Ortello Business Company (OBC) kuongezewa muda kinyemela Loliondo?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,442
113,452
Kuna tetesi nimeisikia mahali, kuhusu uwezekano wa Kampuni ya Uwindaji ya Ortello Business Company (OBC), kuongezwa kinyemela mkataba wa umiliki wa vitalu vya Uwindaji huko Loliondo.

Mkataba wake wa awali unakwishwa tarehe 31/Dec/2010 at 23:59 Hrs, EAT.

Kwa sasa kampuni hiyo imeanza underground lobbying kuiolobby Halmashauri husika, kuvishawishi vijiji husika kuiomba serikali kuiruhusu kampuni hiyo kuendelea na mkataba wake ili kukamilisha kazi nzuri inayofanywa na kampuni hiyo kwenye huduma za jamii kwenye vijiji husika.

Hivi karibuni, nilishuhudia full pages spread za matangazo ya jinsi Ortello Business Company (OBC) ilitumia mapesa kede kede kuboresha huduma za jamii kwa kuonyesha fedha ilizotumia na huduma zilizopatikana zikiambatana na picha mbalimbali za baadhi ya huduma hizi.

Samahani kwa kutosema source ya tetesi hii, ila huu ni muda muafaka kwa kale ka inzi ka Mzee Mwanakijiji, kakaingia tena kazini, unless yajitokeze mambo ya uwezeshaji.

Naomba kuwasilisha.
 
Watanzania wataweza tu kupumua na kuwa salama siku watakapolikataa na kulitupilia mbali hili genge la wezi na walafi wanaoifilisi na kuitafuna taifa kama mchwa, CCM.
 
Nasikia zile BMW X-5 za Ikulu zimehongwa na jamaa wa kampuni hii. Kama Kikwete atapewa muda mwingine wa kutawala hawa jamaa wataendelea kupeta kwenye sovereignty yao ya Loliondo.
Jasusi, zile X-5 ni kazi ya Mzee wa Noble Motors. Alijaribu kwa Mkapa, akampiga offer ya 7-Series ili Ikulu iachane na S-Class, Mkapa akamgomea, JK kaingia line
 
Jasusi, zile X-5 ni kazi ya Mzee wa Noble Motors. Alijaribu kwa Mkapa, akampiga offer ya 7-Series ili Ikulu iachane na S-Class, Mkapa akamgomea, JK kaingia line

Tabia hizi za kupokea kila unachopewa zinaonesha jinsi huyu rais alivyo wa ajabu na low class. Kama ikulu inataka magari si zoezi la kupiga simu tu kwa mtengenezaji na gari zinakuja? Hizi njaa za 20% zinaaibisha taifa
 
Tabia hizi za kupokea kila unachopewa zinaonesha jinsi huyu rais alivyo wa ajabu na low class. Kama ikulu inataka magari si zoezi la kupiga simu tu kwa mtengenezaji na gari zinakuja? Hizi njaa za 20% zinaaibisha taifa
Si kuliabisha taifa tu, kuliweka hatarini pia. Si ajabu magari ya rais yanaharibikaharibika hovyohovyo barabarani
 
Tabia hizi za kupokea kila unachopewa zinaonesha jinsi huyu rais alivyo wa ajabu na low class. Kama ikulu inataka magari si zoezi la kupiga simu tu kwa mtengenezaji na gari zinakuja? Hizi njaa za 20% zinaaibisha taifa
Siyo hiyo tu, rafiki yangu pale Kempiski kanidokeza kuwa tajiri mwenye hoteli humletea rais suti zilizoshonwa nje ya nchi. Wanaenda kuzichukua pale wafanyikazi wa Ikulu. Ndiyo maana hujamwona Mwungana akivaa suti moja mara tatu.
 
I believe this year we will make some changes in this country so even if the contract was extended Slaa will cancel it. as he will have that power....
 
Kuna tetesi nimeisikia mahali, kuhusu uwezekano wa Kampuni ya Uwindaji ya Ortello Business Company (OBC), kuongezwa kinyemela mkataba wa umiliki wa vitalu vya Uwindaji huko Loliondo.

Mkataba wake wa awali unakwishwa tarehe 31/Dec/2010 at 23:59 Hrs, EAT.

Kwa sasa kampuni hiyo imeanza underground lobbying kuiolobby Halmashauri husika, kuvishawishi vijiji husika kuiomba serikali kuiruhusu kampuni hiyo kuendelea na mkataba wake ili kukamilisha kazi nzuri inayofanywa na kampuni hiyo kwenye huduma za jamii kwenye vijiji husika.

Hivi karibuni, nilishuhudia full pages spread za matangazo ya jinsi Ortello Business Company (OBC) ilitumia mapesa kede kede kuboresha huduma za jamii kwa kuonyesha fedha ilizotumia na huduma zilizopatikana zikiambatana na picha mbalimbali za baadhi ya huduma hizi.

Samahani kwa kutosema source ya tetesi hii, ila huu ni muda muafaka kwa kale ka inzi ka Mzee Mwanakijiji, kakaingia tena kazini, unless yajitokeze mambo ya uwezeshaji.

Naomba kuwasilisha.

Tuletee orodha ya makampuni yote yenye vitalu vya kuwinda huko badala ya kupick hao waarabu tu? mbona wazungu umewaacha? Pasco udini unakutafuna!
 
Tuletee orodha ya makampuni yote yenye vitalu vya kuwinda huko badala ya kupick hao waarabu tu? mbona wazungu umewaacha? Pasco udini unakutafuna!

KANDA2

Ni vema kujibu tu hususani kitu ambacho hukijui, mara nyingine ni vema kunyamaza au kuliza,,, na nina amnini haupo Tz na wala hujui lolote kuhusu hii kambuni ya Ortello,,,hata kama ingekuwa ya wazungu, wahindi hata Myamwezi,,,vitendo vilivyofanywa na hawa wakolini wa kiarabu kwa WAMASAI wa LOLIONDO si vya kibinadamu hata kidogo, watu wamepoteza maisha, wamechomewa nyumba, mazingira yanaharabiwa, wanyama wanaibiwa na kupelekwa sehemu mbalimbali duniani bila idhini ya wahusika, hawa waarabu wakija msimu wa kuwinda ni vitendo vya Umalaya, na Ufirahuni mkubwa wanafanya, walipewa hili eneo kama zawadi na MWINYI, taratibu hazikufuatwa,,,sasa nashangaa unapokurupuka na kuanza kuwatetea kisa waswalina wenzako,,,,shame on you na uswalina wako
 
KANDA2

Ni vema kujibu tu hususani kitu ambacho hukijui, mara nyingine ni vema kunyamaza au kuliza,,, na nina amnini haupo Tz na wala hujui lolote kuhusu hii kambuni ya Ortello,,,hata kama ingekuwa ya wazungu, wahindi hata Myamwezi,,,vitendo vilivyofanywa na hawa wakolini wa kiarabu kwa WAMASAI wa LOLIONDO si vya kibinadamu hata kidogo, watu wamepoteza maisha, wamechomewa nyumba, mazingira yanaharabiwa, wanyama wanaibiwa na kupelekwa sehemu mbalimbali duniani bila idhini ya wahusika, hawa waarabu wakija msimu wa kuwinda ni vitendo vya Umalaya, na Ufirahuni mkubwa wanafanya, walipewa hili eneo kama zawadi na MWINYI, taratibu hazikufuatwa,,,sasa nashangaa unapokurupuka na kuanza kuwatetea kisa waswalina wenzako,,,,shame on you na uswalina wako

kwa kweli hili suala la loliondo lina sikitisha saana, sijui katiba mpya ina semaje kuhusu raisi kujiamulia mwenyewe kukodisha au kutoa sehemu kwa muwekezaji au rafiki, halafu baada ya muda tutawaambo viongozi wa siasa au dini kuomba watu wadumishe amani, wakati wateketezaji wakubwa wa amani nchi hii ni yule tunaye mchagua na kiumlipa vizuri.
 
..... Kampuni ya Uwindaji ya Ortello Business Company (OBC),...

Wapo wanaosema kuwa hii siyo kampuni bali "a sham or mere a facade concealing the truth facts".

Kama uki-pierce or lift the veil of corporate personality, utajua nini kinaendelea.

Kenya outlawed big game hunting in 1978.

But Tanzania says that hunting is the best use of the land and wildlife.

Really? Kwa kuwafukuzia mbali local people?

Maasai fury as plan to lure Arabian Gulf tourists threatens their ancestral land | World news | The Observer
 
Kuna tetesi nimeisikia mahali, kuhusu uwezekano wa Kampuni ya Uwindaji ya Ortello Business Company (OBC), kuongezwa kinyemela mkataba wa umiliki wa vitalu vya Uwindaji huko Loliondo.

Mkataba wake wa awali unakwishwa tarehe 31/Dec/2010 at 23:59 Hrs, EAT.

Kwa sasa kampuni hiyo imeanza underground lobbying kuiolobby Halmashauri husika, kuvishawishi vijiji husika kuiomba serikali kuiruhusu kampuni hiyo kuendelea na mkataba wake ili kukamilisha kazi nzuri inayofanywa na kampuni hiyo kwenye huduma za jamii kwenye vijiji husika.

Hivi karibuni, nilishuhudia full pages spread za matangazo ya jinsi Ortello Business Company (OBC) ilitumia mapesa kede kede kuboresha huduma za jamii kwa kuonyesha fedha ilizotumia na huduma zilizopatikana zikiambatana na picha mbalimbali za baadhi ya huduma hizi.

Samahani kwa kutosema source ya tetesi hii, ila huu ni muda muafaka kwa kale ka inzi ka Mzee Mwanakijiji, kakaingia tena kazini, unless yajitokeze mambo ya uwezeshaji.

Naomba kuwasilisha.

Pasco tunakuomba utupe update ya hii thread yako, watu wasije fikiria nawe umepewa suit zako uaka ka kimya baada ya kuwalipua.
 
humu
Haya sasa Waziri Kagasheki anathibitisha haya.
Mkuu Dingishwayo, watu humu jf mna kumbukumbu balaa!, nilikuwa siikumbuki tena hii kitu!. Mwanzo ilikuwa ni kwa waarabu, sasa serikali ya CCM, imeuza kila kitu kwa Wachina kwa bei ya bure kabisa!, kwa kisingizio cha mkopo nafuu wenye riba ya 01% per annum, with 20 years grace period and 80 year's repayment period!, hivyo total time ni mkopo wa riba rahisi ya asilimia 01% kwa miaka 100!, hivyo at the end of the day, tutalipa 100% interest!.

Mungu Ibariki Tanzania CCM itawale milele!,

Pasco.
 
Back
Top Bottom