Baija Bolobi
JF-Expert Member
- Feb 25, 2009
- 1,093
- 1,726
Leo siku nzima nimefanya kazi ya kutafuta maoni kwa watawala wetu na baadhi ya majaji wazoefu, walio kazini na wastaafu. Maoni ya wengi katika niliongea nao ni kama hivi ifuatavyo:
-Mchezo mchafu umefanyika na kwa bahati mbaya ukavuja kabla ya wakati. CCM kwa kushindwa kujizuia wakaagiza DC wa Arusha afunge ofisi ya mbunge hata kabla hukumu haijatangazwa. Hapa JF hukumu hiyo ilikuwa ni gumzo.
-Mtakumbuka Nape alianza kampeini mjini Arusha mpaka wakili wa Lema akaiomba mahakama imuite aje kuieleza ni kwa nini anadhani uchaguzi utarudiwa. Ukweli ni kuwa tayari wakati huo mazungumzo yalikuwa yameanza na Jaji aliishawapa early indicators za kubatilisha ubunge wa Lema.
-Majaji na wanasheria wamechukia sana kuona mwenzao amewasaliti kwa kuonyesha jinsi wanavyoingiliwa na wanasiasa. Wanakubali hili ni tatizo lakini linawaaibisha majaji kuliko wanasiasa, maana kimsingi, hawalazimishwi bali wanaombwa kupendelea. Uhuru wa mahakama haupaswi kulindwa na dola bali na mahakama yenyewe kwa kukataa kutumiwa.
-Majaji wanakubali kuwa jaji Rwakibalira ni "M-serikali". Huu ni msemo maarufu katika korido za mahakama unaowatambulisha majaji ama wanaojikomba kwa wanasiasa, au majaji walio katika idara nyeti iliyochafuka sana (TISS). Hali kadhali Jaji Mujulizi aliyekataliwa na Lema ni "M-serikali" pia.
-Watu mashuhuri, wanasheria na baadhi ya majaji wanashauri kuwa ni MUHIMU hukumu hii ikatiwe rufaa ili kuondoa aibu kwa judiciary nzima.
-Wanasiasa makini ndani ya CCM wanaona rufaa ni njia nzuri ya kuiondolea aibu CCM na aibu hiyo aibebe Jaji Rwakibalira peke yake. Mmoja amekwenda mbali na kusema, mahakama ya rufaa ikimpa haki LEMA, CCM impongeze Lema kama njia ya kujiosha mbele ya wapiga na kuandaa mazingira ya awali ya uchaguzi wa 2015.
-Mwisho, kama Jaji alivuta mshiko, hakuvuta mshiko, alishinikizwa, alijipendekeza, ibaki ni aibu yake badala ya kuwa aibu ya judiciary au dola inayodaiwa kuhonga ili kubatilisha ubunge wa Lema. Aliyefanya hivyo kama yupo, alifanya hivyo kwa matashi yake mwenyewe na si kwa niaba ya dola. Kwa bahati mbaya, Salva wa Ikulu yuko implicated na kuwa aliongea na Jaji mara kadhaa kwa kutumia lugha ya kikwao. Makarani na madereva wa jaji wamethibitisha tuhuma hizi.
-Mchezo mchafu umefanyika na kwa bahati mbaya ukavuja kabla ya wakati. CCM kwa kushindwa kujizuia wakaagiza DC wa Arusha afunge ofisi ya mbunge hata kabla hukumu haijatangazwa. Hapa JF hukumu hiyo ilikuwa ni gumzo.
-Mtakumbuka Nape alianza kampeini mjini Arusha mpaka wakili wa Lema akaiomba mahakama imuite aje kuieleza ni kwa nini anadhani uchaguzi utarudiwa. Ukweli ni kuwa tayari wakati huo mazungumzo yalikuwa yameanza na Jaji aliishawapa early indicators za kubatilisha ubunge wa Lema.
-Majaji na wanasheria wamechukia sana kuona mwenzao amewasaliti kwa kuonyesha jinsi wanavyoingiliwa na wanasiasa. Wanakubali hili ni tatizo lakini linawaaibisha majaji kuliko wanasiasa, maana kimsingi, hawalazimishwi bali wanaombwa kupendelea. Uhuru wa mahakama haupaswi kulindwa na dola bali na mahakama yenyewe kwa kukataa kutumiwa.
-Majaji wanakubali kuwa jaji Rwakibalira ni "M-serikali". Huu ni msemo maarufu katika korido za mahakama unaowatambulisha majaji ama wanaojikomba kwa wanasiasa, au majaji walio katika idara nyeti iliyochafuka sana (TISS). Hali kadhali Jaji Mujulizi aliyekataliwa na Lema ni "M-serikali" pia.
-Watu mashuhuri, wanasheria na baadhi ya majaji wanashauri kuwa ni MUHIMU hukumu hii ikatiwe rufaa ili kuondoa aibu kwa judiciary nzima.
-Wanasiasa makini ndani ya CCM wanaona rufaa ni njia nzuri ya kuiondolea aibu CCM na aibu hiyo aibebe Jaji Rwakibalira peke yake. Mmoja amekwenda mbali na kusema, mahakama ya rufaa ikimpa haki LEMA, CCM impongeze Lema kama njia ya kujiosha mbele ya wapiga na kuandaa mazingira ya awali ya uchaguzi wa 2015.
-Mwisho, kama Jaji alivuta mshiko, hakuvuta mshiko, alishinikizwa, alijipendekeza, ibaki ni aibu yake badala ya kuwa aibu ya judiciary au dola inayodaiwa kuhonga ili kubatilisha ubunge wa Lema. Aliyefanya hivyo kama yupo, alifanya hivyo kwa matashi yake mwenyewe na si kwa niaba ya dola. Kwa bahati mbaya, Salva wa Ikulu yuko implicated na kuwa aliongea na Jaji mara kadhaa kwa kutumia lugha ya kikwao. Makarani na madereva wa jaji wamethibitisha tuhuma hizi.