ORIGINAL imechakachuliwa.

cheusimangala

JF-Expert Member
Feb 27, 2010
2,585
497
Hili neno ORIGINAL naona wabongo wameamua kulichakachua.Ninamaanisha kwamba,mara nyingi utasikia mtu anakwambia nenda duka fulani wale wanauza lace wig au brazillian hair original.

Kusema ukweli mim naona kama wadada wengi wakibongo hawajui wanachokiongea hasa kwenye maswala ya vipodozi,nywele na human hair.
Vitu kama MAC make ups,brazillian hair na designer pieces kama nguo viatu na mabegi vinapendwa sana na wadada wa kibongo sababu wamesikia viko juu na watu wenye pesa zao wanavitumia hivyo na yeye anapokua navyo anajiona yuko juu.

Ila ukweli ni kwamba hivi vitu vyote mtu ukinunua bongo ni fake,copy kutoka china na thailand.Kama hizo nywele nyingi zinakua zina quality nzuri na zinaonekana kama real human hair lkn ni fake,mtu huwezi kununua brazilian hair ya kutosha kichwa kizima ya ukweli kwa laki 3,watu tunatoa hadi milion mbili kwa hizo nywele za ukweli halafu mtu anakupitia na vya kwake vimekakamaa anakwambia ni original,how come.

Unakuta mtu kavaa loubs kanunua elfu themanini za kikwete anadai ni original.

Ila sio wadada tu hata mabrazameni,wanashobokea sana vitu vyenye majina lkn ni aibu mtu kapiga mtisheti wa YSL mbwembwe nyingi halafu hata bila kuulizwa atakwambia original hii nimenunua elfu sittini,za kikwete,hii si aibu jamani,maana yaani unajua tu kaka wa watu hata hajui ukubwa wa hilo jina fake alilovaa.

Mi naona ni vizuri kuacha kusema copy za big brands kuwa ni original wakati zimefyatuliwa hapo Thailand.Vile vile kwenda na fasheni sio lazima kuvaa big names wakati uwezo wa kupata original haupo,kuliko kuvaa immitations huku wanaojua vya ukweli vikoje wakitusanifu ni bora kuvaa vitu ambavyo havina majina lkn ni vizuri.

Kama hujaipenda mada yangu gonga like.
Kama umeipenda usinipe like.

Love u all.
 
lol subiri mashorobaro na masistaduu watoke mlimani city..........................................!
watakukomesha.............................!
 
duh..umenikumbusha wimbo fulani...

"Cheusimangala usibadili mwendo huo, mangala eee mangala eee binti afurika
 
Ngoja wahusika waje, bz mi vitu vyangu navichukuliaga pale Tengeru j5 na jmosi alfajirii na mapema ila ukinikuta kwa mtaa utadhani nimevin'golea pale Manhattan NY.
 
Hakuna red bottoms za alfu themanini za Kitanzania. Asemaye zake kazinunua kwa bei hiyo basi atakuwa bonge la mshamba maana huko ni kujichoresha tu.

si ndio maana mi nikasema ni aibu sababu mtu mjanja kama hana hela ya kununua kitu cha designer cha ukweli utamuona akivaa nguo za kawaida tu anazomudu ambazo ziko nzuri tu na watu wanavaa na wanapendeza.
Sasa aibu ni pale mtu kavaa igizo halafu anaamini kabisa kuwa kanunua original,bora kuna wale anavaa fake lkn anajua hii ni fake lkn wabongo wengi ni original kama kanunua desh desh butique iliyoko namannga na anajua fake ni zile za kariakoo.
 
Ngoja wahusika waje, bz mi vitu vyangu navichukuliaga pale Tengeru j5 na jmosi alfajirii na mapema ila ukinikuta kwa mtaa utadhani nimevin'golea pale Manhattan NY.

aminia mkuu huo ndo ujanja,kupendeza sio kugharamia pesa mingi upangiliaji wako tu.Kuna watu wanavaa mitumbo na wanapendeza ile mbaya.Unakuta mtu kavaa tisheti ina nembo kuubwa ya gucci,angalia shingo ya hiyo tisheti ilivyovutika sasa.
 
nimepotea njia, . . .ila wacha tu niulize maana kuuliza si ujinga ingawa ni ushamba, loubs ndo nini mwanadafada?

hivi kweli aliyepotea ana muda wa kuuliza maswali,we ungeuliza njia ningekujibu ila nikikujibu hilo swali lako nitazidi kukupoteza mwishowe ushindwe kurudi kwenu na mie sitaki wakimbizi kwenye uzi wangu.
 
mkuu erick si useme ukweli tu kuwa hapa ndo una feel at home la sivyo tusingokuona hapa.
Ingia kwenye friji kuna juice yako tumekubakizia upooze koo.
Teh siunajua hapo umetumaliza aisee...lol
Nimekosa la kusema...
Ila nemekuja kugundua vitu vingi huwezi jua ni original fake au original ya ukweli...
 
cheusi, akijidanganya mwenyewe kuna shida gani? Au inakuuma wewe ambaye umetumia zaidi ya $1,200 kununua hizo nywele za mbrazil na wote mkaonekana mbele ya kina Kongosho (ambao ni wengi) mko sawa?
 
cheusi, akijidanganya mwenyewe kuna shida gani? Au inakuuma wewe ambaye umetumia zaidi ya $1,200 kununua hizo nywele za mbrazil na wote mkaonekana mbele ya kina Kongosho (ambao ni wengi) mko sawa?

my love mtu ambaye kwa mfano ameshawahi kuwa na hermes bag ya kweli akiiona feki yake hata ikiwa umbali wa hatua tatu mbele ataijua tu,ambao watadhani kuwa mim niliyena kitu changu cha ukweli wakadhani ni sawa na kile cha mtu aliyenunua feki watakua ni wale ambao hawajawahi kuona cha ukweli kilivyo.Haya mabegi au viatu vya madesinger wakubwa vinatofauti nyingi na copy zake,mfano zile nyuzi tu wanazotumia kushonea viatu au mapochi unakuta jinsi zinavyoingia na kutoka zinakua zina idadi ambayo kila pochi ya aina hiyo ina idadi sawa nayo na alama nyingine nyingi.
Hivyo sijaandika sbb roho inaniuma kuwa nitaonekana sawa na wa fake,na sina shida mtu kuvaa fake,bali tu nimeona ni vizuri mtu ukivaa fake ujue ni fake,kuliko kuvaa fake halafu ukapita ukisema kwa kujiamini kuwa ni original sbb fake inajulikana tu.
Yaani kama tunavyofundishana kupaka wanja,japo kila mtu ana uhuru wa kupaka wanja wake atakavyo,sio mbaya pia kufundishana kuepeuka aibu kwa kuvaa fake bila kujua ni fake.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom