Pengo amtolea uvivu Kikwete

Kuna MwanaJF mmoja aliwahikuwasema humu Jamvi kuwa Ni Bora Kikwete akiwa nje ya nchi kuliko akiwa ndani ya nchi anatoa maneno ya Kukejeli, Kuudhi na ya kijingajinga anaropoka hovyo kama vile hakuwahi kumaliza Shule. Nimeamini kuwa Kikwete akiwa nje ya Tanzania, Watanzania wanakuwa na uafadhali kuliko akiwa ndani.


Kwanini tusimtoeni kwa Nguvu ya Umma, ni kitu gani kinashindikana? Watanzania wenzangu muda wa kuchukuwa hatua umefika mambo mengine sio ya kuyafumbia Macho lazima tusimame na nchi yetu
 
Kwanini Pengo ilimuuma ile kauli ya Kikwete? au ni mmoja wa washukiwa.

lakini siku hizo hana uzito wowote kulinganisha na Wakati za Nyerere.
kilichomuuma ni usaliti wa JK wa kukataa kutaja majina ya wahusika. Pole kwa kushinda njaa sheikh ubwabwa.
 
Kwanini Pengo ilimuuma ile kauli ya Kikwete? au ni mmoja wa washukiwa.

lakini siku hizo hana uzito wowote kulinganisha na Wakati za Nyerere.


mkuu vp mmefikia wapi huko libya? endelea kutupa taharifa kutoka kwenye eneo la mapigano
 
''Kuna walioandaa wagombea wao, na taasisi zao ambazo ni taasis za heshima zikagharamia uchapishaji wa majarida, wakaandaa semina, makongamano, na kufanya kampeni kwenye kila ibada. Lakini hawakufanikiwa kupenyeza mtu wao kwenye nafasi walioitaka, sasa hii tunayoishuhudia ni kuchanganyikiwa kwao na ndio maana nilieleza kule Dodoma wakati wa sherehe za kuzaliwa CCM kuwa, kuna baadhi yetu bado wamenuna na matokeo ya uchaguzi. Kwa bahati mbaya hata wakiendelea kununa, rais wa nchi hii ataendelea kuwa yule yule, hakuna mwingine, na shida zao watakuja kuniambia mimi hawana pakwenda.''

Huu ndio ujasiri wake Jakaya Mrisho Kikwete rais wa awamu ya nne, Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Mipasho kama kawa, maneno gani gani hayo ya kusema prezidaa jamani
 
naam mkuu, hapo umenena...,
Ngoja tuwasikie watasema nn khs hiyo kauli ya Pengo...!,
its ma hope that, na wao watakuja na kauli thabiti, safi na komavu ya kuijenga nchi yetu....!
hapo kwenye red na doubt sana...! sasa hivi nadhani watakuwa wanatoka mapovu kwa sana tu.....kauli yao itakuwa ya kumtete tu Sultan Kikwete ! hakuna jipya!
 
Kwanini Pengo ilimuuma ile kauli ya Kikwete?

lakini siku hizo hana uzito wowote kulinganisha na Wakati za Nyerere.

Pengo kapata uaskofu mwaka 1984 yaani mwaka mmoja kabla Nyerere haja-retire.

Na hakusikika wakati kwa sababu jimbo alilokuwa nalo hata leo waandishi hawajikiti huko wakihadaika kudhani ukimsikia askofu wa Dar basi umemsikia mkubwa wao hapa Tanzania!

Pengo ameikamata Dar mwaka 1992 miaka mitatu kabla ya Mwinyi ku-resign.

Acha chuki zako kwa Nyerere ambaye asingetaifisha shule za dini ungeishia kwenye alifa, be, che nk
 
Mipasho kama kawa, maneno gani gani hayo ya kusema prezidaa jamani

Bahati nzuri, watanzania walipiga kura kumchagua rais m k w e re, maneno ya kuudhi na kukera hasa walionuna ni jadi, natamani kuingia ndani ya moyo wa pengo kila akimuona JK, maana uwekezaji walioufanya kwa Slaa ni mkubwa sana.
 
wakuu tunaomba sana tupunguze jazba kwani thread hii inaelekea kuongeza hisia za kidini , tunaipenda Tanzania tusingependa hisia hizi ziongezeke sana.


pls wana JF tusiingize udini kama hoja zijengwe kwenye utendaji na si udini wakuu

 
JF tusiingize udini kama hoja zijengwe kwenye utendaji na si udini wakuu

Ni vigumu sana kumuongelea Pengo na kuiacha dini yake, acheni tu tujadili halafu Tanzania si hakuna udini bali ni JK ndio anayeuongelea?
 
hakuna mnafiki kama kikwete...yaani yule baba sijui nimfananishe na nini...mtu gani wa vugu vugu? ..
 
Kule Pwani kuna neno linajulikana sana "Kusiganisha" Maana yake ni kuzunguka nyuma na kukoroga mahusiano mazuri kati ya marafiki huku ukijidai "rafiki" wa mwathirika wa "kusiganishwa". Hii ni tabia iliyopo kwa wanafiki wote. Mara nyingi mkakati huu korofi wa kichawi hutumika wakati unapojua adui yako kakuzidi kila kitu. Iliyobaki ni kumuharibia tu kwa jamii na marafiki.

JK ni bingwa wa mtindo huu wa "kusiganisha". Hebu sikia hiki kichefuchefu " siyo nyie ni makanisa madogo madogo".

Tabia hii ndiyo iliyotumika kuanzisha mtandao wa "kusiganisha watz" ili kupata urahisi 2005. Mh Salim Ahmed Salim alisiganishwa na wananchi vivyo Sumaye na wengineo wote walioingia kwenye ligi ya Urais.

Lowasa anamfahamu vizuri rafiki yake huyo na sasa "anasiganishwa"

Rostam baada ya kusaidia kuupata Urais sasa "anasiganishwa" na rafiki aliyeshirikiana na kushauriana waibe toka BOT ili washinde urais.

Pole watz mmeingia choo cha kike kwa kuchagua Rais "Msiganishaji"

Dawa kuu ni hii aliyoitumia Pengo. Straight shooting on the head!! endelea pengo!!!!
 
Bahati nzuri, watanzania walipiga kura kumchagua rais m k w e re, maneno ya kuudhi na kukera hasa walionuna ni jadi, natamani kuingia ndani ya moyo wa pengo kila akimuona JK, maana uwekezaji walioufanya kwa Slaa ni mkubwa sana.
Kama wana jf tunataka kusaidiana kimawazo tuache uswahili kama huu, toa a reasoned analysis badala ya kuwa mswahili. kwamba pengo amenuna is rubbish!
 
Bahati nzuri, watanzania walipiga kura kumchagua rais m k w e re, maneno ya kuudhi na kukera hasa walionuna ni jadi, natamani kuingia ndani ya moyo wa pengo kila akimuona JK, maana uwekezaji walioufanya kwa Slaa ni mkubwa sana.
Kama ni kweli ni sawa LAKINI HAKUIBA benki ili kushinda
 
. kwamba pengo amenuna is rubbish!

Hakuna chochote kinacho msumbua huyo mnafiki zaidi ya kununa, nchi hii imepitia mambo mangapi makubwa kabla kanisa lake halijaingia kwenye kampeni za Slaa lakini hakuwahi kuongea kitu lakini tokea huyo padri mwenzake ameshindwa uchaguzi basi ni nongwa tu kila kukicha. Narudia tena Pengo na wenzake wa TEC na wengine wooote waliokuwa wapiga kampeni wa Slaa wamenuna tu ndio kinacho wasumbua, na salamu zao wataendelea kunua hadi 2015 labda wakaze buti kwenye hizo mbinu zao za kupindua serikali halali.
 
Ni vigumu sana kumuongelea Pengo na kuiacha dini yake, acheni tu tujadili halafu Tanzania si hakuna udini bali ni JK ndio anayeuongelea?
punguzeni jazba kwani udini hauna maana sana mwisho ni mapambano yasiyo na tija kwani siku hizi mtu akiambiwa kitu watu wanatafsiri udini .....tatizo nini ? rais ajae anatoka visiwa vya Tumbatu sasa nyinyi mbona mnauana
 
Nimeipenda sana kauli ya Pengo. rais ameapa kuilinda katiba na katiba inasema watu wote ni sawa mbele ya sheria. sasa unawajua wahalifu wa madawa halafu huchukui hatua maana yake umesaliti kiapo chako. anataka kuwapaka matope wakristo halafa anajifanya anawaficha wasiaibike. unafiki!
 
Kama mtandao ni mkubwa utakua unawahusu wakubwa wa serikali ndio maana hawatajwi. Hivi sheria hapa tanzania zimewekwa kwaajili ya wanyonge tu?kwasababu angekua mnyonge asingetajwa tu bali angekamatwa kwa virungu juu serikali yafaakuliangalia hili kwa umakini wa hali ya juu
 
Nawaomba wana jf ambao ni waumini wa the so called makanisa madogo muwashauri viongozi wenu watoe statement wambane jk ataje hao wahalifu wa madawa na awapeleke mahakamani. kwa jinsi jk alivyo mnafiki amehamisha tuhuma kutoka makanisa makubwa baada ya kubanwa sasa anayaonea makanisa madogo kuwatwisha mzigo wa tuhuma ili waonekane ni magenge ya wahalifu. tuhuma ni nzito lazima aombe radhi au awataje
 
Back
Top Bottom