Papa ateua maaskofu wasaidizi wawili Dar

SubiriJibu

JF-Expert Member
Jun 26, 2009
1,803
1,863
Hata miezi miwili haijapita tangu kuhamishwa kwa askofu Methodius Kilaini kwenda kuwa askofu msaidizi wa Bukoba, Papa Benedict XVI amewateua mapadri wawili kuwa maaskofu wasaidizi wa jimbo kuu la D’Salaam. Wawili hao ni Padri Salutaris Libena na Padri Eusebius Nzigilwa.

Wakati askofu Kilaini alikuwa na Phd. Sasa jimbo limempata professa kwani mmoja wa hao watakaokuwa maaskofu wasaidizi ni Professa (Padri) Salutaris Libena ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa na ni mhadhiri kwenye seminari kuu ya Kipalapala iliyoko nje ya mji wa Tabora. Vilevile alikuwa mkurugenzi wa kiroho au spiritual director wa seminari hiyo. Yeye (Libena) alikuwa ni padri wa jimbo la Mahenge kule kwa askofu Ndorobho nadhani na nimzaliwa wa Itete.

Mwenzake Padri Eusebius Nzigilwa ni padri wa jimbo la D’Salaam na ni mzaliwa wa Mwanza na amewahi kuwa rector wa seminary ndogo ya Visiga iliyoko mkoa wa Pwani karibu na Kongowe.

Hivyo jimbo kuu la D’Salaam sasa linakuwa na maaskofu watatu yaani Kadinali Polycarp Pengo na hawa wasaidizi wake wawili. Aliondoka mmoja yaani Kilaini sasa wameletwa wawili kwa mpigo.

Chanzo: RADIO TUMAINI
 
Hata miezi miwili haijapita tangu kuhamishwa kwa askofu Methodius Kilaini kwenda kuwa askofu msaidizi wa Bukoba, Papa Benedict XVI amewateua mapadri wawili kuwa maaskofu wasaidizi wa jimbo kuu la D’Salaam. Wawili hao ni Padri Salutaris Libena na Padri Eusebius Nzigilwa.

Wakati askofu Kilaini alikuwa na Phd. Sasa jimbo limempata professa kwani mmoja wa hao watakaokuwa maaskofu wasaidizi ni Professa (Padri) Salutaris Libena ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa na ni mhadhiri kwenye seminari kuu ya Kipalapala iliyoko nje ya mji wa Tabora. Vilevile alikuwa mkurugenzi wa kiroho au spiritual director wa seminari hiyo. Yeye (Libena) alikuwa ni padri wa jimbo la Mahenge kule kwa askofu Ndorobho nadhani na nimzaliwa wa Itete.

Mwenzake Padri Eusebius Nzigilwa ni padri wa jimbo la D’Salaam na ni mzaliwa wa Mwanza na amewahi kuwa rector wa seminary ndogo ya Visiga iliyoko mkoa wa Pwani karibu na Kongowe.

Hivyo jimbo kuu la D’Salaam sasa linakuwa na maaskofu watatu yaani Kadinali Polycarp Pengo na hawa wasaidizi wake wawili. Aliondoka mmoja yaani Kilaini sasa wameletwa wawili kwa mpigo.

Chanzo: RADIO TUMAINI

Fr. Nzigilwa pia alikuwa ni paroko msaidizi Makongo majuu hadi anateuliwa na ni mwanafunzi wa masters degree(Education) pale mlimani!
 
Fr. Nzigilwa pia alikuwa ni paroko msaidizi Makongo majuu hadi anateuliwa na ni mwanafunzi wa masters degree(Education) pale mlimani!

Nakumbuka wakati tunajadili suala la Askofu Kilaini kwenda Bk hapa JF, wengi walihoji iweje apelekwe Bukoba amako si hata jimbo kuu kwa qualification na experience aliyonayo? Tukapata majibu kwamba kanisa katoliki aliendeshwi kisiasa/kidunia zaidi. Wana taratibu zao na kanuni zao kwamba kondoo wa bwana wanaweza kuchungwa popote pale, na mchungaji hachagui wapi yalipo malisho!

Hili limejithibitisha kwa kummteua Fr. Nzigilwa ambaye ndio kwanza anaitafuta Masters degree! Wangapi wenye elimu zaidi ya hiyo wameachwa?
 
Jamani qualification za mapadre tofauti sana na serikalini,acheni kuanza kulinganisha usomi wa mapadre eti ndiyo wanastahili kuwa kwenye jimbo kuu.
 
Tuna wakaribisha sana hao maaskofu wapya,tuwaombee Amani,afya njema,na maadili mema waweze kuifanya vema kazi ya Bwana.

Tutakukumbuka sana Askofu Kiliani,ulifanya mambo mengi mazuri,Mungu Akubariki
 
All in all naomba nipongeze sana kanisa Katoliki kwa kuwaweka viongozi wa kiroho wasomi kwa kweli wanaongoza na nadhani wanasimamia sana suala la elimu ya juu ambayo ni zaidi pia ya theolojia; hii inawapa ufahamu zaidi na upeo mkubwa zaidi katika kuwachunga Kondoo wa bwana!

Jina la Bwana libarikiwe!
 
Fr. Nzigilwa pia alikuwa ni paroko msaidizi Makongo majuu hadi anateuliwa na ni mwanafunzi wa masters degree(Education) pale mlimani!

Interesting. Yaani askofu bado yuko shule. Sasa atafanya uaskofu au itabidi aahirishe hiyo masters degree. Mapadre hawaeleweki, msishangae akaamriwa na mkuu wake kuwa aache shule, maana nasikia huko kwa wakatoliki ukishakuwa padre unasarenda akili na utashi wako wote kwa mkuu wako!
 
Interesting. Yaani askofu bado yuko shule. Sasa atafanya uaskofu au itabidi aahirishe hiyo masters degree. Mapadre hawaeleweki, msishangae akaamriwa na mkuu wake kuwa aache shule, maana nasikia huko kwa wakatoliki ukishakuwa padre unasarenda akili na utashi wako wote kwa mkuu wako!


Nonsensical!
 
Interesting. Yaani askofu bado yuko shule. Sasa atafanya uaskofu au itabidi aahirishe hiyo masters degree. Mapadre hawaeleweki, msishangae akaamriwa na mkuu wake kuwa aache shule, maana nasikia huko kwa wakatoliki ukishakuwa padre unasarenda akili na utashi wako wote kwa mkuu wako!
uongozi wa kanisa katoliki wanawaencourage watumishi waende shule,Askofu huyo ataendelea na masters na kazi ya utumishi kama kawaida.
 
Interesting. Yaani askofu bado yuko shule. Sasa atafanya uaskofu au itabidi aahirishe hiyo masters degree. Mapadre hawaeleweki, msishangae akaamriwa na mkuu wake kuwa aache shule, maana nasikia huko kwa wakatoliki ukishakuwa padre unasarenda akili na utashi wako wote kwa mkuu wako!


MTU B

hapo umekosea sio kweli kabisa, ni kwamba wana miongozo yao ukiona padre anasoma akaacha ujue labda kazidiwa na shughuli za kikazi, ninao marafiki wengi mapadre wako free tena saana tu,
 
Hongera sana kwa mapadre hao, na Mungu awaongoze vema katika kazi yao ya kuchunga kondoo!
 
Nawapongeza wachungaji wapya na kuwatakia kila la kheri....naamini papa kuna move anayoikusudia maana kama kawaida, Vatican haina papara kwenye mambo yake.Pengine safu ya uongozi wa kanisa la Tanzania inaapangiliwa upya, taratibu taratibu. Who knows!
Ila yote ni heri tu!
 
Interesting. Yaani askofu bado yuko shule. Sasa atafanya uaskofu au itabidi aahirishe hiyo masters degree. Mapadre hawaeleweki, msishangae akaamriwa na mkuu wake kuwa aache shule, maana nasikia huko kwa wakatoliki ukishakuwa padre unasarenda akili na utashi wako wote kwa mkuu wako!


`Utopian` ideas!!!!!!! usipende kusikia na kukonkludi wangapi wako kazini na wanasoma?:rolleyes::rolleyes::rolleyes:
 
Nawapongeza wachungaji wapya na kuwatakia kila la kheri....naamini papa kuna move anayoikusudia maana kama kawaida, Vatican haina papara kwenye mambo yake.Pengine safu ya uongozi wa kanisa la Tanzania inaapangiliwa upya, taratibu taratibu. Who knows!
Ila yote ni heri tu!


nakubaliana na wewe kwani hawa wajamaa wanavyofanya kazi hawaendi papara hata kidogo,,,,nakumbuka hata Kilaini kwenda Bukoba kuna kitu kwani hicho kituo chake cha kazi nasikia mambo hayaendi kabisa, kuna kanisa limeanzwa kujengwa tangu kipindi kile alipokufa kadinali Rugambwa mpaka leo halija kamilika kapelekwa kwa maksudi kabisa huko
 
mavuno ni mengi lakini watenda kazi ni wachache. Ingefaa kila jimbo liwe na askofu msaidizi
 
Wow hongera Padre Libena...you deserve it....MUNGU ambariki sana na ampe mafanikio mema katika kazi zake mpya.
 
Back
Top Bottom