Kardinali Pengo: Wanasiasa waacheni Maaskofu wafanye kazi zao, msiwafundishe kazi

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo anazungumza katika mazishi ya Askofu Mayala Mwanza ambako anazungumzia ufisadi na maovu mengine, lakini anaonekana kukemea ufisadi huku akionekana kuwabeza wanaopambana na ufisadi. Iko live Star TV.

Yuko JK na Mkapa
Na Betty Kangonga
Tanzania Daima


ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amewashukia makamanda wanaopigana vita dhidi ya ufisadi kwa kuwataka wawe na dhamira ya kweli katika kukabiliana na ufisadi nchini.

Kardinali Pengo, alisema bila dhamira ya kweli, vita hiyo haiwezi kufanikiwa kwani wanaopiga kelele bila kusukumwa na dhamira ya kweli, wataonekana kama wana wivu kwa kukosa fursa ya kuwa mafisadi.

Alitoa kauli hiyo jana wakati wa ibada ya kumuaga Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza, Anthony Mayala (69), aliyefariki dunia Agosti 19 na kuzikwa jana katika Kanisa la Mtakatifu Epifania, Parokia ya Bugando, jijini Mwanza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyopatikana jana jijini Dar es Salaam, Pengo alisema Watanzania wengi wanaokemea ufisadi, wanaongeza hasira kwa jamii, kwani uovu huo bado unaendelea kufanywa na mafisadi kwa vile wapiganaji wenyewe hawana dhamira ya kweli.

"Wote tunalalamika na kulaani matendo ya ufisadi, kama kweli tungekuwa tunalaani kutoka ndani ya mioyo yetu, basi vita hivi vingepungua ama kuisha kabisa nchini kwetu.

"Kupigia kelele ufisadi, bila dhamira ya kweli kunaonyesha hisia tu na ni bora kuacha kulizungumzia suala hilo kwani linaongeza hasira kwa wananchi na hata kusababisha amani iliyokuwepo nchini kutoweka," alisema.

Pengo alisema, makamanda wa ufisadi, lazima wajiulize kwanza wao binafsi wamechangia kwa kiasi gani katika kuwaibia wananchi, ndipo waanze kupiga vita ufisadi kwa kuwa hawana makosa.

"Hakuna aliye mkamilifu, wengi wetu tumekuwa tukiwapinga mafisadi, huku sisi tukijiona wema wakati kwa upande mwingine bado wanafanya ufisadi na kuwaibia watu, ndiyo maana vita hii kamwe haiwezi kuisha,'' alifafanua Kardinali Pengo.

Bila kutaja majina ya watu, Kardinali Pengo alisema baadhi ya wapiganaji wa ufisadi, wanafanya hivyo kwa kuwa wamekosa nafasi ya kuwa mafisadi, hivyo wanawaonea wivu wenye nafasi ya kufanya ufisadi.

Aliwageukia maaskofu wenzake kwa kuwataka wawe imara na wasiwe tayari kuyumbishwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa, kwani dini na siasa kamwe haviwezi kwenda pamoja.

"Mambo yanayoendelea kutokea katika nchi yetu hatuelewi yanatupeleka wapi, kwani tunashangazwa na chama kuingilia masuala ya maaskofu ambayo ni mema, kwani yana lengo la kusaidia jamii iwe na viongozi wenye maadili.

"Leo unafikia hatua ya kumwambia askofu haruhusiwi kufanya jambo lolote mpaka akutane na chama na kupewa ruhusa ya kujua namna ya kuandika waraka huo, huko ni kutaka kuingilia mamlaka ya Kimungu na kamwe haitawezekana.

"Waacheni maaskofu wafanye kazi zao na wasifundishwe kazi, kwa maana kuandika waraka huo ni mamlaka kutoka kwa Mungu na si kwa uwezo wao, vyama visilazimishe kuwa lazima vitoe ushauri, huo ni upuuzi na inaonyesha kuchanganyikiwa," alieleza Kardinali Pengo.

Ingawa Kardinali Pengo hakumtaja mtu, lakini kwa kauli hii ni dhahiri kuwa alimlenga mkongwe wa siasa nchini, Mzee Kingunge Ngombale- Mwiru ambaye siku za hivi karibuni, alijitokeza hadharani kuupinga waraka wa Kanisa Katoliki, kwamba unaweza kuhatarisha amani na utulivu nchini.
 
ndio unafiki wake huo...
viongozi wa dini inapaswa wawe straight na hoja na si kuiongea kwa mafumbo ambayo si rahisi kung'amuliwa na asilimia 75 ya wananchi wetu..
 
Anasema waraka wa kichungaji haupaswa kuomba baraka kwa wengine, na anasema Maaskofu waachwe wafanye kazi yao bila kuingiliwa na mamlaka yoyote iwe ya chama ama yoyote kwani Mwenyezi Mungu ndiye anayewaongoza, wanatenda kwa dhamira ya dhati. Ikiwa Maaskifu lazima waawaconsult political sysytem watachanganyikiwa
 
ndio unafiki wake huo...
viongozi wa dini inapaswa wawe straight na hoja na si kuiongea kwa mafumbo ambayo si rahisi kung'amuliwa na asilimia 75 ya wananchi wetu..
Usiwaonee mkuu.

Alichosema ni kuwa anawambia MOJA KWA MOJA kuwa wasiwafundishe kazi maaskofu kuwa wasifanye hivi na wafanye hivi.

Amewapa moja kwa moja bila kuwaficha. Kasema wasitake maaskofu waonekane wanaenda kisiasa ilhali si dhamira yao.

Hapendi kuongelea siasa msibani lakini anapenda kuona Tanzania inakuwa njema.
 
Nimependa namna ambavyo ameonekana kuongea bila kuona haya mbele za JK na BWM. Hii ndiyo inatakiwa, hakuna kumwangalia mtu usoni.

Naona sasa wanaendelea na ibada. Si wengine mlikuwa mnaona via JumpTv? Si lazima uwe Tanzania
 
Kwa kweli amewapa bila woga wowote. Hajamungunya maneno kuhusu ufisadi na serikali au chama kuingilia Barua za kichungaji kutoka kwa maaskofu (Hapa alikuwa anampa kijembe Kingunge) na kutoa mfano tawala za kikomunisti zilivyoshindwa katika kupingana na uenezaji wa barua hizo
 
Kwa kweli amewapa bila woga wowote. Hajamungunya maneno kuhusu ufisadi na serikali au chama kuingilia Barua za kichungaji kutoka kwa maaskofu (Hapa alikuwa anampa kijembe Kingunge) na kutoa mfano tawala za kikomunisti zilivyoshindwa katika kupingana na uenezaji wa barua hizo
TBC1 wanaonyesha pia mkuu? Huwa wanapatikana online? Quality ya StarTv si nzuri natafuta alternative
 
Hivi naweza kuona online kwa kutumia internet?
Hapo wanaweza kumpa chance BWM ajisafishe nae
 
Lakini anaonekana kukemea ufisadi huku akionekana kuwabeza wanaopambana na ufisadi.

'Hii ndio inaweza kumsababisha mtu amwite Mnafiki' . Mtoa habari tafadhari toa habari kamili na donoa dodoa hii yaweza kutufanya wengine tupatwe na mdondo hasa ingizingatiwa kwamba watu hawa wa kanisa tunawafahamu fika kwa maana kwamba tumetokea humo na yemetushinda ya upadrisho na mengineyo.
 
Lakini anaonekana kukemea ufisadi huku akionekana kuwabeza wanaopambana na ufisadi.

'Hii ndio inaweza kumsababisha mtu amwite Mnafiki' . Mtoa habari tafadhari toa habari kamili na donoa dodoa hii yaweza kutufanya wengine tupatwe na mdondo hasa ingizingatiwa kwamba watu hawa wa kanisa tunawafahamu fika kwa maana kwamba tumetokea humo na yemetushinda ya upadrisho na mengineyo.

Alisema kwamba kama wote wanaopiga kelele za ufisadi wangekuwa wanafanya hivyo kwa dhati ya moyoni, kusingekuwa na ufisadi nchini na kwamba isije kuwa wanaopiga kelele wamekosa fursa za kufanya ufisadi kutokana na mafisadi kuzimaliza.
 
Alisema kwamba kama wote wanaopiga kelele za ufisadi wangekuwa wanafanya hivyo kwa dhati ya moyoni, kusingekuwa na ufisadi nchini na kwamba isije kuwa wanaopiga kelele wamekosa fursa za kufanya ufisadi kutokana na mafisadi kuzimaliza.
Hicho ni kijembe mkuu kwa CCM inayosema wanapambana na mafisadi lakini hawasemi ni akina nani na wako wapi!
 
Pengo Nimemkubali leo: "Unapomuua nyani usimwangalie usoni"
Nasubiri kuona magazeti kesho yataandika nini... Tatizo StarTv inaelekea wataonyesha ibada ya mazishi na si mazishi kwa ujumla. Wapo Kawekamo jijini Mwanza
 
Back
Top Bottom