Macos
JF-Expert Member
- May 12, 2008
- 1,979
- 1,416
WANAMAZINGIRA FEKI NA UENDELEZWAJI WA VIWANJA VYA UFUKWENI ENEO LA MASAKI
Cha kushangaza kampeni chafu ati ujenzi huu utaharibu mazingira ya eneo hilo ? hivi ni kweli ? na ati waswahili watakosa sehemu ya kukoga??? Huu ni uongo kwani sehemu ile iko juu ya usawa bahari, eneo lote kutoka Seacliff mpaka Golden tulip kuna bonde kuteremkia bahari na hakuna mswahili wala mzungu anaeogelea sehemu ile!!!! Pale wapo wavuta unga na bangi na vibaka ndio mafichio yao .Hawa wanamazingira feki wanamdanganya Mkuu wa Mkoa ati waswahili watakosa sehemu ya kuogelea SIKU ZA SIKUKUU!!
Ukweli wa mambo fukwe yoyote isipoendelezwa basi mmomonyoko wake ni wa kasi zaidi.hii ipo wazi tangu wakati ule Sumaye apige marufuku kupumzika eneo la Oysterbay basi sasa hivi ile minazi ilobaki ipo ndani ya bahari!!!! Si ajabu miaka kama 10 ijao bahari hio itapiga hodi kwenye barabara .
hebu tuchukue mfano wa wazi kuna mazingira gani yaloathirika na uwepo wa Police mess pale Oystebay/Masaki ?? Ipo pale zaidi ya miaka 40 watumabie mazingira gani yameatirika zaidi ya kuizuia erosion ? kama isingekuwepo basi bahari ingekula ile eneo.
Kuna sea cliff hotel na golden tulip ubaya gani na mazingira gani yameathirika? Bali eneo limependeza na serikali pamoja na halmashari zetu zinapata kodi.
Lipo eneo ambalo mimi nadhani kweli linaharibu mazingira nalo ni Coco beach huyu kajenga banda lake bila kuzingatia uharibifu wa mazingira lakini hawa watu kimya!!! Kuna tahadhari gani pale imechukuliwa? MACHUPA YA ULEVI NA CONDOMS ZIMEZAGAA SEHEMU YA COCO BEACH !!!!!!!!!
Mbali na kuharibu mazingira ni eneo maarufu kwa uvutaji bangi na kubwia unga .lakini hawa watu wa mazingira kimyaaaaa
Unajua serikali ya awamu ya tatu iliuza nyumba za serikali na nyngi zipo Masaki na Oystebay na haw ndio wanaopiga kelele , kisa nyumba nyingi hizi zimegeuzwa store za pombe..tena nje..na hawa watu wamazingira hapa sio ishu .leo ukipita maenea haya utadhani upo maeneo uwanja wa fisi..pita tu usiku utajionea .hawa wanaogopa kuanguka biashara zao za pombe .
Tuangalie mfano wa mji wa zanzibar sio mbali
Zaidi ya miaka 300 ndio hapa palijengwa Zanzibar !!! mji unapendeza na bahari inapendeza ..hakuna mazingira yalioathirika..
Na tuangalie London .Thames River ilivojengwa??? Unafikiri kama hawakuendeleza fukwe hizi leo london yote ingemegwa na maji
Angalieni Zanzibar,Manahattan pale nenda Hongokong .Dubai .na sehemu nyingi amabazo miji yao imejengwa maeneo ya bahari hakuna hii sheria ya kutojenga mita 60 kutoka ufukweni .watalaam wetu wamesoma lakini wanatia aibu kutunga sheria pofu kama hii Mungu ametupenda kutupa bahari .lakini uchoyo umetupofua .
Angalia chini jinsi Zanzibar walivoendeleza Beach area yao?? Hapa sio ulaya ni Forodhani park Zanzibar.
Mambo mengi ya nchi hii hayendi kwa kuwasikiliza watu ambao wana uchoyo na wabinafsi..hawajali maslahi ya nchi watu hawa huwa na visingizio kibao wanapo pinga kitu cha maendeleo ..
Huu mji unahitaji maeneo kama haya ya forodhani ya zanzibar pale Oysterbay .ili watoto wapate sehemu ya kweli kupumzika wakati wa sikukuu NA SIO SEHEMU ISOKUA NA MIPANGILIO ZAIDI YA KUWEKA ULEVI KILA SEHEMU .lakini pia serikali itapata kodi
Mimi nampa 5 Mzee Mwinyi watu wanasema alikua mpole lakini alifanya maamuzi ya kweli na busara ..na yanayozingatia maslai ya nchi alipo ruhusu ujenzi wa hotel ya Sheraton wakati ule ,sasa Movernpick ..Walikuwepo watu kama hawa wa Masaki .kupinga na kila sababu za kijinga..chambilicho Nyerere watu kama hawa hakusita kuwaita wajinga wajinga
Cha kushangaza hata gazeti la daily news limeingia katika mtego huu wa kupinga kuendeleza mji
Pia alitoa kibali ujenzi wa Golden tulip..ipo pale na watu wanaoshi Masaki kama yupo aloathirika aseme ..pia aliruhusu Seacliff kujengwa .mbali maeneo mengi ya Kawe najamngwani beach..Whitesands,Water world, Kunduchi water park ..
Walipinga sana watu hawa lakini hakuwasikiliza ..alijua wanasumbuliwa na choyo.sio wakweli hawana utafiti wa kitaalaam unaonesha uharibifu utao tokea
Point yangu ni kwamba faida kwa taifa ni kubwa zaidi kama maeneo yale yataendelezwa..yakichwa basi hakuna zaidi ya kutumiwa na wabwia unga .
Na ni wakati wa Rais kutoa kibali na amri kuendeleza hayo maeneo na utaratibu ufanywe eneo la oysterbay mpaka cocobeach ligeuzwe Park kama forodhani Zanzibar hapa chini jionee
Hii ni beach ya forodhani sio .pengine
Hata sehemu ya watoto ipo beach!!!..hapa ni zanzibar