Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Hivi mtu kama huyu ambae anataka kuwashauri waTanzania juu ya kuendelea kuichagua CCM tumuelewe vipi ?
Ni kweli wakatoliki wanaridhika na uongozi wa CCM ,Pengo kwa maoni yake ya kujipendekeza anaelekea kuigawa nchi maana unaposema utawashauri wakatoliki waipigie CCM kura tayari utakuwa umeshaitenga jamii ,Je asilimia kubwa ya kura wanazo wakatoliki , Pengo awache kujipendekeza kwa kuona yeye ndie anaewaelekeza watanzania wamchague nani ,huku ni kuwapotosha WaTanzania . Aidha ajijulishe kuwa yeye ni Mwanachama wa CCM hapo haitawezekana kumuingilia katika maamuzi yake ,hivi Mtanzania huyu anaweza kuwapigia makelele mafisadi ? Hivi Pengo anamwambia nini Kikwete juu ya mafisadi ?
WaTanzania washauriwe kuchagua Chama kile ambacho kitawaletea maendeleo bila ya kushawishiwa wampigie nani kura ? WaTanzania washauriwe kuwa tayari kulinda kura zao zisiibiwe ,WaTanzania wapime na kuona utawala wa CCM umefikia wapi na unaelekea wapi.Pengo anaomba rushwa maana ukimwambia mtu tuzungumze vizuri ,kwa Tanzania ya leo inaeleweka umekusudia nini.
______________________________________________________
Pengo alisema hayo mbele ya Rais Kikwete, marais wastaafu wa awamu ya pili na tatu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa Jaji Mkuu, Augustine Ramadhan na Spika wa Bunge, Samuel Sitta.
Alitoa mfano kuwa ikiwa Rais Kikwete atahitaji kura za urais kutoka kwa waumini wa Katoliki nchini ni dhahiri kwamba atazungumza naye (Pengo) vizuri ili awashawishi waumini wa kanisa hilo wamchague.
``Ikiwa hivyo, mimi nitazungumza nao na kuwaambia, huyu ndiye wa kumchagua, utapata kura nyingi za Wakatoliki, lakini kama hazikuwa zinaridhia Watanzania kwa ujumla, kesho na keshokutwa hali itakuwa ngumu nchini,`` alisema
_________________________________________________
Yaani Pengo atawadanganya wakatoliki na kuwambia CCM ni Chama kizuri kipeni kura .
Kasome utumbo wake kamili hapa ,hawa ndio waliotuambia kama ni chaguo la Mungu ,sasa wanasema maneno yao ni ya unabii :-
http://ippmedia.com/ipp/nipashe/2009/02/23/132181.html
Ni kweli wakatoliki wanaridhika na uongozi wa CCM ,Pengo kwa maoni yake ya kujipendekeza anaelekea kuigawa nchi maana unaposema utawashauri wakatoliki waipigie CCM kura tayari utakuwa umeshaitenga jamii ,Je asilimia kubwa ya kura wanazo wakatoliki , Pengo awache kujipendekeza kwa kuona yeye ndie anaewaelekeza watanzania wamchague nani ,huku ni kuwapotosha WaTanzania . Aidha ajijulishe kuwa yeye ni Mwanachama wa CCM hapo haitawezekana kumuingilia katika maamuzi yake ,hivi Mtanzania huyu anaweza kuwapigia makelele mafisadi ? Hivi Pengo anamwambia nini Kikwete juu ya mafisadi ?
WaTanzania washauriwe kuchagua Chama kile ambacho kitawaletea maendeleo bila ya kushawishiwa wampigie nani kura ? WaTanzania washauriwe kuwa tayari kulinda kura zao zisiibiwe ,WaTanzania wapime na kuona utawala wa CCM umefikia wapi na unaelekea wapi.Pengo anaomba rushwa maana ukimwambia mtu tuzungumze vizuri ,kwa Tanzania ya leo inaeleweka umekusudia nini.
______________________________________________________
Pengo alisema hayo mbele ya Rais Kikwete, marais wastaafu wa awamu ya pili na tatu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa Jaji Mkuu, Augustine Ramadhan na Spika wa Bunge, Samuel Sitta.
Alitoa mfano kuwa ikiwa Rais Kikwete atahitaji kura za urais kutoka kwa waumini wa Katoliki nchini ni dhahiri kwamba atazungumza naye (Pengo) vizuri ili awashawishi waumini wa kanisa hilo wamchague.
``Ikiwa hivyo, mimi nitazungumza nao na kuwaambia, huyu ndiye wa kumchagua, utapata kura nyingi za Wakatoliki, lakini kama hazikuwa zinaridhia Watanzania kwa ujumla, kesho na keshokutwa hali itakuwa ngumu nchini,`` alisema
_________________________________________________
Yaani Pengo atawadanganya wakatoliki na kuwambia CCM ni Chama kizuri kipeni kura .
Kasome utumbo wake kamili hapa ,hawa ndio waliotuambia kama ni chaguo la Mungu ,sasa wanasema maneno yao ni ya unabii :-
http://ippmedia.com/ipp/nipashe/2009/02/23/132181.html