Wakuu JF,
Nimeletewa gazeti moja la Kanisa Katoliki linaloitwa MWENGE nikisisitizwa nisome makala ya padri mmoja anaitwa Baptiste Tunda. Sina kawaida ya kusoma gazeti hilo lakini nikamuheshimu aliyeniletea. Niliposoma makala hiyo sikuamini niliyosoma ambapo huyu padri bila kumung'unya maneno amebeza ule ushindi wa kishindo wa CCM iliyoshindwa kwa kishindo kupambana na ufisadi. Inaelekea gazeti lilitoka mwezi wa nne (Toleo. Na. 851) na huku kwetu likachelewa kufika. Atakayeona toleo la sasa (Toleo. Na. 852) asisitie kutumwagia jamvini.
Faidi utamu wa maka hiyo na wale wasioamini haraka scan yake imeweza kupatikana kama kiambatanisho:
$ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $:
Toka mwaka jana tulianza kusherehekea Jubile ya Mmisionari na Mtume wa kimataifa, yaani Paulo. Mtume Paulo hakuwa kati ya mitume 12 wa Yesu kama alivyowaita yeye mwenyewe. Mtume Paulo aliitwa kivyake kwa njia ya kuanguka barabarani na farasi wake kule Dmascus na ndipo akasikia sauti ya Bwana wake anayemdhulumu.
Mtakatifu mtume na mmisionari huyu shujaa anajulikana sana kwa misimamo yake mbalimbali. Kwa sababu ya kuanzisha makanisa mengi kama ya Wakorinto, Waefeso, anajulikana kwa barua zake kwa makanisa hayo. Ninaweza kusema kwamba wongofu wa Paulo ulikuwa ni wa kishindo, na hivi kazi zake zilikuwa za kishindo pamoja na kifo chake kilikuwa cha kishindo.
KARAMA YA UNYENYEKEVU:
Baada ya kukutana na Bwana hakutaka kusikia upuuzi mwingine tena. Hata hivyo Paulo alijifunza karama ya unyenyekevu na akabaini kuwa sisi sote ni wadhambi. Kwa njia hiyo kusiwepo majivuno ya aina yoyote ile. Paulo anasema kwamba, Aliyesimama ajiangalie asije akaanguka.
Tangu uchaguzi wa mwaka 2005 Chama Cha Mapinduzi kimekuwa na semi nyingi na majigambo mengi sana ya kwamba CCM ilipata ushindi wa kishindo. Sina uhakika huo, lakini ninachojua ni kwamba CCM ilishinda na ikaunda serikali ya awamu hii ya nne. Ushindi wa kishindo aliupata Yesu siku ya ufufuko, umeleta ushindi kwetu waamini wote wanaomfuata. Yesu ni mshindi na mtawala, ni mfalme wa wafalme hakika.
Sasa ufalme wa Yesu na ushindi wake umemuondoa mwanadamu katika utumwa mbalimbali. Ushindi wa Yesu umeleta uhai mpya, matumaini, na jinsi ya kuishi upya.
Sasa ushindi wa CCM umeleta nini kwa maisha ya watanzania? Kauli mbiu ilikuwa Maisha Bora kwa Kila Mtanzania, watu tumebaki kuhoji, je, yamefika au bado?
Ushindi wa kishindo maana yake nini? Unapothubutu kusema ushindi wa kishindo, wakati rushwa imekithiri kila kona, umaskini umeongezeka, ajira kwa vijana Hakuna, utapeli umezidi, mikataba ya ovyo inaendelea kusainiwa, viongozi wa juu kujihusisha na ufisadi wa mabilioni ya pesa za wananchi, tena walalahoi, makabwela. Huu ushindi wa kishindo unamaanisha nini?
SERIKALI YA AWAMU YA NNE:
Kilichonikera ni hasa baada ya miaka 3 na uchaguzi kupita, bado wana-CCM wanaimba wimbo wa Ushindi wa Kishindo majukwaani. Imefika mahala sasa tuanze kuiona hali halis na kuikubali. Je, tunaweza kusema serikali ya awamu ya nne imeshinda? Imeshinda nini?
Mimi kwa Mawazo yangu ningetaka kuutafakari ushindi wa wapinzani. Maana wamefanikiwa kuufukua ufisadi na wizi wa mabilioni ya pesa za wananchi maskini katika sekta mbalimbali, EPA ya Benki Kuu, Richmond, Kiwira n.k.
Na hadi sasa ni kesi tu zinafunguliwa, hakuana aliyehukumiwa kwa kisingizo cha kwamba tunataka ushahidi, ni ushahidi gani unatafutwa?
Watuhumiwa wengi wa ufisadi bado wana nyadhifa zao kama wabunge na kadhalika.
Wenzetu Ulaya na Amerika, mtu akituhumiwa mara moja anasimamishwa kazi bila kujali cheo ama uhusiano wake na rais na mara moja anaanza kuchunguzwa. Lakini sisi hapa kwetu Kisiwa cha Amami kama ipo, watu ni vinganganizi kweli. Unasikia wanasema Siondoki, sijiudhuru NGOO!! Tena kwa kiburi na jeuri. Hii ni hatari kubwa sana kwa taifa letu.
Je, kwa mtindo huu utasema serikali imeshinda au imehindwa? Kwa mtindo huu serikali inapoteza imani kila siku kwa wananchi wake hata kama hawajasema tumepoteza imani nawe serikali ya awamu ya nne.
Lakini tuache unafiki na kujifanya umbuni wa kuficha kichwa mchangani na kiwiliwili chote nje na kujidanganya kuwa hawakuoni. Yesu alikuwa anatumia usemi kuwa Mwenye masikio na asikie.
Kuendelea kujidanganya mmeshinda kwa kishindo si kweli. Kuwafanya watanzania wote ni wajinga kwamba hawajui kinachoendelea katika nchi yetu ni kujidanganya wenyewe kwa wenyewe.
Nenda sokoni, nenda kilabuni, ndani ya basi, ndani ta teksi, sikiliza waumini wakitoka kwenye ibada zao, waalimu, wafanyakazi wa ngazi za chini, mapolisi, manesi na watumishi wengine utabainisha mwenyewe.
Yesu anasema Ukwelu utawaweka huru.
Itaendelea tolea lijalo.
$ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $:
Nimeletewa gazeti moja la Kanisa Katoliki linaloitwa MWENGE nikisisitizwa nisome makala ya padri mmoja anaitwa Baptiste Tunda. Sina kawaida ya kusoma gazeti hilo lakini nikamuheshimu aliyeniletea. Niliposoma makala hiyo sikuamini niliyosoma ambapo huyu padri bila kumung'unya maneno amebeza ule ushindi wa kishindo wa CCM iliyoshindwa kwa kishindo kupambana na ufisadi. Inaelekea gazeti lilitoka mwezi wa nne (Toleo. Na. 851) na huku kwetu likachelewa kufika. Atakayeona toleo la sasa (Toleo. Na. 852) asisitie kutumwagia jamvini.
Faidi utamu wa maka hiyo na wale wasioamini haraka scan yake imeweza kupatikana kama kiambatanisho:
$ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $:
Toka mwaka jana tulianza kusherehekea Jubile ya Mmisionari na Mtume wa kimataifa, yaani Paulo. Mtume Paulo hakuwa kati ya mitume 12 wa Yesu kama alivyowaita yeye mwenyewe. Mtume Paulo aliitwa kivyake kwa njia ya kuanguka barabarani na farasi wake kule Dmascus na ndipo akasikia sauti ya Bwana wake anayemdhulumu.
Mtakatifu mtume na mmisionari huyu shujaa anajulikana sana kwa misimamo yake mbalimbali. Kwa sababu ya kuanzisha makanisa mengi kama ya Wakorinto, Waefeso, anajulikana kwa barua zake kwa makanisa hayo. Ninaweza kusema kwamba wongofu wa Paulo ulikuwa ni wa kishindo, na hivi kazi zake zilikuwa za kishindo pamoja na kifo chake kilikuwa cha kishindo.
KARAMA YA UNYENYEKEVU:
Baada ya kukutana na Bwana hakutaka kusikia upuuzi mwingine tena. Hata hivyo Paulo alijifunza karama ya unyenyekevu na akabaini kuwa sisi sote ni wadhambi. Kwa njia hiyo kusiwepo majivuno ya aina yoyote ile. Paulo anasema kwamba, Aliyesimama ajiangalie asije akaanguka.
Tangu uchaguzi wa mwaka 2005 Chama Cha Mapinduzi kimekuwa na semi nyingi na majigambo mengi sana ya kwamba CCM ilipata ushindi wa kishindo. Sina uhakika huo, lakini ninachojua ni kwamba CCM ilishinda na ikaunda serikali ya awamu hii ya nne. Ushindi wa kishindo aliupata Yesu siku ya ufufuko, umeleta ushindi kwetu waamini wote wanaomfuata. Yesu ni mshindi na mtawala, ni mfalme wa wafalme hakika.
Sasa ufalme wa Yesu na ushindi wake umemuondoa mwanadamu katika utumwa mbalimbali. Ushindi wa Yesu umeleta uhai mpya, matumaini, na jinsi ya kuishi upya.
Sasa ushindi wa CCM umeleta nini kwa maisha ya watanzania? Kauli mbiu ilikuwa Maisha Bora kwa Kila Mtanzania, watu tumebaki kuhoji, je, yamefika au bado?
Ushindi wa kishindo maana yake nini? Unapothubutu kusema ushindi wa kishindo, wakati rushwa imekithiri kila kona, umaskini umeongezeka, ajira kwa vijana Hakuna, utapeli umezidi, mikataba ya ovyo inaendelea kusainiwa, viongozi wa juu kujihusisha na ufisadi wa mabilioni ya pesa za wananchi, tena walalahoi, makabwela. Huu ushindi wa kishindo unamaanisha nini?
SERIKALI YA AWAMU YA NNE:
Kilichonikera ni hasa baada ya miaka 3 na uchaguzi kupita, bado wana-CCM wanaimba wimbo wa Ushindi wa Kishindo majukwaani. Imefika mahala sasa tuanze kuiona hali halis na kuikubali. Je, tunaweza kusema serikali ya awamu ya nne imeshinda? Imeshinda nini?
Mimi kwa Mawazo yangu ningetaka kuutafakari ushindi wa wapinzani. Maana wamefanikiwa kuufukua ufisadi na wizi wa mabilioni ya pesa za wananchi maskini katika sekta mbalimbali, EPA ya Benki Kuu, Richmond, Kiwira n.k.
Na hadi sasa ni kesi tu zinafunguliwa, hakuana aliyehukumiwa kwa kisingizo cha kwamba tunataka ushahidi, ni ushahidi gani unatafutwa?
Watuhumiwa wengi wa ufisadi bado wana nyadhifa zao kama wabunge na kadhalika.
Wenzetu Ulaya na Amerika, mtu akituhumiwa mara moja anasimamishwa kazi bila kujali cheo ama uhusiano wake na rais na mara moja anaanza kuchunguzwa. Lakini sisi hapa kwetu Kisiwa cha Amami kama ipo, watu ni vinganganizi kweli. Unasikia wanasema Siondoki, sijiudhuru NGOO!! Tena kwa kiburi na jeuri. Hii ni hatari kubwa sana kwa taifa letu.
Je, kwa mtindo huu utasema serikali imeshinda au imehindwa? Kwa mtindo huu serikali inapoteza imani kila siku kwa wananchi wake hata kama hawajasema tumepoteza imani nawe serikali ya awamu ya nne.
Lakini tuache unafiki na kujifanya umbuni wa kuficha kichwa mchangani na kiwiliwili chote nje na kujidanganya kuwa hawakuoni. Yesu alikuwa anatumia usemi kuwa Mwenye masikio na asikie.
Kuendelea kujidanganya mmeshinda kwa kishindo si kweli. Kuwafanya watanzania wote ni wajinga kwamba hawajui kinachoendelea katika nchi yetu ni kujidanganya wenyewe kwa wenyewe.
Nenda sokoni, nenda kilabuni, ndani ya basi, ndani ta teksi, sikiliza waumini wakitoka kwenye ibada zao, waalimu, wafanyakazi wa ngazi za chini, mapolisi, manesi na watumishi wengine utabainisha mwenyewe.
Yesu anasema Ukwelu utawaweka huru.
Itaendelea tolea lijalo.
$ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $ $: