Losambo
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 2,612
- 864
Wanajamvi,
Kwa muda kidogo nimekuwa nikifuatilia jukwaani na kuona au kusikia kuwa katibu mwenezi wa CCM Nape Nauye amezindua operation ijulikanayo kama Vua Gamba, Vaa Uzalendo akiwa mkoa Kagera kwa shughuli za chama.
Kiukweli nilibaki na maswali mengi ambayo naomba wanajamvi akiwepo Nape mnisaidie.
1.0 Ile operation ni ya kichama au ni ya mtu binafsi yaani Nape? Kwa nini? Nifahamuvyo mimi operation kubwa kama hizo ni lazima zifanyike kitaifa au ziwe na sura ya umoja wa kichama na si mtu mmoja mmoja.
Mf. CDM walipozindua operation yao M4C Arusha ilikuwa na sura ya kichama kwa maana maandalizi na hata uzinduzi wake ulilenga kuwajulisha umma nini maana ya M4C n.k
Lakini hilo sijaliona katika operation inayodaiwa kuanzishwa na Nape. Je hili linahalarisha ile kauli ya kuwa Nape anakifanya chama kama mali yake? Anaweza akaamka na kuja na operation yoyote bila ya Mkama au mwenyekiti wake kujua?
2.0 Ikiwa Vua Gamba, Vaa Uzalendo ni operation ya kichama basi itakuwa imekidhalilisha sana Chama Cha Mapinduzi? Kwa nini? Chama cha Mapinduzi ni chama kikongwe hivyo hakiwezi kufanya mambo yake kienyeji namna ile!!!! Kimantiki kama Nape hakutumwa na Chama inapaswa achukuliwe hatua kali ikiwemo karipio la maandishi kwa kufanya mambo kienyeji yaani bila mawasiliano (Networking)
3.0 Hata kama ni programme ya kichama bado CCM itakuwa imekosa ubunifu kwa kuiga kutoka CDM. Kama wao walipaswa kuja na programme tofauti ambayo itakuwa na manufaa kwa chama hasa katika kipindi hiki cha kupigana kubaki madarakani au kuondoka!!!! Mwanzo mbaya unaashiria mwishilizo mbaya.
Naomba nihitimishe kwa kuomba nifahamishwe juu ya sintofahamu ya Vua Gamba, Vua Gwanda Vaa Uzalendo.
Kwa muda kidogo nimekuwa nikifuatilia jukwaani na kuona au kusikia kuwa katibu mwenezi wa CCM Nape Nauye amezindua operation ijulikanayo kama Vua Gamba, Vaa Uzalendo akiwa mkoa Kagera kwa shughuli za chama.
Kiukweli nilibaki na maswali mengi ambayo naomba wanajamvi akiwepo Nape mnisaidie.
1.0 Ile operation ni ya kichama au ni ya mtu binafsi yaani Nape? Kwa nini? Nifahamuvyo mimi operation kubwa kama hizo ni lazima zifanyike kitaifa au ziwe na sura ya umoja wa kichama na si mtu mmoja mmoja.
Mf. CDM walipozindua operation yao M4C Arusha ilikuwa na sura ya kichama kwa maana maandalizi na hata uzinduzi wake ulilenga kuwajulisha umma nini maana ya M4C n.k
Lakini hilo sijaliona katika operation inayodaiwa kuanzishwa na Nape. Je hili linahalarisha ile kauli ya kuwa Nape anakifanya chama kama mali yake? Anaweza akaamka na kuja na operation yoyote bila ya Mkama au mwenyekiti wake kujua?
2.0 Ikiwa Vua Gamba, Vaa Uzalendo ni operation ya kichama basi itakuwa imekidhalilisha sana Chama Cha Mapinduzi? Kwa nini? Chama cha Mapinduzi ni chama kikongwe hivyo hakiwezi kufanya mambo yake kienyeji namna ile!!!! Kimantiki kama Nape hakutumwa na Chama inapaswa achukuliwe hatua kali ikiwemo karipio la maandishi kwa kufanya mambo kienyeji yaani bila mawasiliano (Networking)
3.0 Hata kama ni programme ya kichama bado CCM itakuwa imekosa ubunifu kwa kuiga kutoka CDM. Kama wao walipaswa kuja na programme tofauti ambayo itakuwa na manufaa kwa chama hasa katika kipindi hiki cha kupigana kubaki madarakani au kuondoka!!!! Mwanzo mbaya unaashiria mwishilizo mbaya.
Naomba nihitimishe kwa kuomba nifahamishwe juu ya sintofahamu ya Vua Gamba, Vua Gwanda Vaa Uzalendo.