Paul Chizzi amuumbua Mwakyembe

Kila mtu anapokuwa amebanwa lazima atafute utetezi hata kama ni wa uongo, hapo Chizi anatapatapa tu ukweli unabaki palepale, ATCL kulikuwa na ubadhirifu mkubwa saana, Miaka Ishirini iliyopita kulikuwa na ndege kubwa zaidi ya tano,Leo hii shirika hoi, Loh tumechoka kudanganywaa!!!
 
Usiwe unakurupuka kuchangia kitu usichofahamu! Unajua ni nani wameifikisha hapo ATCL au unajiropokea?
Kila mtu anapokuwa amebanwa lazima atafute utetezi hata kama ni wa uongo, hapo Chizi anatapatapa tu ukweli unabaki palepale, ATCL kulikuwa na ubadhirifu mkubwa saana, Miaka Ishirini iliyopita kulikuwa na ndege kubwa zaidi ya tano,Leo hii shirika hoi, Loh tumechoka kudanganywaa!!!
 
Aliyekuwa mtendaji mkuu wa ATCL ameibuka na kusema kwamba Dr Mwakyembe alidanganya umma kutokana taarifa alizopewa kuwa ni za uongo na zisizokuwa na ukweli wowote.

Kwa mfano uniform ziligharimu dola 18,000 tu na sio dola 50,000 kama alivyosema mwakiembe, Bwana Chizi alisema pia tatizo ni kwamba kuna watu hawajui chochote kuhusu sekta ya anga lakini wanajidanganya kuwa wanajua mbele ya umma.

Chanzo: The Guardian on Sunday


Mwakyembe hajakurupuka kuna jambo kaliona na ndiyo maana kachukua maamuzi mwacheni afanye kazi yake watanzania tumezoea kutokuona uwajibikaji. siku zote mfa maji haishi kutapatapa big up Mwakyembe nakutakia kazi njema kwani mpigania haki hakosi maadui usijali tuko pamoja.
 
Mkuu mwalimu wako wa kiingereza ana laana, yaani maelezo yanajitosheleza na hadi gharama ya unit imeelezwa bado hujaelewa na unabisha...

Ninashauri sio lazima kuchangia mada kama hujaelewa, haya mambo ya aviation ni ya kitaalam, nyie mliotokea shule za kata kaeni pembeni wataalam walumbane.
Nenda jukwaa la lugha kajifunze kiingereza au hire a translator

unasema sisi tuliosoma shule za kata tukae pembeni wakati mnapojadili mambo ya kitaalam!sasa wakati mnakusanya kodi mbona huwa hamtuambii sisi tuliosoma shule za kata tukae pembeni ili ninyi wa st meriz,st john,feza,consolata,marian,mulipe kodi kwa raha zenyu?next time acha dharau dogo,mngekuwa hamna njaa msinge ng'ang'ania kukaa ktk ofisi za uma na kukwiba malizetu tuliosoma shule za kata,instead mngelikuwa wafanyabiashara kama kina mengi na bakhresa.
 
Tusiwakatishe tamaa watendaji wazuri huyo Chizi inawezekana akawa kama jina lake,
 
umaige tu huu, hakuna lolote kama ameonewa angeenda kumuonesha hizo document sasa katimuliwa ndio analalama magazetini, amken watz wizi mpaka lini?
 
Si ajabu anaitwa chizi....utatumiaje dola 18,000 kushona nguo ambazo zaweza shonwa kwa batiki za hapa hapa na hata Millioni 2 isifike.....
chizi wewe

je unajua ni yunifomu ngapi na kwa staffs wangapi??

unajua bei ya batiki wewe kima?
 
Hata kama hivyo ndivyo alivyosema, bado kuna tatizo kubwa sana hapo.

USD 18,000 X 1500=Tsh. 27,000,000 kwa unifomu moja! Milioni 27 kweli kwa nguo moja?

Hajaweza bado kuniweka kwenye kundi la watu wa kumuamini na sana sana ananiongezea machungu tu ya PAYE niliyokatwa mwezi uiopita.

Suala la jina ni suala la msingi sana hata wazazi wa huyu jamaa wanalijua tatizo la mtoto wao na ndio maana hawakumwita michosho,John au James bali wakamwita "chizi" kama kaonewa aende kwenye vyombo vya sheria adai haki yake yy sio mwanasiasa ya nini kuanza ngonjera na kuuza magazeti.
 
Chizi anafahamu sana anachokifanya, ameharibu akubali, aondoke akapumzike.Mwakyembe amezungumzia gharama ya uniforms ni $49,900, tena amesama wazi. lakini chizi kwa usanii wake na huyo mwandishi wanazungumzia bei ya uniform ni $18,000. bei na gharama ni vitu viwili tofauti, sasa sitegemei CEO apindishe tafsiri kati ya bei na gharama.
hao precision air walinunua uniform kwa bei kati ya $ 200 na $ 600 kwa kila mmoja. ATCL hata kama wangenunua kwa bai kama ya precision air, gharama ya ATCL kwa uniform zao bado ni juu , kwani wao (ATCL) walituma wafanyakazi wao kwenda kununua na walitumia siku 45 huko, so maisha yao huko yanaingia ktk gharama ya uniform.je precision air nao walituma watu china kwa siku 45?, kama wangefanya hivyo, si precision air ingeshakufa?. chizi ni mtu mzima ameharibu akubali. baadhi ya waandishi wetu nao ni waandishi uchwara, wana ripoti bila kuchunguza na kutafsiri wanacho ripoti

chizi ni chizi tu
 
Likirushwa jiwe kichakani unayesikia anapiga kelele ujue limempata, huyu Chizi Waziri altengua uteuzi wake lakini kuna maofisa wengine wa ATCL waliosimamishwa na hatujawasikia wakibwabwaja kwenye vyobo vya habari. Huyu jamaa cizi kweli! Mtu unapewa kukaimu hata hujathibitishwa unafikiria umekuwa wadhifa wa kudumu?
 
Ka -ka -ka -ama jamaa aliiba mbona hajfikiswa kwa pilato. wezi wakiiba vijijini huwa wanafukuzwa tu vijijni au hushitakiwa na kuhukumiwa kwa mujibu wa sheria. Mwakyembe anasema ushahidi wa maandishi upo what is he waiting for men, wasitukoroge hawa watu men!
 
Mwakyembe ni mpenda misifa, msiomjua nawapa pole.

Tindikali umesema kweli kabisa. Na hana muda mrefu atalikoroga big time.
Kusafiri kwa treni, kwenda railway station saa sita za usiku as if hakuna watu wa chini yako (au huna imani nao?) Yote hii ni kujipamba ktk media.
Naamini kabisa anao uwezo wa kufuatilia mambo lkn inaonekana yupo ki media zaidi. Wapo wengi tu wanapiga kazi zao bila ya kutembea na camera man muda wote.
Cheap popularity sometimes is very expensive!
 
ni kweli kuna wizi karibu kila pahala katika nchi hii, lakini lazima tufike mahali tujue kwamba hata wanaotoa hizi tuhuma nao ni wale wale na kwa maana hiyo wakati tunapoamua kujiunga katika kumtuhumu mtu yeyote eti kwa sababu waziri ama pengine CAG kasema, ni vizuri tujitahidi kutojiapiza. Binafsi siko katika nafasi yoyote inayoniwezesha kufanya ufisadi wowote wa kuweza kujadirika hapa lakini ninayoyasikia (TUHUMA) kutoka kwa CAG, kamati za bunge etc juu ya ufisadi wa mahali ninapofanyia kazi yananipa shaka kuamini kama kweli hata yanayotamkwa na mwakyembe ni ya kweli.
 
Back
Top Bottom