazito ya nguoni,
hakuna kuheshimiana, nyumba ikawa na amani,
penzi la kumegeana, ni baya sana jamani.

kalamu naweka chini, pumzi imekata kifuani,
wangu usia usikieni, wakike na wa kiumeni,
penzi la mafichoni, baya si kama hadharani,
penzi la kumegeana, ni baya sana jamani.
 
Hapana chako na changu, hivi vyote ni shirika
Mimi wako wewe wangu, kipi cha kugawanyika?
Kuungana walimwengu, ni neno lenye mwafaka,
Linapendeza kwa Mungu, pamoja na malaika

Kukwambia nenda zangu, sithubutu kutamka,
Na kadhalika mwenzangu, sidhani hilo wataka,
"Hutaki" lina uchungu, na kwangu ni kadhalika.
Dunia ina mizungu, nikwambiayo kumbuka.
 
Mliyonena ni kweli, kayafundisha Mwenyezi,
Tuache kuwa tapeli, kwa kumegeana penzi,
Tupeane kwelikweli, si mara moja kwa mwezi,
Penzi la kumegeana, alifai asilani.
 
Haya mzee..nimekupata vilivyo. Mimi namegewa penzi kwahiyo shairi lako limepiga kumoyo
 
hodi hodi jamvini, kwakasi kubwa leo nakuja,
nguvu nyingi mwilini, kama mabomu ya faluja,
ari nayo akilini, ndio inipayo na ujanja,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana

magonjwa ni mengi, ukimwi ni namba wani,
shule za msingi, umetapakaa hadi vyuoni,
vijana kwa madingi, mijini mpaka vijijini,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.

penzi la kumegeana, ni penzi la kifisadi,
mashaka tele kupeana, si kutongozana hata miadi,
penzi dhahiri kukosekana, ukibisha muulize mchukia_fisadi,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana

dada belinda sikia, kuna mjanja yo-yo usimmegee,
hata kwalolote akikwambia, usiruhusu akusogelee,
nyaningabu na mpitanjia, jihadhari usiwape wachekelee,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana

mama joe heshima kwako, nyingi sana kama kilo,
usigawe penzi lako, kwa bujibuji au masanilo,
siwasahau asilani mamaparoko, mzee mwanakijiji na lunanilo
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.

kuna mambo ya tigo, vijana siku hizi ndio mtindo,
ndugu yangu kigogo, haraka mjulishe hata invizibo,
kumegeana hata tigo, siku hizi ndio mtindo,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.

ingawa la kumegeana, wanasema tamu kama asali,
lakini mgoni akijulikana, kipigo lazima kulazwa hospitali,
manundu usoni yamelundikana, afya yake haina hali,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.

cha mtu ni mavi, wahenga walitwambia,
usimege kama kiwavi, utakuja jijutia,
upatwapo na kimavi, usiseme George_Porjie sijakwambia,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.


mwanajamiiOne anajua hatari kumegemeana, hata masanilo alitoswa,
wasingeweza kuelewana, mwanajamiiOne hapendi kunyanyaswa,
alijua wasingeshibana, mchakamchaka angepelekeshwa,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.
 
Last edited:
hodi hodi jamvini, kwakasi kubwa leo nakuja,
nguvu nyingi mwilini, kama mabomu ya faluja,
ari nayo akilini, ndio inipayo na ujanja,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana

magonjwa ni mengi, ukimwi ni namba wani,
shule za msingi, umetapakaa hadi vyuoni,
vijana kwa madingi, mijini mpaka vijijini,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.

penzi la kumegeana, ni penzi la kifisadi,
mashaka tele kupeana, si kutongozana hata miadi,
penzi dhahiri kukosekana, ukibisha muulize mchukia_fisadi,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana

dada belinda sikia, kuna mjanja yo-yo usimmegee,
hata kwalolote akikwambia, usiruhusu akusogelee,
nyaningabu na mpitanjia, jihadhari usiwape wachekelee,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana

mama joe heshima kwako, nyingi sana kama kilo,
usigawe penzi lako, kwa bujibuji au masanilo,
siwasahau asilani mamaparoko, mzee mwanakijiji na lunanilo
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.

kuna mambo ya tigo, vijana siku hizi ndio mtindo,
ndugu yangu kigogo, haraka mjulishe hata invizibo,
kumegeana hata tigo, siku hizi ndio mtindo,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.

ingawa la kumegeana, wanasema tamu kama asali,
lakini mgoni akijulikana, kipigo lazima kulazwa hospitali,
manundu usoni yamelundikana, afya yake haina hali,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.

cha mtu ni mavi, wahenga walitwambia,
usimege kama kiwavi, utakuja jijutia,
upatwapo na kimavi, usiseme George_Porjie sijakwambia,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.


mwanajamiiOne anajua hatari kumegemeana, hata masanilo alitoswa,
wasingeweza kuelewana, mwanajamiiOne hapendi kunyanyaswa,
alijua wasingeshibana, mchakamchaka angepelekeshwa,
penzi la kumegeana, si penzi hilo hiana.

Georgie ... mbona?
 
Ama kweli weye umeliona kwa mapana' wanopeana hilo penzi haweshi kuumana' ni penzi la utata hamweshi kulumbana' liwapo shubiri mashati kuchaniana' penzi lisilo upana liendalo kwa dhamana' ukosapo faranga nalo walichana' penzi hili lilo sugu kwa chuki kama gonjwa lisopona' nipe nikupe ndo sheriayo watafuna' mikopo na fadhila humu huwezi kwona' magomvi na madhila moyoni kujazana' mwanakijiji ndugu yangu nakuasa usijezama' dimbwi hili si salama'
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom