MaxShimba
JF-Expert Member
- Apr 11, 2008
- 35,772
- 4,054
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imesema kisiwa cha Pemba kinaongoza kwa umasikini wa kipato Zanzibar.
Hayo yalisemwa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha, Uchumi, Mipango na Maendeleo, Omar Yussuf Mzee, wakati akijibu swali la Mwakilishi wa Viti Maalumu, Viwe Khamis Abdalah, aliyetaka kujua Serikali imechukua hatua zipi kukabiliana na umasikini unaoukabili ukanda wa Mashariki wa Micheweni.
Mzee alisema, kuna hatua zimechukuliwa na Serikali kukabiliana na tatizo hilo lililoko Micheweni, Pemba.
Alizitaja hatua hizo kuwa ni pamoja na kuwasiliana na jumuiya za kimataifa kufanya utafiti na kuanzishwa kijiji cha milenia Micheweni.
Alisema, baada ya kukubaliwa maombi hayo zilianzishwa programu zikiwemo za kupeleka maji safi na salama na umwagiliaji maji katika bonde la Sawinga na kuanzisha miradi ya ufugaji.
Mzee alifafanua zaidi kwamba utekelezaji wa malengo ya maendeleo ya milenia kwa kiasi kikubwa utasaidia kupunguza umasikini kwa wananchi wa Micheweni.
Alisema, katika malengo ya kutoa taarifa kwa wananchi kimeanzishwa Kituo cha Redio Jamii Micheweni.
Aliongeza kuwa redio hiyo inafanya kazi ya kutoa taarifa kwa wananchi zinazohusu kilimo na ufugaji.
HabariLeo | Pemba yaongoza kwa umasikini Zanzibar
Hayo yalisemwa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha, Uchumi, Mipango na Maendeleo, Omar Yussuf Mzee, wakati akijibu swali la Mwakilishi wa Viti Maalumu, Viwe Khamis Abdalah, aliyetaka kujua Serikali imechukua hatua zipi kukabiliana na umasikini unaoukabili ukanda wa Mashariki wa Micheweni.
Mzee alisema, kuna hatua zimechukuliwa na Serikali kukabiliana na tatizo hilo lililoko Micheweni, Pemba.
Alizitaja hatua hizo kuwa ni pamoja na kuwasiliana na jumuiya za kimataifa kufanya utafiti na kuanzishwa kijiji cha milenia Micheweni.
Alisema, baada ya kukubaliwa maombi hayo zilianzishwa programu zikiwemo za kupeleka maji safi na salama na umwagiliaji maji katika bonde la Sawinga na kuanzisha miradi ya ufugaji.
Mzee alifafanua zaidi kwamba utekelezaji wa malengo ya maendeleo ya milenia kwa kiasi kikubwa utasaidia kupunguza umasikini kwa wananchi wa Micheweni.
Alisema, katika malengo ya kutoa taarifa kwa wananchi kimeanzishwa Kituo cha Redio Jamii Micheweni.
Aliongeza kuwa redio hiyo inafanya kazi ya kutoa taarifa kwa wananchi zinazohusu kilimo na ufugaji.
HabariLeo | Pemba yaongoza kwa umasikini Zanzibar