Papademos ashinda kura ya kuwa na imani; maandamano kufanyika leo.

Che-lee

JF-Expert Member
Jun 10, 2011
318
88
Serikali mpya ya umoja wa kitaifa nchini Ugiriki imeshinda kura ya kuwa na imani bungeni jana Jumatano.

Waziri mkuu mpya, Lucas Papademos, anaweza sasa kuanza kutekeleza hatua za kubana matumizi ambazo haizipendwi katika juhudi za kuzuwia nchi hiyo kushindwa kulipa madeni yake.

Mpango mpya wa kuongeza kodi pamoja na upunguzaji wa matumizi unahitajika ili kuweza kufuzu kupata fungu jingine la mkopo wa dharura kutoka umoja wa Ulaya na shirika la fedha la kimataifa, IMF.

Euro* bilioni* nane* zinahitajika* kulipa* madeni* ambayo yanahitajika* kulipwa* mwezi* ujao. Licha* ya* ushindi* bila matatizo** serikali* mpya** ilioupata* bungeni,* maelfu* ya Wagiriki* wanatarajiwa* kuingia* mitaani* leo* kuandamana. Maandamano* hayo* ni* kwa* ajili* ya* kumbukumbu* ya vuguvugu* la* maandamano* ya* wanafunzi* wa* Ugiriki yaliyosababisha* umwagikaji* wa* damu* mwaka* 1973, wakati* watu* walipoupindua* utawala* wa* kijeshi* nchini humo.
 
Back
Top Bottom