BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,006
Date::9/10/2008
Orodha ya vigogo Benki Kuu katika kashfa ya EPA waongezeka
Claud Mshana na Ramadhan Semtawa
Mwananchi
ORODHA ya maafisa wa Benki Kuu Tanzania (BoT), waliong'olewa kutokana na kushindwa kuwajibika hadi kulitia taifa hasara katika kashfa ya Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), ndani ya Benki Kuu (BoT), sasa imefikia sita.
Kuongezeka kwa kigogo huyo kumekuja wakati tayari maafisa wengine watano wakiwa wameng'olewa kutokana na tuhuma hizo za kushindwa kuwajibika katika kashfa hiyo ya udokozi wa zaidi ya Sh 133bilioni zilizokuwa zikizagaa kwenye akaunti ya EPA.
Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu alithibitisha hilo wakati akizungumza katika Mahojiano Maalumu na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1).
Hata hivyo, Profesa Ndulu baadaye alifafanua kwamba, afisa huyo mwingine pia muda wake wa kustaafu ulikuwa umekaribia.
Profesa Ndulu alitumia fursa hiyo kusisitizia umma kwamba, BoT katika mchakato wake, haimwonei mtu.
Tayari Profesa Ndulu amekuwa akitoa kauli hiyo mara kwa mara kila alipozungumza na Mwananchi kuhusu tuhuma za kwamba mchakato huo umekuwa ukitoa kafara maafisa wa kati huku vigogo wa juu zaidi wakiachwa.
Akizungumzia maafisa wote sita, Profesa Ndulu alisema waliitwa na kuhojiwa na pia walipewa nafasi ya kujitetea, na kuongeza kuwa kati ya hao, wanne wamekata rufaa kupinga adhabu hiyo.
Hata hivyo, Profesa Ndulu aliwataka Watanzania kuachana na uvumi na tabia ya kuwazushia tuhuma za EPA watu ambao hawana hatia, akisisitiza kuwa mtu yeyote ana haki ya kukata rufaa iwapo hakuridhika na maamuzi yoyote yaliyofikiwa dhidi yake.
Kuhusu taasisi hiyo na halisi ilivyo baada ya uamuzi huo wa kung'oa maafisa hao, alisema, BoT ipo imara na inaendelea na utendaji wake wa kazi ikiwa imejipanga vizuri katika kuhakikisha inafanya mambo yake kwa umakini na kuhakikisha masuala ya EPA hayajirudii tena.
Katika kuhakikisha hayo, Profesa Ndulu alisema, BoT imeandaa mikakati mbalimbali ikiwapo kuhakikisha suala la utawala bora, uwazi na usimamizi ulio mkubwa katika akaunti zake.
Alipoulizwa kuhusu ugumu katika kupatikana kwa fedha za EPA zilizohamishiwa nje ya nchi, Profesa Ndulu aliweka bayana kwamba, suala hilo lipo nje ya uwezo wa BoT kwani wenye mamlaka ya kufuatilia fedha hizo ni vyombo vya usalama vya ndani ya nchi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya kimataifa.
Kuhusu akaunti ya hifadhi ya fedha za kigeni zilizopo Benki Kuu ambako kumekuwa na wasiwasi kuwa hazitoshi, Gavana Ndulu aliwatoa hofu wananchi na kuwahakikishia fedha hizo za kigeni zinatosha kwa kuzingatia vigezo vinavyofahamika kimataifa.
Akifafanua hilo alisema, hadi sasa zinafikia zaidi ya dola 2milioni za Kimarekani kiasi ambacho ni mara kumi ukilinganisha na mwaka 1995.
Profesa Ndulu alisema, thamani ya shilingi ya Tanzania pia imekuwa ikiongezeka japo si kwa kiasi kikubwa, ukizingatia kwa kipindi kirefu shilingi hiyo imekuwa ikiporomoka mara kwa mara.
Ufisadi katika EPA, ambao bado unaendelea kuitikisa BoT, ulitokana na ukaguzi uliofanywa na Kampuni ya Ernst &Young. Awali, ukaguzi huo ulifanywa na Kampuni ya Deloitte & Touche ya Afrika Kusini, lakini ikasitishwa.
Orodha ya vigogo Benki Kuu katika kashfa ya EPA waongezeka
Claud Mshana na Ramadhan Semtawa
Mwananchi
ORODHA ya maafisa wa Benki Kuu Tanzania (BoT), waliong'olewa kutokana na kushindwa kuwajibika hadi kulitia taifa hasara katika kashfa ya Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), ndani ya Benki Kuu (BoT), sasa imefikia sita.
Kuongezeka kwa kigogo huyo kumekuja wakati tayari maafisa wengine watano wakiwa wameng'olewa kutokana na tuhuma hizo za kushindwa kuwajibika katika kashfa hiyo ya udokozi wa zaidi ya Sh 133bilioni zilizokuwa zikizagaa kwenye akaunti ya EPA.
Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu alithibitisha hilo wakati akizungumza katika Mahojiano Maalumu na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1).
Hata hivyo, Profesa Ndulu baadaye alifafanua kwamba, afisa huyo mwingine pia muda wake wa kustaafu ulikuwa umekaribia.
Profesa Ndulu alitumia fursa hiyo kusisitizia umma kwamba, BoT katika mchakato wake, haimwonei mtu.
Tayari Profesa Ndulu amekuwa akitoa kauli hiyo mara kwa mara kila alipozungumza na Mwananchi kuhusu tuhuma za kwamba mchakato huo umekuwa ukitoa kafara maafisa wa kati huku vigogo wa juu zaidi wakiachwa.
Akizungumzia maafisa wote sita, Profesa Ndulu alisema waliitwa na kuhojiwa na pia walipewa nafasi ya kujitetea, na kuongeza kuwa kati ya hao, wanne wamekata rufaa kupinga adhabu hiyo.
Hata hivyo, Profesa Ndulu aliwataka Watanzania kuachana na uvumi na tabia ya kuwazushia tuhuma za EPA watu ambao hawana hatia, akisisitiza kuwa mtu yeyote ana haki ya kukata rufaa iwapo hakuridhika na maamuzi yoyote yaliyofikiwa dhidi yake.
Kuhusu taasisi hiyo na halisi ilivyo baada ya uamuzi huo wa kung'oa maafisa hao, alisema, BoT ipo imara na inaendelea na utendaji wake wa kazi ikiwa imejipanga vizuri katika kuhakikisha inafanya mambo yake kwa umakini na kuhakikisha masuala ya EPA hayajirudii tena.
Katika kuhakikisha hayo, Profesa Ndulu alisema, BoT imeandaa mikakati mbalimbali ikiwapo kuhakikisha suala la utawala bora, uwazi na usimamizi ulio mkubwa katika akaunti zake.
Alipoulizwa kuhusu ugumu katika kupatikana kwa fedha za EPA zilizohamishiwa nje ya nchi, Profesa Ndulu aliweka bayana kwamba, suala hilo lipo nje ya uwezo wa BoT kwani wenye mamlaka ya kufuatilia fedha hizo ni vyombo vya usalama vya ndani ya nchi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya kimataifa.
Kuhusu akaunti ya hifadhi ya fedha za kigeni zilizopo Benki Kuu ambako kumekuwa na wasiwasi kuwa hazitoshi, Gavana Ndulu aliwatoa hofu wananchi na kuwahakikishia fedha hizo za kigeni zinatosha kwa kuzingatia vigezo vinavyofahamika kimataifa.
Akifafanua hilo alisema, hadi sasa zinafikia zaidi ya dola 2milioni za Kimarekani kiasi ambacho ni mara kumi ukilinganisha na mwaka 1995.
Profesa Ndulu alisema, thamani ya shilingi ya Tanzania pia imekuwa ikiongezeka japo si kwa kiasi kikubwa, ukizingatia kwa kipindi kirefu shilingi hiyo imekuwa ikiporomoka mara kwa mara.
Ufisadi katika EPA, ambao bado unaendelea kuitikisa BoT, ulitokana na ukaguzi uliofanywa na Kampuni ya Ernst &Young. Awali, ukaguzi huo ulifanywa na Kampuni ya Deloitte & Touche ya Afrika Kusini, lakini ikasitishwa.