Elections 2010 PEMBETATU YA USHINDI: Kuelekea kuyatikisa Malango ya CCM

Mzee Mwnakijiji, tafadhali tuambie hayo mambo matatu au manne ambayo Chadema wanatakiwa kuyafanya ili ushindi uwe ni lazima! Fanya hivyo kwa ukombozi wa Taifa zima. Please!
 
Kati ya watu ambao nna imani nao katika Taifa hili kwa umakini, Dr Slaa ni mmoja wao.
Wakati CHADEMA wanafanya uzinduzi wa kampeni pale Jangwani, waliongea vitu vingi halafu wakasema baadhi ya vitu wataendelea kuvitoa jinsi kampeni zinavyoendelea.

Naami moja ya vitu watavyoongea kipindi hiki lazima iwe counterpunch kwa ushindi wa KO dhidi ya CCM.
CHADEMA ni chama chenye watu makini sana.

I'm eagerly waiting for the final two rounds...
 
"Ninaamini kuna mambo kama matatu au manne ambayo Chadema wakiamua kweli kuyafanya siyo tu kwamba watashika hatamu ya uongozi lakini wataonekana kwa haki kabisa wamestahili kufanya hivyo na hakuna mtu atakayeweza kuamua vinginevyo".

Nimesoma makala yako yote na ninakiri kuwa ni nzuri na umeeleza kwa urefu ni nini hasa kinatakiwa kifanyike ili Dr. Slaa na timu yake wapate ushindi. Ila kwenye nukuu ya maneno yako kwenye makala hiyo umetaja mambo kama matatu au manne ambayo Chadema wanatakiwa kufanya ili kupata ushindi. Sijayaona mambo haya yakielezewa kwa urefu. Au umeamua kuwapa Chadema wenyewe?
 
Ni waraka mzuri sana lazima waonyeshe umoja zaidi kuliko kipindi chochote kilicho salia wameona wananchi wanavyotaka kubadili uongozi siku kumi na mbili zilizobaki wanatakiwa kushambulia kama nyuki kila pande na kila kona
Mungu Ibariki Tanzania
 
Big up mzee mwanakijiji. Naamini wazee wenzio kijijini wako na sisi. Ushindi ni muhimu kwa future ya nchi yetu. Mungu atusaidie ili kila mpango usiotakia mema nchi yetu ubatilishwe. Kama Mungu alivyobatilisha shauri la Ahithopheli ndivyo ninavyoomba abatilishe shauri la wezi wa kura na mashauri mengine yanayopangwa kuhujumu fair elections. Mungu ni Mungu wa haki, na haki itatawala. Haleluyaaaaa
 
PEMBETATU YA USHINDI: KUELEKEA MABADILIKO
Na. M. M. Mwanakijiji

Njia ya Dr. Slaa kuingia Ikulu inapitia moja kwa moja katika migongo na mabega ya Zitto Kabwe na Freeman Mbowe. Na pamoja nayo inapitia katika pembetatu ya watu hawa watatu kuongoza shambulizi la mwisho katika wiki hizi mbili zilizosalia kabla ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010.

Kama kuna kiongozi ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema anayeamini kuwa ipo nafasi nyingine ya kugombania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kushinda nje ya nafasi hii ya 2010 basi mtu huyo anajidanganya. Kama wapo wanachama na mashabiki ambao wanaamini kuwa wakati wa kugombea Urais na kushinda siyo sasa na hivyo wasubiri hadi 2015 au 2010 watu hao vile vile wanajizuga wao wenyewe. Endapo viongozi, wanachama na mashabiki wa Chama hicho maarufu cha upinzani nchini hawatafanya yote wanayopaswa na wanayoweza kufanya katika wiki hizi mbili za mwisho za kampeni basi ndoto ya kuupata Urais itatoweka kama umande wa alfajiri.

Nalazimika kuandika hili kama kuwatia shime wale wote ambao wanataka kweli mabadiliko nchini kupitia chama hicho kuondoa vizuizi vyote vya kihisia na kiakili na kutumia nafasi hii ya kihistoria kuweza kuigombania ipasavyo nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano.

Mkakati wowote wa kutaka kupata wabunge wengi zaidi na siyo kupata Urais wa Jamhuri ya Muungano ni mkakati uliokubali nafasi ya kudumu ya upinzani. Kama viongozi na mashabiki wa Chadema wanapita na kuhamisha watu wawachague wabunge ili kuwe na wabunge zaidi Bungeni ili kwa kufanya hivyo waanze kusikilizwa zaidi na CCM basi watu hao wanakuwa wamekubali nafasi ya upinzani na hawako tayari kuwa watawala. Mkakati wa kupata wabunge wengi ni mkakati mzuri isipokuwa pale tu unapoendana na lengo zima la kutaka nafasi ya urais vile vile.

Kumbe washauri wa chadema mko hai bado humu JF OK SIO MBAYA kazaneni sana.halafu huyu ZITTO kabwe kutompaisha hewani mgombea wake inaleta picha gani?me naona HAMKUBALI HIVYO HAFAI KUWA RAISI au kale kaWARAKA kalikotolewa kamemkolea hadi yeye teh teh teh fanyeni uchunguzi asije akawa anawauza oh oh
 
Quality.. mbona umejisahau tena.. bado.. nitawasiliana nawe usidhani nimesahau; tunaongeza tracks nyingine n.k Tracks zote zitakuwa tayari before the end of this week. stay put.
Good news!! Nilikuwa nina hamu ya kusikia hilo. Pia hizo track tunaomba uziweke kwenye ile website yako ambako huwa unapost audio music.
 
MwanaVilagge wala sintashangaa kwakua tunakoelekea sasa hivi ukweli unaanza kujulikana hata kwa viongozi wa dini kwamba wanataka mtu safi sio chama safi! Hata waziri mkuu mstaafu wa awamu ya tatu kasema watanzania chagueni mtu safi na makini atakayewaletea maendeleo sasa hapa analengwa nani? watanzania wanataka change na sasa naona change is coming!! God Bless Tanzania!! USIUZE KURA YAKO UTAJUTA!
 
Mkuu Mkjj. kwa mtazamo wangu mimi nadhani huu ni wakati muafaka wa kuwa na mkakati wa kuzuia mianya yote ya kuiba kura otherwise CCM hawana chao kuanzia kusini mpaka kaskazini, magharibi mpaka mashariki.. Nilitegemea labda bagamoyo JK angeshinda kumbe hata huko kabanwa mbavu ile mbaya!!! Nasikia muungwana walimuibia ng'ombe wake miezi kama mitatu iliyopita na mpaka leo hii hajawapata na wezi hawajulikani!!!!!!!!
 
Kiukweli tunahitaji mabadiliko tena kwa haraka. Lakini bahati mbaya iliyopo hakuna anayefaa kutuletea haya mabadiliko kwa sasa. Si wapinzani wala chama Tawala.

Nahisi una matatizo na humu JF sio mahali pako ni bora ukahamia kwa Michuzi.
 
Back
Top Bottom