Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 733
ROHO ya Stadi wa Muziki wa Bongo Flava, Suleiman Msindi a.k.a Afande Sele nusu itolewe kwa bastola, aliyokaribia kupigwa na Prodyuza, Paul Matthysse ‘P Funky'.
The Biggest IQ Paper, Ijumaa Wikienda lina tukio kamili kama lilivyonasa data kamili.Rafiki wa Afande Sele (jina linahifadhiwa), alisema kuwa tukio zima lilichukua nafasi Ijumaa iliyopita katika Studio za Bongo Records, Bamaga, Mwenge, Dar es Salaam.
Alisema, Afande alifika katika studio hizo baada ya kuweka ‘apointimeti' maalum ya kwenda kuchukua singo yake mpya aliyorekodi kwa P Funky a.k.a Majani ‘Kinywele Kimoja' siku chache kabla ya tukio.
Majani anakiri kumchapa kibao Afande lakini anakanusha kumtolea bastola kama alivyodai Sele na kunukuliwa katika media, Hapa anaelezea kisa kizima na sababu zilizomfanya amuadabishe mfalme huyo wa Rhymes wa Bongo.
Video hii hapa chini inamuonyesha P Funky ambaye ameamua kuvunja ukimya na kueleza tukio zima lilivyokuwa...
Huyu P Funky amedata kuliko kudata kwenye.....au nguvu ya "jani" ndiyo inampa kichwa??
Last edited by a moderator: