Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,766
- 894
Imeelezwa kuwa siasa nchini inaendeshwa katika mfumo ambao ni wakupakana matope baina ya kundi fulani la viongozi kwa lengo la kuchafua sifa za viongozi wa kundi jingine ili kulifanya lionekane baya miongoni mwa wanajamii hata kama lina viongozi wenye sifa nzuri za za uongozi.
Hayo yalisemwa na Paroko wa Parokia ya Sinza, Padri Cathbeth Maganga wakati wa mahubiri yake katika Ibada ya misa ya Dominika ya matawi iliyofanyika Parokiani hapo, Padri Maganga alisema kuwa baadhi ya watu wasio na nia njema wamekuwa wakiwazushia wenzao mambo yasiyo ya kweli kwa lengo la kuharibia sifa nzuri walizonazo jambo ambalo husababisha taifa kuwa na viongozi wenye hila mbaya na ufisadi mkubwa. kuwabebesha sifa mbaya watu wema hakipishani na kitendo kilichofanywa na Wayaudi cha kumtesa Yesu Kiristo mpaka kufa msalabani, pamoja na kwamba kauli ya Padri Maganga haikutaja ni kundi gani la viongozi au chama kinachofanya mchezo huo, lakini kauli hiyo imekuwa ni jibu baada ya Katibu Mkuu wa Chadema, DK Willibrod Slaa kutaja orodha mpya ya majina ya watu aliyodaiwa kuwa ni mafisadi.
SOURCE: MWANANCHI APRILI 20, 2011
Hayo yalisemwa na Paroko wa Parokia ya Sinza, Padri Cathbeth Maganga wakati wa mahubiri yake katika Ibada ya misa ya Dominika ya matawi iliyofanyika Parokiani hapo, Padri Maganga alisema kuwa baadhi ya watu wasio na nia njema wamekuwa wakiwazushia wenzao mambo yasiyo ya kweli kwa lengo la kuharibia sifa nzuri walizonazo jambo ambalo husababisha taifa kuwa na viongozi wenye hila mbaya na ufisadi mkubwa. kuwabebesha sifa mbaya watu wema hakipishani na kitendo kilichofanywa na Wayaudi cha kumtesa Yesu Kiristo mpaka kufa msalabani, pamoja na kwamba kauli ya Padri Maganga haikutaja ni kundi gani la viongozi au chama kinachofanya mchezo huo, lakini kauli hiyo imekuwa ni jibu baada ya Katibu Mkuu wa Chadema, DK Willibrod Slaa kutaja orodha mpya ya majina ya watu aliyodaiwa kuwa ni mafisadi.
SOURCE: MWANANCHI APRILI 20, 2011