Kapo Jr
JF-Expert Member
- Jan 31, 2011
- 996
- 280
Wana Jf, kutokubali kukosolewa ndiyo kinachopelekea yanayojiri kipindi hiki baada ya waumini wa kiislamu kuanzisha taasisi tofauti(UAMSHO na jumuiya ya kiislamu),taasisi hizi zimekuwa zikivunja sheria za nchi kama vile uchomaji makanisa bila kuchukuliwa hatua na serikali, waliosema udhaifu wa mkuu wa nchi unadhirishwa kwa yanayojiri kwani amani iko mbioni kutoweka. Wazalendo walipoonya waliomadarakani walipinga vikali nadhani kwa tukio la waislamu kukusanyika kwenda ikulu ni ishara tosha kuacha mara moja kulindana kiudini,rais ni wa uma wote na si dini hata anayoabudu,itoshe sasa 'kidole kinaelekea jichoni' ,watawala wachukue hatua madhubuti kulinda amani ya Tanzania.Wameanza waislam,je wakristo wataendelea kuvumilia uchomwaji makanisa kama serikali haitochukua hatua kuzuia hayo?Nawasilisha jamvini