Penzi-kipato= mgogoro (?)

Akiwa mwanaume mwelewa atazidisha bidii kutafuta sources nyengine za pesa ... mwanaume hasa ... rijali kabisa hawezi kupokea hela ya mwanamke ..... mwanamke kumpa hela yake ya mshahara .. mhh! sidhani kama ni kuwa thabit ama kumpa uhalisi wake ... mwengine ni mharibifu ... na hela usioifanyia kazi waweza kuzitumia utakavyo maana hujui uchungu wake ... mimi nadhani mugawane majukumu halafu umsaidie tu pale ambapo anaupungufu ... heshima ibaki palepale

Mwanaume kuwa rijali 100% ni ngumu kama ilivyo mwanamke kuwa mtii 100%
tukubali kukosa kidogo kila upande.
manake hapa mimi napata picha ya mwanaume rijali kiafrika ni yule ambaye maamuzi yote ya nyumbani anafanya yeye. mimi kama mwanamke sitamuweza.

Kwa ajira za sasa, kupanda na kushuka kwa kipato si kitu cha muda mrefu sana.
sisi tumeshawahi kusimamia nyumba kwa zamu mara kibao, ila tofauti ni kuwa yeye akiwa nazo anatoa kiasi fulani anaweka mahali/account naweza kuchuka bila kuombaomba kila saa, na mimi pia hivyo hivyo, ila uwazi katika jumla kuu ni muhimu.
Pia kwamba balance uliobaki nayo ni kwaajili ya personal use tu.
inahitaji kujitoa zaidi na TOTAL TRUST IN EACH OTHER. Ambayo nadhani kwa muelekeo wa hapa ni ndogo.
tution ya bure kwa kina dada (ambao bado bado) ukiua self confidence ya mumeo utamchukia mara moja. Jitahidi aweze kutembea kifua mbele humu duniani, hasa kwa rafiki zake na ndugu.
 
Kwa maoni yangu, Hamna tofauti iwe ni mume au mke, mwenye kipate zidi ya mwenzake. Cha muhimu ni heshima katika ndoa. Kwani hata ikiwa ni Mume mwenye uwezo akamkosa heshima mkewe ndoa haitadumu.
Kutatua shida ya pesa za matumizi ya kibinafsi [Tukubali ukweli, its hard kuomba pesa kila unapotaka kununua chupi, ka konyagi ama kumnunulia aliyekupa zawadi nk.]. Basi wapenzi wakubaliane kiasi ambacho ni asilimia fulani ya mapato yao kibinafsi ambacho watachangia towards kutimiza majukumu pale nyumbani mathalan karo ya shule, Bill ya simu, umeme, maji chakula nk. Atakacho baki nacho kila mtu atumie kwa majumu ya kibinafsi, Ikiwa mwenzako anahitaji basi ukamuongezea.
Hesabu ya asilimia inamwezesha kila mtu basi kuchangia kulingana na uwezo wake. Haibagui ni mme au mke.
 


lakini je? kiukweli unaamini/unadhani kumpa mshahara wako ili 'kusawazisha' mambo ndio suluhisho la kudumu?

Vipi inapokuja suala la kusaidia ndugu upande wa mume, ndugu upande wako (mke), na maamuzi kwa ujumla ndani ya nyumba yenu kuhusiana na matumizi ya fedha?.

kwa muda gani utaachia hali hii iendelee? ?

naamini ni suluhisho la kudumu, kwani kupanda na kushuka kifedha ni hali ya kawaida iwe mke au mme, huwezi kujua siku moja mimi naweza kurudi chini, nayeye anweza akainuka tena,

cha muhimu ni kwamba ile hali iliyokuwa ikimpa unyonge kwamba yeye sio “dereva” katika maamuzi ya ki fedha haipo, na ndio hasa iliyojuwa ikileta tatizo,

kwa maswala ya kusaidia ndugu hakuna kilichobadilika, kuna kiasi cha pesa ambacho kila mmoja anaweza kutoa kwenye account (per month )bila kujadiliana, mahitaji ya kusaidia ndugu yakizidi kiasi hicho, tunajadiliana na kukubaliana tusaidie vipi, hii ina apply kwa ndugu wa upande wangu na wake pia

kama nilivyosema kuhusiana na matumizi ya fedha na bajeti kwa ujumla yeye alikuwa kiongozi, ninachokiepuka ni kuchukua uongozi na kumweka benchi, ati tu kwa sababu mshahara wangu umekuwa mkubwa kumzidi

nitaendelea as long as kipato chake hakitoshelezi mahitaji. Baada ya hapo sijajua itakuwaje

hapa point ni kwamba kwa sisi nimeprove kwamba :
1. Sio practical kwamba eti yeye awe kiongozi wa masuala ya fedha ambayo haipo mikoni mwake
2. Mimi kuchukua uongozi kifedha kwa sababu kipato chake ni kidogo kunampa insecurity, hali ambayo inaleta mushkeli na haimsaidii yeye wala mimi kama tuition ya Haika inavyoeleza hapo juu
 
...nitaendelea as long as kipato chake hakitoshelezi mahitaji. Baada ya hapo sijajua itakuwaje

hapa point ni kwamba kwa sisi nimeprove kwamba :
1. Sio practical kwamba eti yeye awe kiongozi wa masuala ya fedha ambayo haipo mikoni mwake
2. Mimi kuchukua uongozi kifedha kwa sababu kipato chake ni kidogo kunampa insecurity, hali ambayo inaleta mushkeli na haimsaidii yeye wala mimi kama tuition ya Haika inavyoeleza hapo juu


well said Triplets, Uzidishiwe!
 

Kwa jamii nyingi hasa za kiafrika, hata nyumbani Tanzania, bado inaonekana ni jukumu lako mume kutimiza kama si yote, basi kwa asilimia kubwa mahitaji ya mkeo na watoto, pamoja na nyumba kwa ujumla.

Wakati huo huo, wanawake wengi sasa sehemu mbali mbali duniani ikiwamo Tanzania, baadhi mmekuwa na uwezo mkubwa tu kifedha kuliko waume zenu.

mfano; Mke unakuwa na cheo kikubwa kuliko mumeo, mke unakuwa na mshahara mkubwa kuliko mume, au mke unakuwa na uwezo mkubwa kimaisha kuliko mumeo!


Huenda hili linatokana na haki sawa mnazozipata kwenye elimu, kazi, madaraka na hata wale mnaomudu kufanya biashara kubwa...

Je, mabadiliko haya yanaathari zipi katika ndoa, ...na je? njia zipi zinafaa kuepusha migogoro, ili mume nawe 'ujisikie/ajiskie ni mwanaume' nyumbani kwenu?


Ngoja na mimi nitoe yangu machache.....

Katika Dunia ya leo, Bi'mkubwa kuwa na kipato zaidi ya Bw'mkubwa ni kawaida kabisa. Hii ishu wala sio ya kuchanganyikiwa/kushangaa tena.

Sasa basi, migogoro mingi (ambayo pengine usababisha kwa sitwesheni mzima kuonekana kana kwamba tofauti ya kipato inamfanya Bw'mkubwa kuwa mdogo) uanzia pale matumizi ya Bw'mkubwa yasiyoeleweka yanapogundulika.

Kutokana na nyendo za Bw'mkubwa (hasa wa kibongo), utaona kwamba wana matumizi mengi ambayo ni ya kibinafsi (ulevi) au yenye kunufaisha watu wengine nje ya familia yake (vimada na marafiki). Matumizi haya huwa yapo, haijalishi nani ana kipato kikubwa.

Tofauti ni kwamba, kwenye familia ambayo Bw'mkubwa ndio mwenye kipato cha juu, Bi'mkubwa huwa ana kosa haki (ingawaje anatakiwa awe nayo) ya kuuliza kuhusu matumizi hayo.

Sasa kwenye familia ambayo mtiririko wa kipato uko tofauti na wa kiutamaduni, utakuta Bi'mkubwa anajikuta ana nguvu za haki za kuuliza kuhusu matumizi yote ya kifamilia na ya kibinafsi.

Na pindi Bw'mkubwa akishindwa kutoa maelezo yanayoeleweka, hapo ndipo cheche za migogoro zinapoanza.

Hatimaye, Bw'mkubwa kujiona kuwa ana onewa/nyanyaswa kwa sababu kipato chake kidogo.
 
Ngoja na mimi nitoe yangu machache.....

Katika Dunia ya leo, Bi'mkubwa kuwa na kipato zaidi ya Bw'mkubwa ni kawaida kabisa. Hii ishu wala sio ya kuchanganyikiwa/kushangaa tena.

Sasa basi, migogoro mingi (ambayo pengine usababisha kwa sitwesheni mzima kuonekana kana kwamba tofauti ya kipato inamfanya Bw'mkubwa kuwa mdogo) uanzia pale matumizi ya Bw'mkubwa yasiyoeleweka yanapogundulika.

Kutokana na nyendo za Bw'mkubwa (hasa wa kibongo), utaona kwamba wana matumizi mengi ambayo ni ya kibinafsi (ulevi) au yenye kunufaisha watu wengine nje ya familia yake (vimada na marafiki). Matumizi haya huwa yapo, haijalishi nani ana kipato kikubwa.

Tofauti ni kwamba, kwenye familia ambayo Bw'mkubwa ndio mwenye kipato cha juu, Bi'mkubwa huwa ana kosa haki (ingawaje anatakiwa awe nayo) ya kuuliza kuhusu matumizi hayo.

Sasa kwenye familia ambayo mtiririko wa kipato uko tofauti na wa kiutamaduni, utakuta Bi'mkubwa anajikuta ana nguvu za haki za kuuliza kuhusu matumizi yote ya kifamilia na ya kibinafsi.

Na pindi Bw'mkubwa akishindwa kutoa maelezo yanayoeleweka, hapo ndipo cheche za migogoro zinapoanza.

Hatimaye, Bw'mkubwa kujiona kuwa ana onewa/nyanyaswa kwa sababu kipato chake kidogo.

...shukran QM, namsubiri mama naye aje amwage busara zake hapa...:D
 
Duu, mjadala mzuri kweli,
Labda nitoe uzoefu wangu ambao umeifanya nyumba yangu iwe edeni ndogo lol!

Kuwa na kapu moja, yaani pato la mji, kama kapata mama anaweka kama baba anaweka na zote huwa ni zetu bila kujali huyu kaweka mbili huyu kaweka tatu, kwani kama wengine walivo changia siku hizi leo aweza weka tatu mwenzie mbili kesho kutwa ikawa tofauti aliye weka mbili akaweka saba!

Kutegemea na viwango vyenu ( mzee wa vijisenti) matumizi makubwa makubwa mnajulishana, mfano kama mji wenu alfu 20 ni nyingi basi hiyo mna ambizana, lakini yale madogo madogo ya vocha na soda, hapo mna chukua na kugawiana kwamba mwenzio leo wallet yangu haina senti na mna geana, na zikiisha yeyote yule anachukua ATM na kudraw na password za ATM zote ziko huru kati yetu.

La msingi hapa ni kila mmoja kuwa mwaminifu na kuondoa tabia za matumizi ya kichini chini ambayo mara nyingi yanakiuka maadili na misingi ya ndoa.

Kusaidia ndugu kama kiwango ni kikubwa ni swala la kuweka priority na mkajadiliana kipi kifanyike nani asaidiwe kwanza kulingana na uwezo wenu.

Ni uzoefu wangu tu wakuu, na kwangu yaani mtindo huu una nifanya kama signature ya ngabu, ...'having more fun than...... kila mmoja akimuheshimu na kumpenda mwenzie hadi kifo... inshalah.
 
Penzi-kipato =mgogoro kwa wahusika ambao wameamua kuwa na migogoro au wameshindwa kupevuka na kufanya maamuzi ya busara kuizuia au kuisuluhisha.

sababu kubwa nadhani ni
ujeuri wa mmoja wao
kukataa kujishusha.
kutokujua madhara yake
kutokujali whatever the case.
lakini kwa kuwa ni watu wazima tunawachia.
Ila vijana pls commit yourself to someone you can trust only.
 
Asante sana watoa mada nimefurahi sana kusikia maoni haya. Pamoja na kipato utandawazi/mazungumzo stories vinachangia sana kwenye migogoro ya nyumbani. Watu wengi wake kwa waume wanapata uzoefu wa mapenzi aidha kwa kuona au kwa kutendewa kitu ambacho kinapelekea mabishano katika ndoa na kuanza kukomoana. Nilipata habari kwa mwenzangu mmoja ambaye aliambiwa na mkewe mbona....kama wenzako!!!!!! shock ee, au mimi napendeza kama wewe huanitamani kuna wenzio wananitamani sana.

Ikifika hapo nani anacho zaidi ndiye atakayeonyesha makeke zaidi. Na mmoja asipojishusha na kujifanya mjinga mambo yanafika ukomo. Mungu atusaidie
 
Naomba tusiishie kwenye kipato tu kama chanzo cha migogoro hebu tuangalia some other sources of family conflicts and hopefully posible solutions.
 
Mwanaume kuwa rijali 100% ni ngumu kama ilivyo mwanamke kuwa mtii 100%
tukubali kukosa kidogo kila upande.
manake hapa mimi napata picha ya mwanaume rijali kiafrika ni yule ambaye maamuzi yote ya nyumbani anafanya yeye. mimi kama mwanamke sitamuweza.

Kwa ajira za sasa, kupanda na kushuka kwa kipato si kitu cha muda mrefu sana.
sisi tumeshawahi kusimamia nyumba kwa zamu mara kibao, ila tofauti ni kuwa yeye akiwa nazo anatoa kiasi fulani anaweka mahali/account naweza kuchuka bila kuombaomba kila saa, na mimi pia hivyo hivyo, ila uwazi katika jumla kuu ni muhimu.
Pia kwamba balance uliobaki nayo ni kwaajili ya personal use tu.
inahitaji kujitoa zaidi na TOTAL TRUST IN EACH OTHER. Ambayo nadhani kwa muelekeo wa hapa ni ndogo.
tution ya bure kwa kina dada (ambao bado bado) ukiua self confidence ya mumeo utamchukia mara moja. Jitahidi aweze kutembea kifua mbele humu duniani, hasa kwa rafiki zake na ndugu.

Yaani haika nimekupenda gafla!

Nilitaka kusema uliyosema lakini ndo hivo tena wanasema umenipre'empty'

Lakini pia nibwabwaje kuwa
1. kwa mazingira ya sasa, hakuna guarantee kuwa mwanaume ataendelea kuwa na kipato kikubwa kuliko mwanamke..kuna mambo ya uwezeshaji kielimu na kijamii kwa ujamla kwa wanawake, kwa hiyo muhimu kwa sisi wanaume ni KUTAMBUA hali hiyo na kujiandaa kukabiliana nayo

2. huwa nasema siku zote kuwa mwanamke aliye kweli MWANAMKE na kukubali UANAMKE wake, 'hatamsuta' mumewe kwa vile tu ana kipato kumzidi, sana sana atampenda zaidi na kumfanya atembee kifua mbele..kwani kuna haja gani kwa jamii kujua kuwa natembelea gari la mke wangu, au nguo nimenunuliwa na mke wangu? in the first place, ni fahari kwangu! kwa nini ionekane kitu cha ajabu kama wote ni mwili mmmoja?

3. Jingine, kwa wanawake, wasikubali kupotoshw ana ile dhana kuwa ukombozi wa mwanamke unamaanisha kumkandamiza mwanamume hata mumeo wa ndoa..angalia wale wote wanaohubiri haki za wanawake utakuta lau walishaolewa wakaachika au hawajawahi au wamekuwa na uzoefu mbaya kwenye mahusiano yao.

4. Hili wala halihitaji kulisema: Ndo nyingi hasa kwa wenzetu 'walioendelea' zinavunjika kwa sababu ya mambo haya haya ya kubishana 'nani mkubwa' na 'nani mdogo'...taasisi nzima ya ndo imedhalilishwa kiasi kuwa sasa thamani yake haionekani tena..ukiangalia chanzo chake ni mambo haya haya!
 
Upendo, heshima na uwazi ni vitu vya msingi kweli kwenye ndoa. Hiyo ni kwa experience yangu. Lakini pia ninaexperience ya ndoa zilizokosa hayo mambo matatu yaliyo muhimu kwenye ndoa yangu na kujua ni jinsi gani hali inaweza kuwa mbaya yanapokosekana.

Kwenye familia yangu kila kipato kinamilikiwa kwa jumla na kutumia ni kutokana na jinsi tunavyopangilia mipango yetu kwa kuzingatia priorities tulizojiwekea. Mfumo wetu huu umewakwaza familia zetu kwa pande zote mbili kwani wanashindwa kexercise authorities ambazo hawana lakini wanataka kujitwalia. Imechukua muda kuikubali hali hiyo, lakini sisi wawili tuko vizuri kabisa. All our money is owned jointly. All our properties owned jointly na our next of kin ni watoto wetu ambao wote ni wa kike, jambo ambalo baadhi ya wana ndugu hawalielewi kabisa.

Mkipendana, Mkaheshimiana na kuwa wawazi, mambo kwa kweli si magumu kiasi hicho, ila kufanikisha hayo kunahitaji jitihada kubwa kweli, hasa ikizingatiwa nyie wawili mmetoka kwenye background tofauti, jamii nayo ina mtazamo tofauti (mfumo dume) na pengine wanaowazunguka wana mitizamo tofauti.

Lakini mkifanikiwa, bwana ni mbingu yenu hapa duniani.
 
...ni kutokana na jinsi tunavyopangilia mipango yetu kwa kuzingatia priorities tulizojiwekea. Mfumo wetu huu umewakwaza familia zetu kwa pande zote mbili kwani wanashindwa kexercise authorities ambazo hawana lakini wanataka kujitwalia. Imechukua muda kuikubali hali hiyo, lakini sisi wawili tuko vizuri kabisa. All our money is owned jointly. All our properties owned jointly na our next of kin ni watoto wetu ambao wote ni wa kike, jambo ambalo baadhi ya wana ndugu hawalielewi kabisa.

...


...yaani, umesema kweli tupu! kwa tafsiri nyingine, kauchoyo fulani kanahitajika kwenye hizi jamii zetu za kiafrika zinazodhani mke akishaolewa kwa mume mwenye pesa 'wandugu na mashemeji' wanajiona ndio pepo yao,
...wakati huo huo wewe mwanaume ukioa kwenye familia/mke mwenye kipato unaonekana kana kwamba umefuata kitu, au 'unakaliwa!'...
 
...
4. Hili wala halihitaji kulisema: Ndo nyingi hasa kwa wenzetu 'walioendelea' zinavunjika kwa sababu ya mambo haya haya ya kubishana 'nani mkubwa' na 'nani mdogo'...taasisi nzima ya ndo imedhalilishwa kiasi kuwa sasa thamani yake haionekani tena..ukiangalia chanzo chake ni mambo haya haya!


...mfumo dume huo ndio unaomfanya mwanaume ajiskie yeye ndio kichwa cha nyumba!

kuna wanaofuata amri za dini zao, kuna wanaofuata malezi walokuzwa nayo, almuradi adjustments toka kwenye mfumo dume kuwa hakisawa kwa wote, au pengine kujishusha zaidi ya hapo ndio mgogoro zikifuatiwa na Kauli kama "mwanaume mzimaaa,...", au "haitambuliki mwanaume nani mwanamke nani",....

Kuna wanawake wenye expectations mwanaume lazima uwe rijali, na kuna wanaume wenye expectations mwanamke lazima uweze! nakumbukia post ya Haika aliyosema , kuna ulazima kusikiliza kwa makini 'yanayotamkwa' wakati wa uchumba!

Yani wakati wa uchumba, umfahamishe unachukuliaje fedha, majukumu ya kifedha, na mambo yote unayodhani ni muhimu kwako na mtazamo wako kifedha. Mtazame reaction yake ya maneno au matendo, bora kinga kuliko tiba -Haika


au mnaonaje?
 
Off the track
Romance Without Finance Is Nuisance

...Oh oh Icadon,...

inaelekea ulimsikiliza sana Gwen Guthrie na kibao chake; AIN'T NOTHIN' GOIN' ON BUT THE RENT.

:D

...anyway, naamini dunia ya leo, kila mtu na priorities zake kwenye ndoa.
 
Katika mahusiano especially madada na makaka wa kizazi cha dot.com, swala la finance na career linatuchukulia mda sana.

Its tough to balance the two especially kama kila mtu ana kazi yake ataogopa kuiacha na kumfuata mwenzake. Na maana siyo gurantee kwamba mtakuwa kituo kimoja cha kazi. Nimeshaona washkaji mpaka wanahonga kutafuta uhamisho wa wenzi wao, ikishindikana ndo hivyo..yanakuwa mapenzi ya mbali..na wote humu tunajua madhara yake..hawakawii wengine kukusaidia kutoa huduma on either side(kwa mwanamke na mwanaume)!....

Kikubwa ni Trust, but how?

KAzi ipo wandugu!
 
Katika mahusiano especially madada na makaka wa kizazi cha dot.com, swala la finance na career linatuchukulia mda sana.

Its tough to balance the two especially kama kila mtu ana kazi yake ataogopa kuiacha na kumfuata mwenzake. Na maana siyo gurantee kwamba mtakuwa kituo kimoja cha kazi. Nimeshaona washkaji mpaka wanahonga kutafuta uhamisho wa wenzi wao, ikishindikana ndo hivyo..yanakuwa mapenzi ya mbali..na wote humu tunajua madhara yake..hawakawii wengine kukusaidia kutoa huduma on either side(kwa mwanamke na mwanaume)!....

Kikubwa ni Trust, but how?

KAzi ipo wandugu!

Trust ina face nyingi sana, mfano ni trust kwa mwenzio akikaa mbali hatakusaliti,
au trust kwa mwenzio kuwa ukiacha kazi ukamfuata utakuwa salama pia
au trust kwa mwenzio kuwa hakudanganyi anapokuambia nenda tu ukirudi utanikuta.
ni jambo ambalo wewe mwenye kwanza uweze kuwa muaminifu ndio utegemee mwenzio akuamini.
Watu wanashida sana siku hizi kwani wanataka the best partner wakati wao ni the worst. utapata wapi?
kama wewe unataka uaminiwe, kuwa mwaminifu, kama unataka mwenzio awe muwazi, make extra effort wewe kuwa muwazi, na kadhalika
 
ni ya muda but Haika i agree with your comments!TRUST,make sure wewe ni mwaminifu before hujam jurge mwenzio kuwa si mwaminifu,unajua bwana kama wewe si mwaminifu weweunadhani mwenzio naye yupo hivyo
 
NIMEGUSWA HAIKA..MAANA ULILOONGEA NDO REAL LIFE YANGU..i wish mtu fulani angekuwa anaingia humu asome
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom