Open relationships....do they work?

EJM_

JF-Expert Member
Jul 8, 2011
3,836
2,091
Hivi hizi open relationships huku kwetu zina work?

kunahaja sasa kwa wapenzi kuwa na uhusiano wa wazi maana yake kila mtu awe free kuwa na mtu mwengine ila awe na nidham kwa mwenzi wake wa kudum akihitajika basi awajibike ipasavyo nadhani itapunguza ukali wa wivu wa kijinga katika mahusiano kwa asilimia 70 je unafikiri itasaidia?

Habarini wanaJF. Nimeshangaa kuona kwenye FB wabongo wengi wanaweka kwamba wako kwenye open relationship na wanaiona ni hype au fashion flani. Hata kuna wengine eti wanapewa hongera/ likes moving from relationship to open relationship...

Je, open relationship ina maana gani au ni mimi nimekuwa nikielewa maana tofauti....

Nawasilisha.
 
Musimo jr.......before concluding kuwa zina au hazi work hebu tueleze ndo zikoje? kanuni zake ni zipi hizo relationship za wazi. Sie wengine wa longi jamani ni hutu tukozi tufupi twa kompyuta ndo tumetukutanisha na JF
 
M1,asante nami natatizika na hako kaaina ka mauhusiano,tafadhali Mkuu sana Musimi jr....tupe shule tafadhali ili tujue nini tunachochangia,Heshima,
Don.
 
Sababu ya wivu mara nyingi huwa zinaishia kwenye ugomvi.. (lakini mkuu nisikujibie wewe unaweza ukakaa na mtu na ukawa hauna neno yeye akitembea na mtu mwingine..?, kama unaweza basi tafuta anaeweza mkae wote) Lakini angalizo utajikuta una-fall in love na kawivu kanaanza kukutembelea

Open relationships:- Uhusiano ambao partners wanakubaliana kudate/sleep na watu wengine..
 
VoS aksante, je hizi relationship zinakuwa kwenye ngazi ya Uboyfriend na ugalfriend tu yaani sio hata kkwenye ndoa halali?
MWe!! Aksante MUNGU kwa kunileta zamani!
Wenzetu hata kwenye ndoa halali wanakaribisha partners wengine (hawa wanaitwa swingers) badala ya kucheat nyuma ya mgongo wa mwenzako yaani wanaalikana wote na kuendelea na shughuli.., tena hawa jamaa huwa wana parties kabisa ambapo couples wote (yaani swingers) wanabadilishana partners na kuendeleza orgies... (yes I know ni kweli yataka moyo)..
 
Mwanajamii, The last Don
Open relationships ni zile ambazo hazina sifa nyingi za relationships za kawaida. Kwa mfano, watu wanakubaliana kutooneana wivu, wanaweza ku date watu wengine na huwa zinaweza kuvunjika muda wowote hata bila taarifa. Mara nyingi zinaunganishwa na kitu kimoja tu "NGONO"
 
Aksante kiongozi VoR kwa kutujuza maana ya hiyo Uhusiano,..lakini nina maswali bado yananitatiza kiasi nashindwa kutoa mchango wangu kwa mwenye uzi huu,..Hivi hiyo aina ya mahusiano ipo katika jamii yetu hii hii, au ndio kale kale ka nyumba ndogo mkuu,kwa maana kama mimi niko katika ndoa then mpango kando unajua kabisa mimi nipo full kwa nyumba kubwa lakini kapo tayari kudate nami na kama ndio aina hii ya uhusiano mbona kama vile hiyo makubaliano yapo upande mmoja tu? au ni hii ni kitu ingine kiongozi naomba unifahamishe manake naonage inshu nyingine ni kama zina apply kwenye tv mkuu.Heshima,
Don.
 
Ohh mkuu sana Musimo nimekupata sasa,kumbe mahusiano ya wazi ni yale ambayo wahusika wanatakana kwa ngono tu..hapo powa no wivu kabisa kwa ukweli....maana hakuna kufikiria kuhusu wat next...hiyo mkuu haina shida nadhani...ni sawa sawa na mtu ambaye atakuwa anaenda kununua ngono kwa mtu mmoja kila siku kiasi ambacho wanakuwa marafiki wazuri tu,only katika kusaidiana kila mtu na shida yake mmoja pesa mwingine ngono.
 
TLD, kwenye ndoa pia mahusiano haya yapo hasa pale inapofikia hatua ya watu kufika kikomo cha mapenzi. But wanabaki kuunganishwa vitu vingine kama watoto ama vingine, ingawa reference nyingi za hili zinatoka huko ughaibuni
 
hakuna cha relationship hapo ni ushenzi tu, unasemaje mtu ana uhusiano na wewe tena wa kimapenzi harafu ana........
 
Nadhani kitu kimoja ambacho wachangiaji wa mada hii wamekubaliana ni kwamba hiili ni jambo la tamaduni za kigeni na sio za kiTz kama ambavyo tunafahamu. Mambo ya swingers, four-some , three -some sex parties ambazo wahudhuriaji wanabadilisha wenza kwa tendo la ngono usiku kucha na biashara zote zinaishia hapo..Ole wako uchukue namba ya simu ya mtu aliyekufurahisha..utakuwa umevunja mapatano ya party husika.

Lakini tukipekua tamaduni zetu na tukaenda kwa baadhi za jamii za kimasai, kimeru na Kalenjin huko Kenmya tunakuta wana namna ya mahusuano ya wazi.. ( Kumradhi niliwatolea mfanoi...nimetonywa na watu wa maeneo hayo. mwanamume anavizia mume wa mwanamke aliye na mahusiano ya siiri akitoka tu- yeye anajiwahi na kusimika mkuki nje ya nyumba au boma wakati anajivinjari na huyo mke wa mtu na mwenye mali akijirudi kabla ya "karamu" haijaisha na kuona mkuki umesimikwa anamezea na kupotelea mbali kutoa muda wa majeruhi ili "karamu" iiishe. Na akiirudi maisha yanendelea bila hoja ya kilichotokea... Nadhani ni mila za zamani ambazo pengine zilikuwa maana kwa wakati ule lakini kwa jamiii ya sasa ya kiTz ni kinyume cha maadili ya utamaduni wa kitaifa kwa sasa na kwakweli kwa maadili yetu ni changamoto kubwa kuzifuata kuliko kuzikataa KWA SABABU HAZIFANYI KAZI
 
Ndugu yangu hayo mambo wazungu naomba kwa dhati kabisa kuwa tuwaachie tu hao wazungu na ninaomba yasifike huku kwetu jamani!
Jamani jamani hii Dunia ina mambo ya ajabu kweli kweli na ni aibu hata kuyaongelea manake ni aibu tupu na ni balaa tupu jamani! Tumekwishi hiki kizazi cha nyoka.
 
Ashadii,
Umewahi kujaribu kuwa kwenye aina hii ya relationship?
 
Jada Pinkett na Will Smith wana Open Relationship
Demi Moore na Ashton Kutcher wana Open Relationship
Megan Fox na Brian Austin Green wana Open Relationship
Angelina Jolie na Bradd Pitt wana Open Relationship
 
Back
Top Bottom