Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Baraza Kuu la Makanisa ya Pentekoste nchini limeibua upya hoja ya Kadhi kwa kuitaka Serikali kutopeleka muswada Bungeni kuhusu masuala ya dini moja kwa kuwa huo ni uvunjaji wa Ibara ya 19 ya Katiba ambayo inasema kuwa Serikali haina dini ila watu wake wana dini. Badala yake wawaachie Waislamu wenyewe kushughulikia suala hilo kivyao na kimsingi hawana tatizo na uanzishwaji wa mahakama hizo isipokuwa hawaafiki Serikali kujishughulisha na suala hilo kama ilivyoanza kujionyesha wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipounda kamati kushirikiana na waislamu kuanzisha mchakato wa kuunda mahakama ya Kadhi. (Source: Majira, tr 02/11/2009).