Pengo: Nchi imeoza!

Sasa hii inamaanisha kwamba ni amri ya kupiga vita maovu?

Hiyo ilishabadilishwa na mengi yameandikwa kwamba sheria does not count anymore.

Romans 10:4 Christ is the end of the law so that there may be righteousness for everyone who believes.

Kama unaaamini tafsiri yangu sio sahihi nijulishe nilete ushahidi wa tafsiri niliyoitaja kwa mujibu wa wahubiri wenyewe.

Oh, my God! Hivi wenzetu huwa mnasoma nini? Biblia ina 'deep meaning'. Amesema - He's The Way, The Truth and The Life. Na amefundisha kuhusu watu kuwa 'mwanga', 'chumvi' ya ulimwengu na above all, amefundisha upendo...

Kusema he's the end of the law, it means he's the end of 'legalism' - lazima ujue alikuwa anaongelea katika 'context' gani - ambayo watu walikuwa wamepoteza maana ya sheria na kubakiza 'legalism' - jino kwa jino, jicho kwa jicho... na ndiyo maana yeye alisema: "Mmesikia watu wakisema jino kwa jino au jicho kwa jicho lakini mimi nawaambia... wapende hata maadui zenu na kuwaoambea (ile wabadilike).

Watu walimletea mwanamke mzinifu ili wasikie atasema nini lakini yeye aliwaambia "asiye na dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe..." nk. Alifundisha "enendeni duniani kote na kuwafundisha wote kushika haya niliyowaamuru kuyashika na tazama mimi niko nanyi mpaka mwisho wa dunia..."
 
Asante kwa changamoto.

Labda kwanza nianze kwa kukuomba ulete quote ya hapo niliposema waraka unatishia amani.

Nirudie tena msingi wa hoja yangu.
Mtu anaweza kuzungumza katika capacity tofauti. Angekuwa amezungumza kama Raia wa kawaida hapo angekuwa Raia kasema kama vile wewe, mimi, mwanasiasa na kadhalika.

lakini hapo kazungumza kama Kiongozi wa kanisa. Ninahoji, je aliyoyasema anaweza kuya support na maandishi?Nimeuliza wapi ameamriwa kupiga vita yale anayoyaona ni maovu.

Kama hana ulazima wa kuamriwa ili apige vita maovu kama walivyoashiria wengine pia haina tatizo, ili mradi 'isemwe wazi' kwamba maelekezo na mafundisho ya anayoyasema kama Kiongozi wa kanisa hayana ulazima wa kuwa supported na maandishi yake matakatifu. Kwa maana nyingine imani zake zinampa mamlaka ya kusema lolote hata kama anachosema hakina mwongozo huo ndani ya vitabu vyake.

Sina tatizo na content za waraka, nina question process and scope of what he can say and cannot say in his offcial capacity.

Angekuwa Rais tungesema katiba inamdhibiti. Kama Kiongozi wa Kanisa ni kipi kinachodhibiti matamshi yake?

Je, unataka uthibitisho kutoka kwenye Biblia au sheria za Kanisa? Biblia ni 'fundamental document', mafundisho ya Kanisa ni 'application' ya Biblia katika 'contex' ya walengwa (Wakatoliki/Wakristo au mtu yeyote anayeguswa na ujumbe wake) na Canon law (Sheria za Kanisa) - rules of permission & prohibition. Kwa hiyo, ni wapi unataka kuelewa katika hayo niliyotaja?

Pili, kutafsiri kinachofanyika katika Kanisa Katoliki kwa kutumia mtazamo wa dini nyingine ni offpoint.

Anyway, Amri za Mungu Kumi zinakataza kwa kusema: Usiibe [pamoja na rushwa, ufisadi etc], Usiseme uongo [pamoja na udanganyifu, ulaghai etc], Usiue [pamoja na kushiriki kuua, kueweka mazingira ya kufanikisha kuua etc], Usitamani mali ya mtu mwingine (pamoja na kutamani kupora mali ya umma au kujinufaisha na mali ya umma, kutamani kumiliki mali ya umma kwa matumizi binafsi etc]...

Yesu alifundisha kuhusu uadilifu na namna ya kuuishi na mwisho wa yote aliwatuma mitume wake akisema: "Enendeni duniani kote kuwafanya wote kuwa wanafunzi wangu/kuhubiri Habari Njema (Good News - God's saving justice)... na kuwafundisha wote ambayo nimewaamuru kuyashika... Atakayeamini na kubatizwa (atakayeipokea Habari Njema na kuishi kiadilifu) ataokoka na asiyeamini (asiyeipokea na kutoishi kiadilifu) ataangamia."

 
Ona miafrika. Badala ya kujadili "uozo wa nchi" yenyewe inamjadili aliyeanzisha mada, haki zake na dini yake.

Halafu tunashangaa kwanini hatuendelei?
 
Ona miafrika. Badala ya kujadili "uozo wa nchi" yenyewe inamjadili aliyeanzisha mada, haki zake na dini yake.

Halafu tunashangaa kwanini hatuendelei?

Na wewe ni zungu nini! Lakini uozo unaanzaje kama siyo katika 'misconception' au 'deliberate distortion of truth?' Na ili kusiwepo 'misconception' lazima watu fulani waelemishwe ili hatimaye wasilete huo uozo. Hivyo, mjadala si tu kujadili uozo lakini pia 'root causes' za huo uozo. Na hii inaweza kuwa kwenye 'mind-set' ya mtu.

Kuna watu wanapika mambo halafu baadaye wanakuja kuyatumia kufanya huo uozo. Hawa sitawaacha, nitawaelemisha. Mfano, kwa huyu njemba ninayejibu hoja yake, yeye alichukizwa na Pengo kukemea uozo na anataka kutuaminisha kwamba hakuwa na basis yeyote ya kukemea uozo/ufisadi na mimi na wengine tunajaribu kusema kuwa huyu njemba yuko wrong?

Unajua tena kuna namna nyingi za kuwasafisha mafisadi wa Tanzania. Na tunaona jinsi gani baadhi ya watu wanafanya juu-chini kudhoofisha hoja kuwa kuna ufisadi na inabidi tuupige vita kwa nguvu zetu zote.
 
  • Asema Katoliki haliandai mgombea Urais mwaka 2010.
  • Adai anayeogopa waraka wa Kanisa ni Fisadi.

Pengo usitufanye wajinga;Taasisi yake ya TEC, ilipoandaa haya yafuatayo walikuwa na lengo gani??????

Nanukuu

"...Tusiruhusu nchi hii mwanya kwa dini yoyote ile kushika hatamu za uongozi na Kanisa kubaki nyuma na kuwa halina sauti.

Mambo haya yalijitokeza kwa awamu ya pili. Awamu ya tatu tuliweza kudhibiti na kurudisha heshima kidogo lakini Awamu ya nne udhalilishaji wa Kanisaumekuwa kwa kiwango kikubwa..." Mwisho wa kunukuu,

Source; Waraka wa TEC, Siri ya kiutumishi, Mpango wa kuhamasisha Huduma ya Kiuchungaji katika Jamii Kuelekea uchagusi mkuu 2010.

Huu ni UNAFIKI mkubwa, na uchochezi wa hatari katika jamii. Pengo aache kuzunguka mbuyu, aeleze wazi nia yao ya kutaka kuibatiza Tanzania.
 
Hata leo hii Dr. Salim Ahamed Salim na Mzee Sinde Warioba wanaonekana kukiri kwamba hali si shwari ingawa hawakusema direct kama Pengo. Indeed we seem to be flying off course to our predestined land of El Dorado!
 
Mkuu ni kweli kuna separation ya politics na religious matters. Sina hakika kama maana yako ya Church and State, ina maana Mosque yenyewe haiwi separated na state matters, which in many cases it may seems so.

Lakini where do you draw that line. Mambo ya dini yanaishia wapi na ya siasa yanaingia wapi, ukiangalia kwa undani utaona kuwa ni mstari ambao umechorwa hewani tu. Sioni ubaya kwa kiongozi wa msikiti au kanisa kusema hatutaki viongozi wabovu, mtu akiwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa, diwani, mbunge,waziri au rais anaongoza watu wote bila kujali yeye ni mwanadini au la. Kwa hiyo kama uongozi wake haufai unamwathiri moja kwa moja hata mtu wa dini. Kama serikali inalinda na kupalilia maovu, misikiti na makanisa yatakuwa yanafanya kazi bure, yaani kufinidhs amorals wengine wanafanya tofauti. Wakati wao misikitini na makanisani wanapreach honesty, itakuwa ni upuuzi kama watachekelea ufisadi.

Makamba most of the time amekuwa akiquote Qoran na Biblia anapokuwa kwenye kazi za siasa. Alipokuwa RC hata alikuwa anakwenda misikitini kama RC, kumbuka mwembechai au pale kwa mtoro wakati wanachapana bakora ndani. Mbona yeye hakuwahi kukosolewa kuwa anachanganya siasa na dini?

Are we being hypocritical, or is our system hypocritical? Why should politicians mix politics and religion and why shouldn't clergymen mix religion and politics. Inawezekana Pengo hajui kama dini na siasa haviwezi kuchanganywa?
Nadhani watu wengi wasichokielewa ni kwamba hauwezi kuwaongoza nakuwajenga watu wawe imara kiroho hili khali kimwili wamedhoofika. Miminadhani kutenganisha dini na siasa ni kutoruhusu masuara ya kisiasa kuamuliwa na kuongozwa kwa misingi ya dini.
 
Tumuulize kardinali yeye ufisadi huko kanisani kwake kashaacha?...vipi watoto wetu wako salama huko...maana mapadre duniani kote..wana-sodomize watoto???

Shughulikia uchafu kanisani kwako kwanza kabla hujaanza kupiga kelele we mbuzi...
 
Nchi kuoza ni fact, hata vipofu wanafahamu swali ni what is the solution??? Binafsi naamini mpaka yafanyike mapinduzi ya kijeshi kama Uganda na Rwanda ndio tuweza kuikoa nchi yetu
 
Kwa sababu hiyo, waumini wake waachane na siasa na wasishiriki uchaguzi any more?? OK
Waumini wanaruhusiwa kisheria kuwa kwenye chama chochote cha siasa kikatiba...sasa pengo kama anataka siasa aanzishe "christian party" asajili halafu aombe kura kwamba chma chake hakita vumilia mafisadi tutampa na kumpima..

In BTWN apunguze ufisadi kanisani kwake...mapadre wanalawiti watoto mayatima, shule na hospitali za kanisa zinatoa huduma kwa bei za kuruka pamoja na kwamba wanapata ruzuku kutoka serikalini (hela za waislamu na wakristo) damn!

Huyu pengo mpuuzi sana
 
Nafikiri sasa serekali imefika wakati wa kumshuhulikia huyu Polycarp Kardinali Pengo,ni lazima achunge sana hii sio serekali ya kuchezea ipo kihalali na imechaguliwa kwa ridhaa ya wananchi kwa ushindi mkubwa.
 
the so called separation ni ngumu. labda tuanze kwanza kubadili mifumo ya uapishaji viongozi, kwanini wanaapishwa kwa biblia na quoran? je haimaanishi kuwa kila aapaye anakubaliana na kilichoandikwa katika vitabu husika na kwamba hatakiwi kuviweka mbali? naamini Pengi yu sahihi na azungumzizye separation hiyo aota ndoto za mchana. naomba kukosolewa
 
Nafikiri sasa serekali imefika wakati wa kumshuhulikia huyu Polycarp Kardinali Pengo,ni lazima achunge sana hii sio serekali ya kuchezea ipo kihalali na imechaguliwa kwa ridhaa ya wananchi kwa ushindi mkubwa.
Acha kubwabwaja wewe....serikali ipo kwa ridhaa ipi ya wananchi?,,tatizo hamtaki kuambiwa ukweli....utashughlikiwa wewe na siyo Pengo
 
Hahahhahahah sasa KATOLIKI YOTE KIMYA , kisa mkatoliki mwenzao. Huu unafiki wa wakatoliki acha tu tunyooshwe. Pu.mbavu kabisa
 
Back
Top Bottom