MaxShimba
JF-Expert Member
- Apr 11, 2008
- 35,772
- 4,054
Tukio la kusikitisha limeibua hofu, simanzi na maswali ya kila aina baada ya kudaiwa madaktari wa hospitali ya Temeke kuruhusu mazishi ya mapacha wawili...kabla ya mmoja wa kuzinduka muda mfupi kabla ya hajazikwa.
Mtoto huyo, ambaye hadi anataka kuzikwa alikuwa na umri wa siku moja, alishangaza wazikaji baada ya kuonyesha dalili za uhai wakati akiandaliwa kuwekwa kaburini.
Alikuwa bado anapumua na baadaye akaonyesha kufungua macho, kitendo kilichostua wazikaji na kuamua kumkimbiza Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Watoto hao mapacha ni walizaliwa na mama aitwaye Aisha Jabir, mkazi wa Mbagala ambaye alipelekwa hospitalini hapo Jumamosi ya juzi kwa ajili ya matibabu.
Baadaye mama huyo alilazwa na saa 11:00 alfajiri ya jana alijifungua mapacha hao, na inadaiwa kuwa madaktari walisema watoto hao walifia tumboni mwa mama yao kabla ya kuzaliwa.
"Baada ya kupata maelezo kutoka kwa watalaam wa afya, tulianza kushughulikia taratibu za mazishi na ilipowadiwa saa 3:00 asubuhi, tukaenda chumba cha mochwari na kuchukuwa miili ya watoto na kuelekea Charambe kwa mazishi," alisema mtoa taarifa.
"Ndugu yangu!!!,katika maisha yangu sijawahi kukutana na tukio la aina hii, tulichimba kaburi moja kwa ajili mazishi yao na tukiwa makaburini tukaanza shughuli za mazishi na baada ya kumweka mtoto mmoja kaburini, tukamfunua wa pili ili tumvishe sanda, kabla ya kumweka shimoni ndipo tukabaini kuwa yu hai." Alisema mtoto huyo alipofunuliwa alionekana anapumua na baada ya kupigwa mwanga wa jua akafumbua macho.
"Siwezi kusema kilichotea baada ya hapo, isipokuwa tulimkimbiza Hospitali ya Temeke kwa matibabu zaidi huku mmoja ambaye alishafariki dunia akazikwa," alisema. Baada ya kufikishwa Temeke, madaktari waliamua apelekwe Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Chanzo: Alasiri
Mtoto huyo, ambaye hadi anataka kuzikwa alikuwa na umri wa siku moja, alishangaza wazikaji baada ya kuonyesha dalili za uhai wakati akiandaliwa kuwekwa kaburini.
Alikuwa bado anapumua na baadaye akaonyesha kufungua macho, kitendo kilichostua wazikaji na kuamua kumkimbiza Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Watoto hao mapacha ni walizaliwa na mama aitwaye Aisha Jabir, mkazi wa Mbagala ambaye alipelekwa hospitalini hapo Jumamosi ya juzi kwa ajili ya matibabu.
Baadaye mama huyo alilazwa na saa 11:00 alfajiri ya jana alijifungua mapacha hao, na inadaiwa kuwa madaktari walisema watoto hao walifia tumboni mwa mama yao kabla ya kuzaliwa.
"Baada ya kupata maelezo kutoka kwa watalaam wa afya, tulianza kushughulikia taratibu za mazishi na ilipowadiwa saa 3:00 asubuhi, tukaenda chumba cha mochwari na kuchukuwa miili ya watoto na kuelekea Charambe kwa mazishi," alisema mtoa taarifa.
"Ndugu yangu!!!,katika maisha yangu sijawahi kukutana na tukio la aina hii, tulichimba kaburi moja kwa ajili mazishi yao na tukiwa makaburini tukaanza shughuli za mazishi na baada ya kumweka mtoto mmoja kaburini, tukamfunua wa pili ili tumvishe sanda, kabla ya kumweka shimoni ndipo tukabaini kuwa yu hai." Alisema mtoto huyo alipofunuliwa alionekana anapumua na baada ya kupigwa mwanga wa jua akafumbua macho.
"Siwezi kusema kilichotea baada ya hapo, isipokuwa tulimkimbiza Hospitali ya Temeke kwa matibabu zaidi huku mmoja ambaye alishafariki dunia akazikwa," alisema. Baada ya kufikishwa Temeke, madaktari waliamua apelekwe Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Chanzo: Alasiri