minda
JF-Expert Member
- Oct 2, 2009
- 1,068
- 65
Gazeti la mwananchi.
Geofrey Nyang'oro
ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo , amewaasa viongozi wa kanisa hilo kuepuka mafundisho ya upotoshwaji yenye lengo la kujitafutia sifa akidai mafundisho ya aina hiyo ni hatari kwa ustawi wa kanisa la Mungu.
Askofu huyo alitoa kauli hiyo kwenye ibada ya misa takatifu ya upadirisho wa mapadri watatu wa kanisa hilo iliyofanyika jana katika Parokia ya Kristu Mfalme ya Tabata jijini Dar es Salaam.
Alisema katika karne hii, wapo watu wanaoweza kufikiria kutumia nafasi walizonazo kufundisha neno la Mungu kwa lengo la kutafuta umaarufu miongoni mwa jamii na kwamba vitendo hivyo ni hatari kwa ustawi wa kanisa.
Kauli hiyo aliitoa wakati Watanzania wa sasa wanashuhudia kuibuka kwa madhehebu na wahubiri wa aina mbalimbali ambapo baadhi yao wanajitangaza kuwa wana uwezo wa kufanya miujiza ya kutisha ikiwemo ya kufufua wafu, upako katika biashara, kuondoa mikosi, kurudisha ndoa, kufaulu mitihani , na hata kufanikiwa katika masuala ya kutafuta kazi.
Baadhi ya viongozi wa madhehebu hayo wanaomba kwa kupayukapayuka kinyume cha maagizo ya Mungu kupitia kwenye Biblia Takatifu ambamo ameagiza sala zote zifanywe kwa unyenyekevu na hata kwa siri kwa kuwa yeye anaona yote ya siri...
Pengo alisema viongozi wa kanisa wawe tayari kuteketea kama chumvi inayoyeyuka kwa ajili ya kunogesha radha ya chakula.
Maaskofu, Mapadiri na Mashemasi, ninyi mnapaswa kuwa chumvi na si mawe, chumvi ni kiungo kinachotumiwa katika kunogesha radha ya chakula, kiungo hiki hukubali kuteketea na kupoteza hata uhalisia wake ingawa uwepo wake huonekana kwenye ladha ya chakula,alisema Pengo.
KWA HIYO?: suala langu wana jf ni hapo pekundu, je hawa viongozi wa dini za kisasa sio sawa na waganga wa kienyeji tunaowasikia kila siku uswazini? hivi ni kweli wana uwezo wa kutenda mambo hayo?