Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Salam wadau,
Kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam hasa pande za Kigamboni na maeneo ya jirani, kesho kutakuwa na mkutano wa hadhara utakaofanyika Vijibweni na kuhutubiwa na makamanda kadhaa kutoka Makao Makuu pamoja na majimbo jirani na Kigamboni.
Pamoja na shughuli za kuimarisha Chama lakini pia wananchi watapata fursa ya kuzungumza na viongozi wetu juu ya masuala mbalimbali ya kijamii yanayowasibu yanayohitaji msukumo wa kipekee ili kufanikisha utekelezaji wake. Bila shaka suala la malipo kwa wananchi wanaotakiwa kuhama kupisha mji mpya wa kigamboni na wale wanaotakiwa kuhama kupisha upanuzi wa bandari, ambao kwa bahati mbaya serikali imeshindwa kuwalipa stahiki zao ili wahame yatakuwa ni mojawapo ya mambo yatakayojitokeza, kwani kwa takribani miaka minne wananchi wale wameshindwa kufanya shughuli yoyote ya kimaendeleo wakisubiri kulipwa stahili zao.
Shughuli itaanza saa nane kamili mchana.
Kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam hasa pande za Kigamboni na maeneo ya jirani, kesho kutakuwa na mkutano wa hadhara utakaofanyika Vijibweni na kuhutubiwa na makamanda kadhaa kutoka Makao Makuu pamoja na majimbo jirani na Kigamboni.
Pamoja na shughuli za kuimarisha Chama lakini pia wananchi watapata fursa ya kuzungumza na viongozi wetu juu ya masuala mbalimbali ya kijamii yanayowasibu yanayohitaji msukumo wa kipekee ili kufanikisha utekelezaji wake. Bila shaka suala la malipo kwa wananchi wanaotakiwa kuhama kupisha mji mpya wa kigamboni na wale wanaotakiwa kuhama kupisha upanuzi wa bandari, ambao kwa bahati mbaya serikali imeshindwa kuwalipa stahiki zao ili wahame yatakuwa ni mojawapo ya mambo yatakayojitokeza, kwani kwa takribani miaka minne wananchi wale wameshindwa kufanya shughuli yoyote ya kimaendeleo wakisubiri kulipwa stahili zao.
Shughuli itaanza saa nane kamili mchana.