Oooh!!! poor Geita!!!

Ntumami

Senior Member
Sep 3, 2010
127
23
for the fisrt time this week I arrived in Geita, ni sehem ambayo ina mgodi mmoja mkubwa sana wa dhahabu na ni moja ya migodi mikubwa sana Africa kwa jinsi ninavyojua, pamoja na huo kuna migodi midogomidogo mingi sana lakini Geita ni kati ya miji iliyo na miundombinu mibovu ya mahitaji muhimu kwa wakazi wake. Geita maji ni ya shida sana!, barabara pekee yenye lami ni ile itokayo Mwanza kuelekea Bukoba, zaidi ni vumbi kali! ukifika nyarugusu sehemu ambayo pia ni maarufu kwa wachimbaji wadogowadogo ni inasikitisha sana nyumba za kudumu [block au matofali ya kuchoma] ni chache mno! zaidi nasikia eneo hilo ni linatishiwa na kipindupindu cha mara kwa mara!

for sure nimesikitika sana kuona Geita ilitakiwa iwe mbali sana kimaendeleo, na sijui lini watapata kufaidi matunda ya dhahabu iliyotoka na inayotoka hapa kwao! na tena hata baadhi ya maeneo unakuta mashimo tu yaani mabaki ya kulikochimbwa dhahabu lakini huoni imefanya nini!! sanasana kingine nimekiona Geita ni wingi wa wageni hapa maana hapa hata Gesti japo zipo nyingi sana lakini kupata ni hadi uwahi mapema sana! sometimes i fail to understand if hawa watu wapo Geita zaidi kibiashara au kuna tusichokijua? pia maisha ya hapa kiasi fulani ni ghali!!

kero nyingine ni kutofikiwa kwa umeme kwa maeneo mengi ya wilaya hii!!! ukiacha Geita mjini na Kasamwa sijaona sehemu nyingine yenye umeme, na tena kwa taarifa nilizopewa ni mgodini na kata hizo chache ndizo zeenye umeme!!!



oooo por Geita!! i never thought you could be this poorest rich!! or poor millionaire... so sorry.... jamani i may fail to explain it but IMENIUMA SANA KUOONA ILIVYO!!!
 
Poor geita,,njoo tupabadilishe mkuu,,na ni kati ya miji ambapo mzunguko wa pesa ni mkubwa sana.
 
Ufukara na dhiki wanajitakia wananchi wenyewe kwa kuiweka ccm madarakani miaka nenda rudi!! Ngoja wateseke hadi hapo watakapopata akili!!!
 
Ufukara na dhiki wanajitakia wananchi wenyewe kwa kuiweka ccm madarakani miaka nenda rudi!! Ngoja wateseke hadi hapo watakapopata akili!!!

uliambiwa CDM wakiingia madarakani ndio watajenga Hiyo Geita
 
Kama mawazo yako yanakuambia chama ndicho kinabadili maisha yako kalagabaho,utabaki hivo hivo hata kama obama akiongoza tz


Ufukara na dhiki wanajitakia wananchi wenyewe kwa kuiweka ccm madarakani miaka nenda rudi!! Ngoja wateseke hadi hapo watakapopata akili!!!
 
Back
Top Bottom