Elections 2010 Pendekezo: JamiiForums iandae ajenda yake ya Uchaguzi Mkuu

Sheba

JF-Expert Member
May 14, 2009
211
97
Waungwana,

Imekuwa ni ada sasa kwa wanasiasa na hasa katika Bunge letu tukufu kusisitiza aidha umuhimu wa kujipanga au kusema kuwa sasa wanajipanga au wamejipanga. Tatizo kubwa ni kuwa, toka msisitizo wa kujipanga umeanza hakuna anayezungumzia kujipangua.

Lakini, kwa tuliopitia JKT hata wale wachambuzi wa mpira tunafahamu kuwa wakati fulani kikosi kinalazimika kujipangua ikiwa ni mbinu ya kujipanga upya, hususan pale ambapo mpango wa kwanza umejikuta umekwama. Ni maoni yangu kuwa, dhana hii inaweza pia kuwa na mantiki katika siasa na utawala.

Ndani ya Jukwaa hili tumejipanga kila kukicha kulaumu, kudhihaki na kukosoa bila mafanikio, je si wakati wa Jukwaa hili kujipangua kwa kujitokeza na vipaumbele vya Agenda ya Jamii Forum ya Uchaguzi Mkuu wa 2010 na kuinadi kwa wagombea na vyama kuisimamia na kuiweka katika ilani zao? Hatutakuwa tumetenda haki zaidi sisi wasomi kwa taifa letu?

Kama hivyo ndivyo, uchaguzi mkuu na chaguzi za ndani ya vyama vinabisha hodi mbele yetu.................. ni maeneo gani kumi ya vipaumbele tunadhani yanatakiwa kupanguliwa au tunapaswa kama taifa kujipangua? Maeneo haya yanaweza kuandaliwa kama Agenda ya Jamii Forum ya Uchaguzi Mkuu 2010 na kushawishi wagombea na vyama kubeba agenda hizo katika ilani zao.

Tusipofanya hivyo, ipo hatari ya Jukwaa letu hili tukufu kutumika kujadili watu na kuchafuana badala ya 'issues' za msingi na haja za wananchi wetu.

Napendekeza Mwanakijiji na moderator waratibu mchakato huu kwa kuanzia.


Nawasilisha waungwana!
 
Mkuu mi nadhani maoni yako ni mazuri ila kwa upande wangu, wanaotakiwa kujipangua ni chama tawala kwasababu hapa kwetu kinaonekana kuwa chama dola. Ilani zake zilizoandaliwa na wasomi hazitekelezeki, na sababu haijulikani kama ni waalimu wa chuo kikuu wanaandaa mtihani halafu wasahihishaji ni waalimu wa shule za msingi, ama ni sababu ya wadanganyika wengi kuwa hawajitambui na hivyo kuwafanya watawala kutumia uzoefu tu kuburuza nchi.

Hivyo wapinzani wajipange kutetea

(1) katiba inayoendana na mfumo wa vyama vingi.
(2) Tume huru ya uchaguzi
(3)Uundwaji wa mfumo uliyo wazi wa kulinda mali za serikali zisetumike kukampenia chama chochote.
(3)Watumishi wa serikali mfano wa wakuu wa mikoa, wilaya kutojihusisha na harakati zozote za chama cha siasa. Na kama watafanya hivyo basi wapoteze mamlaka yao kikatiba na kubakia kuwa wapembe wa mkuu fulani wa chama cha siasa.

Kila mwenye kutimiza vigezo vya kupiga kura awe ameandikishwa kabla ya siku ya uchaguzi.

NB. Kama masuala muhimu hayazingatiwi ni afadhali uchaguzi kuahirishwa hata kwa baazi ya miaka kuliko kuwa wabeba muhuri wa kuihalalisha ccm kutawala milele.
 
Mkuu mi nadhani maoni yako ni mazuri ila kwa upande wangu, wanaotakiwa kujipangua ni chama tawala kwasababu hapa kwetu kinaonekana kuwa chama dola. Ilani zake zilizoandaliwa na wasomi hazitekelezeki, na sababu haijulikani kama ni waalimu wa chuo kikuu wanaandaa mtihani halafu wasahihishaji ni waalimu wa shule za msingi, ama ni sababu ya wadanganyika wengi kuwa hawajitambui na hivyo kuwafanya watawala kutumia uzoefu tu kuburuza nchi.
Hivyo wapinzani wajipange kutetea
(1) katiba inayoendana na mfumo wa vyama vingi.
(2) Tume huru ya uchaguzi
(3)Uundwaji wa mfumo uliyo wazi wa kulinda mali za serikali zisetumike kukampenia chama chochote.
(3)Watumishi wa serikali mfano wa wakuu wa mikoa, wilaya kutojihusisha na harakati zozote za chama cha siasa. Na kama watafanya hivyo basi wapoteze mamlaka yao kikatiba na kubakia kuwa wapembe wa mkuu fulani wa chama cha siasa.
(1)Kila mwenye kutimiza vigezo vya kupiga kura awe ameandikishwa kabla ya siku ya uchaguzi.
NB. Kama masuala muhimu hayazingatiwi ni afadhali uchaguzi kuahirishwa hata kwa baazi ya miaka kuliko kuwa wabeba muhuri wa kuihalalisha ccm kutawala milele.

Kiby,Asante kwa maoni yako. Nakubaliana kimsingi na hoja ulizotoa hapo chini. Wasiwasi wangu ni kuwa agenda nzima ya JF ya Uchaguzi Mkuu 2010 itakosa maana ikiwa itajikita kuunga upinzania dhidi ya Chama tawala. Maono yangu katika hili ni kuwa na agenda mtambuka na za kitaifa......... kama ambavyo umeziainisha vizuri. Kwa vyovyote vile wadau humu ndani wataleta agenda nyingine zinazohitaji kuzingatiwa. Mwishoni tunaweza kujikuta na agenda mia. lakini zingine zikiwa zinashahabiana na zingine si za msingi. Tukifika hapo tunaweza kuzipunguza na kuzioanisha na kisha na kuwa vipaumbele kumi. Tukifika hapo, sasa tunaanza kuzinadi na kushawishi vyama kuvibeba. Unaonaje? Hatutakuwa tumesaidia taifa badala ya lawama tu?
 
Naunga mkono hoja.Ni vema JF tukaandaa agenda ya uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.Tuchangie kwa pamoja agenda hizo.This is a very good idea.
 
Mkuu Sheba,nadhani ingependeza kama ungeanza kwa kuonyesha njia! Hoja yako ina mshiko lakini wewe mtoa hoja ungeleta agenda ambazo unafikiri zingefaa kuwa-adopted na JF kama ajenda za uchaguzi mkuu na wengine nasi tukaumiza kichwa kuleta dondoo zetu.
 
Agenda namba moja kuwe na mabadiliko ya Katiba ya nchi hii ambayo ndio msingi wa matatizo mengi sana. Na ijadiliwe na watanzania wote si wanasiasa wachache tu. Tunahitaji kukubaliana kuhusu hili.
 
Back
Top Bottom