warumi
R I P
- May 6, 2013
- 16,273
- 18,379
BAADA ya kudaiwa na staa wa Bongo Fleva , Nasibu Abdul ' Diamond Platnumz' kuwa alichoropoa mimba zake mbili , mtangazaji wa Radio E - FM, Penniel Mungilwa ' Penny ' ameibuka na kujibu mapigo kwamba mwanamuziki huyo hana uwezo wa kumpa mwanamke mimba, Risasi linakupa mchapo kamili
CHANZO CHA YOTE
Akizungumza na GlobalTV Online kwenye ofisi za gazeti hili Bamaga - Mwenge jijini Dar , hivi karibuni, Diamond alifunguka : "Nilimpa (Penny ) mimba ya kwanza , sikuamini ikabidi twende naye hospitalini tukapime , akaambiwa anayo… nikafurahi nikampiga na ndinga (gari) mpya siku hiyohiyo, nikamwambia mama tulia unizalie mwanangu . "Sikukaa sana akaniletea maneno… oooh mara hivi mara vile … eti imetoka . Nikasema poa, labda haikuwa riziki. Nikampa ya pili, nayo pia akatoa . Nikasema bora niachane naye na huo ndiyo ukawa mwisho wa mimi na Penny . "
KILICHOFUATA
Baada ya habari hiyo kuchapishwa kwenye gazeti ndugu la hili, Amani wiki iliyopita , Penny alijibu mapigo na kudai kwamba ni kweli staa huyo alikuwa akimridhisha kimapenzi lakini hakuwa na uwezo wa kumpachika mimba kama alivyodai . " Diamond ni mwanaume kama wanaume wengine lakini hana uwezo wa kumpa mwanamke mimba , muulizeni vizuri tatizo ni nini, " alisema Penny .
DIAMOND ANASEMAJE ?
Alipofikishiwa taarifa hizo , Diamond hakutaka kufunguka kwa madai kwamba kuna vitu huwa hataki kuvisema kwa kuwa ni mtoto wa kiume na huwa
anahifadhi siri nyingi za wanawake .
DIAMOND ANA TATIZO ?
Kwa mujibu wa Penny ni kwamba alikuwa akimridhisha vizuri kimapenzi hivyo hana tatizo la nguvu za kiume isipokuwa hawezi kumpa mwanamke kibendi .
KITAALAM ZAIDI
Akizungumzia tatizo la Diamond ( kama maelezo ya Penny ni kweli ) , mtaalam wa masula ya tiba ya uzazi wa gazeti hili (jina tunalo) alisema kuwa mwanaume anaweza kumridhisha vizuri mwanamke wanapokuwa kitandani isipokuwa akashindwa kumpa ujauzito.
"Tatizo la kutopata ujauzito , maana yake mume na mke walio katika uhusiano wa kutafuta mtoto ndani ya mwaka mmoja, lakini wameshindwa .
"Inaweza ikawa zaidi ya mwaka mmoja lakini wastani wa kiwango cha chini ni mwaka mmoja . " Ni tatizo kubwa katika jamii kwani kila mmoja anataka afikie malengo ya kuwa na familia kama anavyotaka Diamond . "Mwanamke na mwanaume wote wanahusika katika tatizo hili japo mara nyingi huonekana ni la mwanamke.
Credit: GPL
CHANZO CHA YOTE
Akizungumza na GlobalTV Online kwenye ofisi za gazeti hili Bamaga - Mwenge jijini Dar , hivi karibuni, Diamond alifunguka : "Nilimpa (Penny ) mimba ya kwanza , sikuamini ikabidi twende naye hospitalini tukapime , akaambiwa anayo… nikafurahi nikampiga na ndinga (gari) mpya siku hiyohiyo, nikamwambia mama tulia unizalie mwanangu . "Sikukaa sana akaniletea maneno… oooh mara hivi mara vile … eti imetoka . Nikasema poa, labda haikuwa riziki. Nikampa ya pili, nayo pia akatoa . Nikasema bora niachane naye na huo ndiyo ukawa mwisho wa mimi na Penny . "
KILICHOFUATA
Baada ya habari hiyo kuchapishwa kwenye gazeti ndugu la hili, Amani wiki iliyopita , Penny alijibu mapigo na kudai kwamba ni kweli staa huyo alikuwa akimridhisha kimapenzi lakini hakuwa na uwezo wa kumpachika mimba kama alivyodai . " Diamond ni mwanaume kama wanaume wengine lakini hana uwezo wa kumpa mwanamke mimba , muulizeni vizuri tatizo ni nini, " alisema Penny .
DIAMOND ANASEMAJE ?
Alipofikishiwa taarifa hizo , Diamond hakutaka kufunguka kwa madai kwamba kuna vitu huwa hataki kuvisema kwa kuwa ni mtoto wa kiume na huwa
anahifadhi siri nyingi za wanawake .
DIAMOND ANA TATIZO ?
Kwa mujibu wa Penny ni kwamba alikuwa akimridhisha vizuri kimapenzi hivyo hana tatizo la nguvu za kiume isipokuwa hawezi kumpa mwanamke kibendi .
KITAALAM ZAIDI
Akizungumzia tatizo la Diamond ( kama maelezo ya Penny ni kweli ) , mtaalam wa masula ya tiba ya uzazi wa gazeti hili (jina tunalo) alisema kuwa mwanaume anaweza kumridhisha vizuri mwanamke wanapokuwa kitandani isipokuwa akashindwa kumpa ujauzito.
"Tatizo la kutopata ujauzito , maana yake mume na mke walio katika uhusiano wa kutafuta mtoto ndani ya mwaka mmoja, lakini wameshindwa .
"Inaweza ikawa zaidi ya mwaka mmoja lakini wastani wa kiwango cha chini ni mwaka mmoja . " Ni tatizo kubwa katika jamii kwani kila mmoja anataka afikie malengo ya kuwa na familia kama anavyotaka Diamond . "Mwanamke na mwanaume wote wanahusika katika tatizo hili japo mara nyingi huonekana ni la mwanamke.
Credit: GPL