MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,562
Mafundisho yako mazuri sana Jethro ila yanataka moyo. Mwenzangu uwe unanyamaza tu, akirudi usiku nyamaza, akija amelewa nyamaza, akilala nje nyamaza, na hata akikuletea UKIMWI nyamaza. Ndio ndoa ah!!FL1,
Kwanza wataka kuniambia ndoa ina formula?
2nd hilo tukio ni zito sana ni si yameanza leo na nina uhakika FL1 umeisha yashuhudia baadhi ya mambo kutoka kwa jirani yako kama kweli mwakaaa uziio mmoja na hilo lililo tokea jana ni lakushangaza.
Katika ndoa kunahitajika mawasiliano mazuri na yaumakinifu kati ya m'me na mke, na kwaupande wa hao waliogombana wamelilea hilo tatizo muda mrefu yani mpaka yafikia hatua ya mke kupigwa na kufukuzwa ndani ya nyumba? kuna jambo kubwa sana hapo yapaswa wazazi au marafiki wakaribu wao washirikishwe pia.
Lafu FL1 huyo dada anapaswa akuambie ukweli wa mambo usikute nae huwa anakiburi cha kujifanya anajua sana pale alezwapo kitu nakujibu haraka haraka na kuja juu, au humkalipia mumewe pindi achelewapo kurudi nyumbani"Ulikuwa wapi au ulikuwa kwa mahawara zako, ooh we endelea tu kwanza umeisha lewaaa!!,na hao marafiki zako ivi kweli hamjui kama mna wake majumbani?hao marafiki zako wnakusaidia nini baba naniii!!" kwa style hiyo kweli kwa mwanaume mwenye hasira lazima tu atampiga mkewe au kunasa vibao.
Ningependa tu kumshauri huyo dada pindi tu pale watakapo resolve hilo tatizo ajaribu kushuka chini na kuwa mkimya tu wala asimfuatilie mumewe kiivyo yeye akae zake kimya tu mume karudi usiku we uchune, kakuulizi habari za watoto mjibu vyema tuu, hata simu yake ikiita mwamnbie simu inaita na wala usirukie simu yake pindi katoka job.
Nakwambia huyo mumeo atajishtukia siku na kujirudi mwenyewe bila kupenda.maana ataanza kuhisi huyu wife vipi sio kama zamani au kuna serengeti boyz nini mbona kabadirika.